Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Visiwa vya Comoro Mheshimiwa Saidi Yakubu,februari 11 Mwaka huu amekutana na kufanya Mazungumzo na Ujumbe maalumu kutoka Serikali ya Comoro unaoshughulikia azma ya nchi hiyo kuimarisha biashara ya bidhaa za chakula. Ujumbe huo uliongozwa na Bw. Snehal SONEJI, Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo ya Umoja wa Mataifa nchini Comoro. Washiriki wengine kwenye Mazungumzo hayo ni Dkt. Hamza A. Azali, Mamlaka ya Utafiti wa Kilimo, Mazingira na Uvuvi (INRAPE), na Bw. Abdillahi M'Saidie, Rais wa Jumuiya ya Wafugaji, Wakulima, Wavuvi na Sanaa nchini Comoro. Ujumbe kutoka Serikali ya Comoro ulijulisha kuwa ulitembelea Tanzania wiki ya kwanza ya mwezi Februari, 2025 ambapo walibahatika kukutana na kufanya mazungumzo na watendaji kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, kukutana na Ushirika wa Uzalishaji katika Chuo cha Kilimo cha SOKOINE, pamoja na kutembelea miradi ya kilimo. Kufuatia mazungumzo yao, Taasisi za Tanzania zimeon...
Marato tv - Sauti ya Jamii