Skip to main content

Posts

Showing posts from July 31, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

MKUU WA MKOA WA MARA APOKEA MWENGE WA UHURU KUTOKA MKOA WA SIMIYU

 Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ameupokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Annamringi Macha katika Uwanja wa Shule ya Msingi Balili, Halmashauri ya Mji wa Bunda.  Akitoa taarifa kwa kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndugu Wazo Michael Mwang'onda Mhe. Mtambi amesema ukiwa katika Mkoa wa Mara Mwenge wa Uhuru utakimbizwa katika kilomita 996 na utatembelea miradi ya maendeleo 63 yenye thamani ya shilingi bilioni 174.  Aidha, Mhe. Mtambi amewakaribisha wananchi wa Mkoa wa Mara na maeneo jirani kushiriki katika hafla ya Mwenge wa Uhuru kuwasha Mwenge wa Mwitongo itakayofanyika tarehe 02 Agosti, 2026 Nyumbani kwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Mwitongo Butiama.  Leo Mwenge wa Uhuru unakimbizwa katika Halmashauri ya Mji wa Bunda na baadae katika Halmashauri zote za Mkoa wa Mara hadi tarehe 09 Agosti, 2026 na tarehe 10 Agosti, 2026 utakabidhiwa Mkoa wa Mwanza kuendelea na mbio zake.  Kauli mbiu ya...

CHATANDA: RAIS SAMIA NI MUUMINI MZURI WA MEZA YA MAZUNGUMZO

 NA: MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Taifa, Mary Chatanda, amesema Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Taifa, ni muumini mzuri wa kutumia meza ya mazungumzo kujadili na kufikia muafaka wa masuala mbalimbali ya kimaendeleo. Chatanda ameyasema hayo, kufuatia kumalizika kwa mazungumzo baina ya Rais Dk. Samia na viongozi wa vyama 18 vya siasa, Julai 30, 2026, Ikulu, Jijini Dar es Salaam. Chatanda amesema, mazungumzo ya pamoja baina ya serikali na viongozi wa vyama vya siasa ni muhimu katika kuimarisha umoja na mshikamano. "Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ni muumini mkubwa wa meza ya mazungumzo. Katika meza hiyo, mengi yanajadiliwa kuliko kutumia mitandao ya kijamii kulalamika. Kimsingi, serikali imepokea ushauri kutoka kwa viongozi wa vyama vya siasa, na hapa kama taifa tunapata mawazo chanya ya kujenga na hivyo tunaimarisha umoja na mshikamano wetu," amesema. Katika hatua nyingine, Chatanda amesema,...

TRA KARIAKOO YATOA ELIMU YA MABADILIKO YA KODI KWA WAFANYABIASHARA

NA: MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM Kufuatia mabadiliko ya sheria za kodi kwa mwaka wa fedha 2026/2027, Mamkala ya Mapato Tanzania (TRA), imetoa elimu na mafunzo ya kuwajengea uwezo wafanyabiashara na walipakodi ili kuwa na uelewa wa pamoja wa masuala ya kodi. Mafunzo hayo yameratibiwa na TRA mkoa wa kikodi wa Kariakoo, Julai 30, 2026, Jijini Dar es Salaam. Katika mafunzo hayo, Meneja wa Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, CPA Paul Walalaze, amesema miongoni mwa mabadiliko ya sheria za kodi ni pamoja kutoa msamaha wa kodi kwa muda wa miezi 12 (mwaka mmoja) kwa mfanyabiashara mpya ambaye mauzo yake kwa mwaka hayazidi shilingi milioni 200. "Serikali imesikia kilio cha wafanyabiashara wapya ambao wanaanza bishara zao. Katika mabadiliko haya, mfanyabiashara mdogo anayeanza biashara ambaye mauzo yake kwa mwaka hayazidi shilingi millioni 200, atapata msamaha wa kodi katika kipindi cha miezi 12 tangu aliposajiliwa," amesema Walalaze. Aidha, amesema mfanyabiashara anapoanza kufanya shughuli za...

DC ITUNDA AWASHUSHA BODABODA MBEYA, AWAPA MCHONGO WA PESA NA ULINZI

 Na Mashaka Mhando, Mbeya VIWANJA vya Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) Mkoa wa Mbeya vilitikiswa na shangwe na nderemo kufuatia mkutano mkubwa uliowakutanisha maelfu ya madereva wa bodaboda na bajaji wa Jiji hilo ana kwa ana na Mkuu wao wa Wilaya, Mhe. Solomon Itunda kuzungumzia amani na utulivu. Mkutano huo, ambao ulitawaliwa na hali ya kirafiki na maelewano, haukuwa tu wa kutoa maagizo, bali ulikuwa ni jukwaa la kimkakati la kuwakumbusha vijana hao nafasi yao nyeti katika uchumi na usalama wa Jiji la Mbeya. Akizungumza huku akishangiliwa na umati huo, Mhe. Itunda aliwaeleza madereva hao ukweli usiofichika kuwa wao ni injini muhimu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa mustakabali wa nchi.  Alisema kutokana na asili ya kazi yao ya kukutana na mamia ya wananchi kila siku, wana nguvu kubwa ya kujenga au kubomoa taswira ya jiji katika sekta ya usafiri kwa kuwaeleza tofauti na uhalisia wa nchi inavyoendeshwa. Hivyo, Mkuu huyo wa Wilaya, ambaye amekuwa akisifika na wananchi wa M...

MAHAKAMA KUU YAPANGA KIKAO CHA AWALI CHA SHAURI LA UHAINI LA LISSU

 Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, imepanga kufanya kikao cha awali cha maandalizi ya usikilizwaji wa Shauri la Uhaini Na. 19605/2025 linalomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Antiphas Lissu. Kwa mujibu wa waraka rasmi uliotolewa Julai 31, 2026 na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, H. S. Mushi, kikao hicho cha awali (Pre-Session Meeting) kitafanyika Agosti 5, 2026 kuanzia saa nane kamili mchana kwa njia ya mtandao kupitia Masjala Ndogo ya Mahakama Kuu, Dar es Salaam. Mahakama imeeleza kuwa lengo la kikao hicho ni kujadili maandalizi muhimu yatakayowezesha usikilizwaji wa shauri hilo kufanyika kwa ufanisi kabla ya kuanza rasmi kwa mwenendo wa kesi. Aidha, usikilizwaji wa shauri hilo umepangwa kuanza Agosti 10, 2026 na unatarajiwa kuendelea hadi Septemba 7, 2026, kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Mahakama. Waraka huo umeelekezwa kwa Mkuu wa Mashtaka wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Mkoa wa Dar es Salaam, Mkuu wa Gereza Kuu la Ukonga na ...

RAIS SAMIA APATA MAPOKEZI MAKUBWA NCHINI ANGOLA

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Quatro de Fevereiro Luanda, tarehe 31 Julai, 2026, kwa ajili ya Ziara ya Kikazi ya siku mbili nchini Angola, kufuatia mwaliko wa Rais wa nchi hiyo Mhe. João Manuel Gonçalves Lourenço.