Skip to main content

Posts

Showing posts from August 9, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

DC MSOFE ATOA ONYO KALI KYERWA: ‘TUKIUUA MNADA, TUNAUA BEI YA KAHAWA'

 Na Angela Sebastian,Kyerwa MKUU wa Wilaya ya Kyerwa, Zaitun Msofe, amewataka madiwani wa Halmashauri ya Wilaya hiyo kuongeza nguvu katika kudhibiti magendo ya kahawa na mianya yote inayosababisha Halmashauri kukosa mapato, akisema vitendo hivyo vinadhoofisha uchumi wa Wilaya na Taifa kwa ujumla. Msofe alitoa agizo hilo jana wakati akizungumza katika kikao cha Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa, kilichojadili utekelezaji wa shughuli za robo ya nne ya mwaka wa fedha 2025/2026. Alisema Kyerwa ipo katika msimu wa biashara ya kahawa, zao ambalo ni tegemeo kubwa kwa wakazi wa Wilaya hiyo na chanzo muhimu cha mapato ya Halmashauri, hivyo madiwani wanapaswa kufuatilia kwa karibu biashara zinazoendelea katika kata zao na kuhakikisha wafanyabiashara wanatimiza wajibu wa kulipa ushuru. “Tuko katika kipindi cha msimu wa biashara hii ambayo tunaitegemea sana Kyerwa katika kukusanya mapato,Kahawa ndiyo zao kubwa tunalolitegemea hapa kwetu hivyo madiwani nawakumbusha kuwa wapo...

MSIGWA DAM DAM NA YANGA SIKU YA MWANANCHI 2026

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Bw. Gerson Msigwa, ameshiriki katika Tamasha la Siku ya Mwananchi 2026 (Yanga Day) lililofanyika Agosti 9, 2026 katika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam. Katika tamasha hilo, Bw. Msigwa alishiriki katika mchezo wa hisani uliowakutanisha wachezaji wa zamani pamoja na wafanyakazi wa Yanga dhidi ya timu ya wasanii wa filamu na muziki nchini. Ushiriki huo umeonesha umuhimu wa michezo katika kuwaunganisha viongozi, wanamichezo, wasanii na wananchi, huku ukitoa nafasi kwa wadau mbalimbali kutumia michezo kama chombo cha kujenga umoja, mshikamano na ushirikiano katika jamii. Tamasha la Siku ya Mwananchi 2026 limekuwa pia jukwaa muhimu la kuendeleza uhusiano kati ya sekta ya michezo, sanaa na jamii, kupitia burudani na shughuli mbalimbali zilizowakutanisha wadau na mashabiki wa Klabu ya Yanga.

MAHAKAMA YA RUFAA TANZANIA YAIPA USHINDI IPTL, PAP KATIKA MZOZO WA U$168M DHIDI YA STANDARD CHARTERED BENKI

 Na Mwandishi Wetu Mahakama ya Rufaa ya Tanzania imezipa gharama za kisheria Kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) na Pan Africa Power Solutions (T) Limited ya Dola za Kimarekani 8,000,000/- kufuatia kufanikiwa kupinga rufaa iliyokatwa na Benki ya Standard Chartered kuhusu mgogoro wa kibiashara uliodumu kwa muda mrefu wa U$168,000,000. Uamuzi huo ulitolewa Agosti 5, 2026 na Ofisa Ushuru J.E. Fovo katika kesi ya Kodi namba 65 ya mwaka 2026, iliyotokana na Rufaa ya Madai namba 386 ya mwaka 2022. Waombaji walikuwa wakiwakilishwa na Wakili Musa Mhagama, huku walalamikiwa wakiwakilishwa na Wakili Deogratias Tesha. Uamuzi huu wa hivi punde unafunga sura nyingine katika kesi ambayo imeendelea kwa zaidi ya muongo mmoja na imehusisha mahakama nchini Tanzania, Uingereza na Malaysia. Kiini cha mzozo huo kinahusiana na mikataba ya uzalishaji umeme iliyotiwa saini mwishoni mwa miaka ya 1990 na mwanzoni mwa miaka ya 2000, na mipango ya ufadhili iliyofuata ambayo ilisababisha usul...

TANZANIA: COURT OF APPEAL AWARDS USD 8M COSTS TO IPTL, PAP IN USD 168M DISPUTE AGAINST STANDARD CHARTERED

By Prosper Makene  The Court of Appeal of Tanzania has awarded USD 8,000,000 in legal costs to Independent Power Tanzania Limited - IPTL and Pan Africa Power Solutions (T) Limited, following their successful opposition to an appeal by Standard Chartered Bank over a long-running USD 168,000,000 commercial dispute. The ruling was delivered on August 5, 2026 by the Court of Appeal’s Deputy Registrar and Taxing Officer, J.E. Fovo, in Taxation No. 65 of 2026, arising from Civil Appeal No. 386 of 2022. The applicants were represented by Advocate Musa Mhagama, while the respondents were represented by Advocate Deogratias Tesha. This latest decision closes another chapter in a case that has dragged on for more than a decade and has involved courts in Tanzania, the United Kingdom, and Malaysia. The core of the dispute relates to power generation agreements signed in the late 1990s and early 2000s, and subsequent financing arrangements that led to arbitration and litigation abroad. The dispu...

