Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini(TAKUKURU) imefanikiwa kuokoa zaidi ya shilingi Millioni Mia Saba kwenye utoaji wa Mikopo ya Asilimia kumi ya mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji la Mwanza kwa mwaka wa fedha 2024/2025. Taasisi hiyo imeokoa shilingi Millioni 706.2 kutokana na Uhakiki na Udhibiti uliofanyiia kwenye utoaji wa Mikopo ya Vikundi vya wanawake,vijana na watu wenye ulemavu inayotokana na asilimia kumi ya mapato ya ndani ya Halmashauri hiyo. Kaimu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Mwanza Protas Henry amesema kuwa katika Uhakiki huo,Vikundi 41 ambavyo Mikopo yake ilikuwa na Thamani ya Millioni Mia Saba havikukidhi vigezo. Vikundi hivyo vilibainika kuwa na Makosa mbalimbali ikiwemo Kuomba mkopo hewa,kuwasilisha kwa kamati vielelezo vya kughushi mfano Profoma invoice na kuwasilisha Mikataba ya uongo ya maeneo ya kufanyia biashara,kuwasilisha bei za Juu za vifaa kuliko bei ya soko,kutokuwa na maeneo ya kufanyia biashara pamoja na Kuomba mkopo kwa ajili ya...
Marato tv - Sauti ya Jamii