Skip to main content

Posts

Showing posts from September 5, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

WAZIRI MKUU ATOA MAELEKEZO UENDESHAJI MRADI SGR

WAZIRI MKUU ATOA MAELEKEZO UENDESHAJI MRADI WA SGR *_Ataka huduma ziboreshwe na usimamizi wa miundombinu uimarishwe_*   WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameitaka Wizara ya Uchukuzi iendelee kulisimamia kwa karibu Shirika la Reli Tanzania (TRC) na kuhakikisha huduma za treni ya SGR zinaboreshwa na miundombinu inaimarishwa ili mradi huo uweze kudumu kwa muda mrefu Amesema katika mwaka wa fedha 2024/2025, Serikali itaendeleza sekta ya uchukuzi ambapo pamoja na mambo mengine itasimamia sekta ya reli ikiwemo ujenzi wa SGR na uendeshaji wa treni ya kisasa ya abiria kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa tarehe 31 Desemba, 2023 Mheshimwa Dkt. Samia Suluhu Hassan alielekeza kuanza uendeshaji wa reli ya SGR kwa kipande cha Dar es Salaam - Dodoma ifikapo mwezi Julai, 2024.   Ameyasema hayo leo (Septemba 6, 2024) wakati wa kuahirisha Mkutano wa 16 wa Bunge, jijini Dodoma. “Naomba kulitaarifu Bunge lako tukufu kuwa, safari za treni ya mwendokasi kutoka Dar es Salaam...

Rais Dkt. Samia Ashiriki na Kuhutubia Mkutano wa FOCAC

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki na kuhutubia katika Mkutano wa Ngazi ya Juu unaohusu Ukuaji wa Viwanda na Kilimo cha Kisasa Afrika kwenye Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha China mjini Beijing, tarehe 5 Septemba, 2024.

Ujumbe wa SUMA JKT Watembelea Miradi ya Kimkakati Comoro

Brig. Jen. PE Ngata, Mkurugenzi Mtendaji kutoka Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMA JKT) ambaye yuko katika ziara ya kikazi nchini Comoro ametembelea Mradi wa Kilimo (CRDE) MITSAMIHOULI. Akiwa kituoni hapo, Brig. Jen. Ngata ameonesha nia ya kushirikiana na kituo hicho katika kuimarisha uzalishaji wa mazao mbalimbali.  Kituo cha CRDE Mitsamihouli kinajihusisha na utafiti wa mazao ya mizizi, na Ufugaji.  Sambamba na ratiba hiyo, Brig. Jen. Ngata alipata nafasi ya kutembelea kijiji cha Hantsindzi Mboimkuu na kukagua mradi wa ujenzi wa Barabara ya kijijini ambayo Kampuni ya SUMA JKT inaendelea na majadiliano ya zabuni ya ujenzi wa barabara hiyo.  Mradi huo unatarajiwa kuwa kazi ya kwanza kutekeleza na Kampuni ya SUMA JKT nchini Comoro.  Mapema siku hiyo, Brig. Jen. Ngatta na Ujumbe wake walitembelea Kampuni ya Ujenzi ya SCPMC inayoendelea na ujenzi wa majengo ya Kiutawala katika Uwanja wa Mpira Mitsamihouli.  Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiy...

Mongella Aanza Ziara Mkoa wa Shinyanga

  Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, John Mongella, leo tarehe 05 Septemba 2024 ameanza ziara ya siku saba mkoani Shinyanga.  Lengo kuu la ziara hii ni kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM ya 2020-2024, kuimarisha uhai wa chama, na pia kusikiliza changamoto zinazowakabili wananchi wa mkoa huo. Mongella, ambaye ni mlezi wa chama mkoani Shinyanga, anatarajiwa kufanya mikutano ya ndani na hadhara, pamoja na vikao na watumishi wa chama na jumuiya zake.  Katika ziara hiyo, atatembelea maeneo ya Shinyanga Mjini, Shinyanga Vijijini, Kahama, Msalala, Kishapu, na Ushetu, ambapo atakutana na viongozi na wananchi kujadili namna bora ya kuimarisha utekelezaji wa sera za chama kwa maendeleo ya mkoa huo. Kupitia ziara hii, Mongella anatarajiwa pia kuhamasisha wanachama wa CCM kushiriki kikamilifu katika shughuli za chama na kuwa mstari wa mbele katika kutatua kero zinazowakabili wananchi.  Ziara hii ni sehemu ya mikakati ya CCM ya kuhakikisha inaendelea kuwa karib...

Fahamu Jinsi Umeme wa Solar na Uoteshaji wa Mbegu Kwenye Kitalu Unavyosaidia Katika Kilimo Cha Tija

  Na Emmanuel Chibasa Katika jamii ya wakulima wadogo wadogo, matumizi ya kilimo cha umwagiliaji ni mbinu muhimu kwa ajili ya kukuza mazao ya mboga mboga na matunda. Hata hivyo, wakulima wengi wanakabiliwa na changamoto kutokana na mbinu wanazotumia. Kwa mfano, baadhi yao wanapanda mbegu moja kwa moja shambani, huku wengine wakipendelea kuotesha kwenye kitalu kabla ya kuhamishia miche shambani. Kwa mujibu wa wizara ya kilimo, sekta ya kilimo kwa mwaka 2023 ilikua kwa asilimia 4.2 ikilinganishwa na ukuaji wa asilimia 3.3 mwaka 2022 huku ikito ajira kwa wananchi kwa wastani wa asilimia 65.6 na kuchangia asilimia 65 ya malighafi za viwanda. Licha ya uwepo wa hekta 727,280.6 za kilimo cha umwagiliaji na serikali kuweka mazingira wezeshi kwa wakulima wadogo kuendesha shughuli zao za kilimo kwa kutumia wataalam pamoja na upatikanaji wa vifaa vya nishati ya umeme jua(solar) lakini bado wakulima wadogo wanakabiliwa na changamoto katika kilimo cha tija. Habari hii inachunguza faida na athar...