GLOBAL EDUCATION LINK KUSAFIRISHA WANAFUNZI 85 KWENDA VYUO VYA INDIA

 Na Mwandishi Wetu WANAFUNZI 85 wanatarajia kwenda masomoni kwenye vyuo vikuu mbalimbali nchini India kuanzia wiki ijayo kupitia Wakala wa Elimu Nje ya Nchi Global Education Link (GEL). Wanafunzi hao na wazazi wao walihudhuria mkutano uliofanyika katika ofisi za GEL mwishoni mwa wiki kwaajili ya kupewa mafunzo ya namna ya kuishi nchini humo. Pia walielezwa mambo wanayotakiwa kufanya na wasiyotakiwa kuyafanya wakiwa masomoni nchini humo ikiwemo suala la vibali, bima na makaazi ili waweze kuhitimu masomo yao. Mbali na mafunzo hayo walipewa tiketi zao za ndege, visa na nyaraka mbalimbali zitakazowawezesha kupokelewa kwenye vyuo wanavyokwenda kusoma nchini India. Wanafunzi hao wanatarajiwa kuanza kwenda nchini India kuanzia tarehe 21 na 23 mwezi huu. Akizungumza kwenye mkutano huo wa wanafunzi na wazazi wao, Mkurugenzi Mkuu wa GEL, Abdulmalik Mollel aliwataka wanafunzi hao kusoma huku wakiangalia fursa mbalimbali ambazo zinaweza kuwasaidia wanapohitimu. “Tunahitaji GPA nzuri lakini pia...

MICHEZO NI DARASA LA USHIRIKIANO KATI YA POLISI NA JAMII – RC MTANDA

 Na Dawati la Habari Polisi;Mwanza  Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda, amempongeza Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Camillus Wambura, kwa hatua ya kuirejesha timu ya Polisi Tanzania katika Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2026/2027. Mhe. Mtanda ametoa pongezi hizo leo Agosti 9, 2026, wakati akifungua rasmi Mashindano ya Polisi Jamii Cup Kanda Namba 7 yanayofanyika katika Uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza. Amesema kurejea kwa Polisi Tanzania katika Ligi Kuu ni hatua muhimu inayopaswa kuungwa mkono, huku akisisitiza umuhimu wa michezo katika kuimarisha mahusiano kati ya Jeshi la Polisi na wananchi. “Nitumie nafasi hii kumpongeza IGP Camillus Wambura kwa hatua ya kuirejesha timu ya Polisi Tanzania katika Ligi Kuu ya NBC. Hii ni hatua nzuri na muhimu kwa Jeshi la Polisi na tunapaswa kuiunga mkono timu yetu ili iweze kufanya vizuri,” alisema Mtanda. Mkuu huyo wa Mkoa amesema michezo ni kiungo muhimu katika kujenga uaminifu, umoja na mshikamano kati ya Jeshi la Polisi na jamii, ak...

KUTOKA WIZARANI HADI JUKWAANI: MWANA FA AAMSHA DUDE MWANZA, EAST COAST TEAM YAUNGANA TENA

 Na Mashaka Mhando, MWANZA NAIBU Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma (maarufu kama Mwana FA au 'Falsafa'), ameacha historia mpya jijini Mwanza baada ya kufanya maajabu jukwaani akiungana na kundi lake la zamani la East Coast Team. Tukio hilo la kukata na shoka limejiri usiku wa Agosti 8, 2026, katika ukumbi wa Climax uliopo Rock City Mall, wakati wa Tamasha kubwa la kusherehekea Miaka 30 ya muziki wa Bongo Fleva, ambapo Mhe. Mwinjuma alihudhuria kama Mgeni Rasmi. Badala ya kuishia kutoa hotuba za kiserikali pekee, Mhe. Mwinjuma aliwapa mashabiki suprise ya kufa mtu alipopanda jukwaani na kuimba sambamba na wakali wenzake wa East Coast Team waliotikisa anga la muziki miaka ya nyuma, akiwemo Crazy GK, AY, na Snare. Muunganiko huo wa East Coast Team jukwaani uliamsha shangwe za mashabiki na kukumbusha enzi za dhahabu za muziki huo, huku Mwana FA akidhihirisha kuwa makali yake ya kuchana mistari bado yako palepale licha ya kubeba majukumu mazito ya ki...