Skip to main content

Posts

Showing posts from February 20, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Waziri Mhagama apongeza kiwanda pekee kinachotengeneza maji tiba nchini

  ……. Ni cha Kairuki Pharmaceuticals Industry Limited Na Mwandishi Wetu Waziri wa Afya, Jenista Mhagama, amekipongeza kiwanda cha kutengeneza maji tiba cha Kairuki Pharmaceuticals Industry Limited kilichoko Mkoa wa Pwani. Alitoa pongezi hizo jana alipotembelea kiwanda hicho kwa lengo la kujionea uzalishaji wa maji tiba na kuzungumza na mwekezaji wa kiwanda hicho. Waziri Mhagama aliongozana na viongozi mbalimbali kutoka taasisi zilizopo chini ya Wizara ya Afya pamoja na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Pwani. Waziri Mhagama alisema amefurahi kufanya ziara katika kiwanda hicho ambapo ameona namna uzalishaji maji tiba unaotumia teknolojia ya kisasa unavyofanyika. Waziri Mhagama alisema serikali inajivunia uwekezaji unaofanywa na taasisi binafsi ikiwemo Kairuki Pharmaceuticals Industry Limited. Alisema utengenezaji wa maji tiba hayo hapahapa nchini unapunguza gharama za usafirishaji pamoja na kupunguza muda wa kusubiri dawa kutoka nje ya nchi. Waziri Mhagama alisema uwekezaji uliofanywa n...

Aliyekuwa Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati Afariki Dunia

Mwenyekiti wa zamani wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) Wafula Chebukati ameaga dunia.  Chebukati alifariki jana Alhamisi jioni wakati akipokea matibabu katika hospitali moja jijini Nairobi. Alikuwa na umri wa miaka 63. Chebukati alisimamia IEBC kwa kipindi cha miaka 6 baada ya kuteuliwa kwenye wadhifa huo mwezi Januari mwaka 2017. Aliondoka kwenye wadhifa huo mwezi Januari mwaka 2023 baada ya kusimamia chaguzi tata za mwaka 2017 na 2022. Chebukati na makamishna Prof. Abdi Guliye na Boya Molu ndio pekee waliohudumu kwa kipindi cha miaka sita. Makamishna wengine ambao ni Juliana Cherera, Francis Wandera, Irene Masit na Justus Nyang’aya (maarufu kama Cherera 4) walijiuzulu kabla ya kumalizika kwa muhula wao wa kuhudumu. Wanne hao walichukua hatua hiyo kutokana na utata uliogubika uchaguzi mkuu wa mwaka 2022. Mchakato wa kutafuta mrithi na Chebukati na waliokuwa makamishna wa tume hiyo kwa sasa unaendelea. Chebukati alikuwa mwanasheria aliyejizolea tajiriba ya miaka 37 katika ...

Wilaya ya Nyamagana yazindua mikopo ya asilimia 10.

  Jumla ya shilingi Bilioni 1.3 imetolewa Kwa vikundi 87 vya wanawake,vijana na watu wenye ulemavu. Akizungumza na vikundi hivyo mkuu wa wilaya ya Nyamagana Amina Makilagi amevipongeza vikundi hivyo 87 vilivyofanikiwa kupata mkopo katika awamu hii ya kwanza na kuwataka kutumia mikopo hiyo Ili kubadili hali za Maisha yao na ya watu wanaowazunguka. "Mikopo hii ikawe na tija kwenu kwa kuendeleza biashara mlizonazo lakini pia kubadili mfumo wa maisha yenu kama ulikuwa unakula mlo mmoja Sasa ule milo mitatu"alisema Makilagi. Aidha mkuu wa wilaya Makilagi amevitaka vikundi hivyo vilivyopewa mkopo vihakikishe vinafanya marejesho kwa mujibu wa mikataba waliyosaini. "Dawa ya deni ni kulipa maana fedha hii mliyopewa sio ya kwenu peke yenu Kuna wenzenu hawajapata hivyo hakikisheni mnarudisha Ili na wenzenu waweze kukopa"alisema Makilagi Kwa upande wake mbunge wa Jimbo la Nyamagana Stanislaus Mabula ameipongeza serikali Kwa kurejesha mikopo hiyo iliyokuwa ikisubiriwa Kwa hamu k...

