MADIWANI wa Manispaa ya Kibaha wameeleza kuwa ziara yao ya mafunzo katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya na Halmashauri ya Mji Tunduma italeta manufaa makubwa katika kuongeza mapato na kuimarisha miradi ya maendeleo ya Manispaa hiyo. Akizungumza baada ya ziara hiyo, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kibaha, Dkt. Mawazo Nicas amesema madiwani pamoja na wataalamu wa halmashauri wamepata uzoefu mkubwa kuhusu usimamizi wa mapato na uendeshaji wa vitega uchumi vinavyochangia maendeleo ya wananchi. Amesema katika Jiji la Mbeya wamejifunza namna miradi ya ujenzi wa maduka, ukumbi pamoja na maeneo ya mapumziko inavyoongeza mapato ya halmashauri na kutoa huduma bora kwa wananchi na wafanyabiashara. Kwa upande wa Halmashauri ya Mji Tunduma, Dkt. Nicas amesema wamevutiwa na mfumo wa parking za malori unaochangia mapato makubwa ya Halmashauri hiyo kutokana na shughuli za biashara mpakani mwa Tanzania na Zambia. “Tumepata mambo mengi ya kujifunza. Tumeona namna parking za malori zinavyoongeza mapato Tundu...
Marato tv - Sauti ya Jamii