Mfumo wa Usimamizi wa Ununuzi wa Umma Kielektroniki (NeST) umeendelea kuiweka Tanzania kwenye ramani ya dunia baada ya kutunukiwa tuzo ya kimataifa na kutambuliwa kuwa miongoni mwa mifumo 20 bora ya Serikali Mtandao duniani katika Tuzo za World Summit on the Information Society (WSIS) Prizes 2026, zilizofanyika Julai 8, 2026 jijini Geneva, Uswisi. Tuzo hiyo ilikabidhiwa kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), Bw. Dennis Simba, na Mratibu Mkuu wa Tuzo za WSIS, Bi. Gitanjali Sah, aliyemwakilisha Katibu Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Mawasiliano (ITU). Kwa mujibu wa ITU, NeST ilishinda katika kategoria ya Serikali Mtandao (e-Government), iliyoshirikisha zaidi ya mifumo 1,500 kutoka nchi 122 duniani. Mifumo hiyo ilitathminiwa kwa mchango wake katika kuimarisha uchumi shirikishi, ustawi wa jamii na maendeleo endelevu kupitia matumizi ya teknolojia. Akizungumza baada ya kupokea tuzo hiyo, Bw. Dennis Simba amesema mafanikio hayo yametokana na maono n...
Marato tv - Sauti ya Jamii