Mbunge Mavunde Akabidhi Mradi wa Shamba Kwa Wanawake Wafanyabiashara Wadogo Dodoma

▪️Mradi wa shamba la zabibu walenga kuwainua wafanyabiashara ▪️Wakinamama wampongeza kwa kuwainua kiuchumi ▪️Awatafutia soko la uhakika wa mazao yao ▪️Rais Samia apongezwa kwa miundombinu rafiki ya biashara kwenye masoko Na Mpunguzi,Dodoma Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini *Mh. Anthony Mavunde* amekabidhi mradi wa Shamba la zabibu kwa Wafanyabiashara Wanawake wa Masokoni (*UWAWAMA*) ikiwa ni utekelezaji wa ahadi aliyoitoa wakati wa kongamano kubwa la Wafanyabiashara wanawake wa Masokoni wakati wa mkutano ulioongozwa na Mwenyekiti wa UWT *Cde Mary Chatanda*. Makabidhiano hayo yamefanyika leo tarehe 20.02.2025 Mpunguzi,Jijini Dodoma na kuhudhuriwa na viongozi  mbalimbali wakiwemo wanachama wa UWAWAMA. “Rais Dkt. Samia S. Hassan amefanya kazi kubwa ya kujenga na kuboresha miundombinu ya masoko Jijini Dodoma kazi ambayo imechochea kukua kwa biashara na kuongezeka kwa kipato kwa   wafanyabiashara wadogo. Mradi huu wa Shamba la zabibu unategemewa kuongeza mapato na kutunisha mfuk...

Jaji aagiza Besigye arejeshwe Gerezani

  Mahakama kuu nchini Uganda imewaamuru wakuu wa gereza wamrudishe gerezani kiongozi wa upinzani Dk. Kizza Besigye ambaye pia ni mgonjwa licha ya afya yake kuendelea kudhoofika. Familia yake na mawakili wanaogopa kwamba kuendelea kuzuiliwa kwa mwanasiasa huyo mashuhuri ambaye yuko kwenye mgomo wa kususia chakula tangu wiki iliyopita kuhatarisha afya yake. Akiongea baada ya kikao cha mahakama Winnie Byanyima, mke wa Dk. Kizza Besigye alisema amesikitishwa na maagizo ya mahakama. "Nilikuja hapa nikitarajia kuondoka na Dk. Kizza Besigye kwenda naye nyumbani leo, nimeumia lakini sijashtuka. Besigye ni mateka, alitekwa nyara ”. Aliwaambia waandishi wa habari. Besigye na mshitakiwa mwenzake Hajji Obeid Lutale walikuwa wamefika mahakamani katika mji mkuu Kampala kwa ajili ya kusikilizwa kwa ombi lililoletwa na mawakili wake wakitaka kuachiliwa kwake. Hata hivyo, iliamuliwa kwamba Besigye ni mgonjwa na hakuweza kuendelea na kikao hicho. Aliamuru arudishwe gerezani ambapo ameshikiliwa kwa ...

Wasira Aihakikishia Marekani Uchaguzi Kuwa Huru Na Haki

* Azungumza na Balozi wa Cuba Nchini Tanzania.  Na Mwandishi Wetu.  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Stephen Wasira amesema kipaumbele cha Chama wakati wote ni kuhakikisha nchi inakuwa na amani. Pia, ameihakikishia kuwa uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika baadae mwaka huu, utakuwa huru na wa haki. Ndg. Wasira amesema hayo leo Februari 20, 2025 alipozungumza na Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Ndugu Andrew Lentz, aliyemtembea ofisi kwake katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam. Makamu Mwenyekiti Wasira alimweleza kaimu balozi huyo kwamba, Tanzania ni taifa linaloendelea, hivyo amani ya nchi haiwezi kuwekwa rehani. Katika mazungumzo yao, wawili hao walizungumzia uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika nchini baadaye mwaka huu, ambapo Wasira alimhakikishia Lentz kwamba utafanyika kwa uhuru na haki. Alimwambia Chama Cha Mapinduzi kinaendelea kujiandaa kushiriki uchaguzi huo na kinatarajia kushinda kwa sababu kimetekeleza ahadi za...

