Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule, ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Dodoma na Watanzania kwa ujumla kujitokeza kwa wingi kushiriki Marathon ya TARI itakayofanyika Agosti 2, 2026, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 10 ya Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI). Mhe. Senyamule ameyasema hayo mara baada ya kutembelea banda la TARI na kukabidhiwa jezi za marathon hiyo, ambapo alieleza kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo anatarajiwa kuwa Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo. Amesema marathon hiyo inalenga kuhamasisha afya, kuunganisha wadau wa sekta ya kilimo na kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu mchango wa TARI katika utafiti na maendeleo ya kilimo nchini. Amesema hadi sasa zaidi ya washiriki 1,000 wamekwishajisajili, huku akiwahimiza wananchi wengine kuendelea kujisajili ili kushiriki mbio hizo zitakazoanzia eneo la Nzuguni saa 2:00 asubuhi. Marathon hiyo itakuwa na mbio za kilomita 5, 10 na 21, ili kutoa nafasi kwa makundi mbalimbali ya washiriki. K...
Marato tv - Sauti ya Jamii