DAR ES SALAAM, AGOSTI 14, 2026 Watanzania, kampuni, taasisi na watoa huduma wenye uwezo na sifa stahiki wamehimizwa kuchangamkia fursa mbalimbali za zabuni zilizotangazwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kuelekea maandalizi na uendeshaji wa Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON2027). Akitoa taarifa hiyo leo jijini Dar es Salaam, Katibu wa Kamati ya Ndani (LOC), Neema Msitha, amesema CAF imetangaza fursa mbalimbali za zabuni zinazohusiana na maandalizi na uendeshaji wa mashindano yake, ikiwamo AFCON 2027, ambayo Tanzania itaandaa kwa kushirikiana na Kenya na Uganda. “LOC inawahimiza Watanzania wenye uwezo, sifa na nia ya kushiriki fursa hizi kufuatilia matangazo rasmi ya zabuni hizo kupitia tovuti ya CAF ambayo ni https://www.cafonline.com/inside-caf/about-us/tenders/tenders-tab/ ili kusoma masharti ya kila zabuni na kuwasilisha maombi yao kufuatana na taratibu na muda uliowekwa na shirikisho hilo” amesisitiza Msitha. Amesema fursa hizo zinahusisha maeneo mbal...
Marato tv - Sauti ya Jamii