Mafunzo ya Watendaji CCM Rorya Yadaiwa Kuvurugwa na Mwenyekiti wa Chama na Mbunge

Na Shomari Binda MAFUNZO ya watendaji wa Chama cha Mapinduzi ( CCM) Wilaya ya Rorya yamedaiwa kuingiliwa na kuvurugwa na viongozi wa chama hicho. Viongozi wanaodaiwa kuvuruga mafunzo hayo ni mbunge wa jimbo la Rorya Jafari Wambura Chege na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Rorya Ongujo Wakibara wakidaiwa kuingilia semina ya makatibu wa matawi na kata leo  20/02/2025 na kugawa posho shilingi 50,000 kwa kila katibu. Kwa mujibu wa taarifa zilizosambaa mitandaoni ukiwa ni pamoja na group la Whassap la CCM mkoa wa Mara zimedai utaratibu huo unakiuka maelekezo  kutoka makao makuu ya chama Taarifa hiyo inadai  kuwa mafunzo hayo ya watendaji yasiingiliwe na viongozi au wanasiasa kwa sababu ni mafunzo ya kiutendaji na chama kilisema kitagharamia kila kitu ikiwemo chakula na posho. "Lengo la chama kufanya hivyo ilikuwa ni kuondoa urasimu wa wagombea kutumia nafasi hiyo kutoa rushwa kinyume chake mwenyekiti wa chama na mgombea wake ambaye ndie mbunge kwa sasa wamevamia ukumbi na kutoa pos...

NIRC yasaini mkataba wa Bilioni 17 ukarabati Skimu za Umwagiliaji bonde la Mto wa Mbu Arusha

📌NIRC, Monduli.  SERIKALI ya Awamu ya Sita ,kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), imesaini Mkataba Wa kukarabati skimu zilizopo katika bonde la Mto wa Mbu Wilayani Monduli, kwa gharama ya shilingi bilioni 17. Mradi huo unajumuisha ukarabati wa mifereji yenye urefu wa jumla ya Mita 37,484.71, sawa na urefu wa zaidi ya Kilomita 37. Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, Raymond Mndolwa, amewataka wananchi wa eneo la mradi kuwa macho dhidi ya watu wasiowaaminifu katika kipindi chote cha utekelezaji wa mradi huo.  “Mradi huu unatarajiwa kuleta mapinduzi makubwa katika sekta ya kilimo na mifugo katika bonde la Mto Wammbu, na kuondoa changamoto za muda mrefu zilizokuwepo katika jamii hizo,”amesema. Nao Wananchi wanaotoka katika kata ya Mto wa Mbu, ambapo skimu hiyo inapatikana, wamepata tumaini jipya la kuimarisha kilimo na kuondokana na migogoro kati ya wakulima na wafugaji. Wakazi hao wameishukuru serikali kwa hatua iliyofikiwa na w...

Dkt. Biteko Ateta Na Jumuiya Ya Wasambazaji Wa Mitungi Ya Gesi Nchini

  📌Awashukuru kwa mchango wao utekelezaji Mkakati wa Nishati Safi ya Kupikia 📌 Ataka LPG ipatikane kwa wingi hadi ngazi ya Vijiji 📌 Ahimiza Tanzania kuwa kitovu cha usambazaji LPG Afrika Mashariki 📌 Tanzania yaendelea kupigiwa mfano Kimataifa matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati.  Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amekutana na kufanya mazungumzo na Jumuiya ya Kampuni zinazohusika na Usambazaji wa Mitungi ya Gesi (LPG) -TZLPGA kwa lengo la kuwashukuru kwa mchango wao katika utekelezaji wa Mkakati wa Nishati Safi ya Kupikia  pamoja na kujadiliana masuala mbalimbali ikiwemo utatuzi wa  changamoto zinazoikumba TZLPGA ili kuhakikisha wanatoa huduma kwa urahisi nchi nzima. Mazungumzo kati ya Dkt. Biteko na Jumuiya hiyo yamefanyika leo Februari 20, 2025 jijini Dodoma na kuhudhuriwa na Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba pamoja Watendaji kutoka.Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma...