📌 Ampongeza Dkt. Tulia kwa ubunifu na kusaidia wahitaji 📌 Wananchi 9,000 wapata bima za afya kupitia Tulia Marathon 📌 Awashukuru wadau na wasanii kwa kushiriki Tulia Marathon Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amempongeza Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani, Mhe. Dkt. Tulia Ackson kwa mchango wake katika sekta za afya na elimu sambamba na kusaidia wahitaji jijini Mbeya. Dkt. Biteko ametoa pongezi hizo leo Mei 10, 2025 jijini Mbeya mara baada ya kukimbia mbio fupi za Tulia (Tulia Marathon) katika Uwanja wa Sokoine. “ Dkt. Tulia anafanya kazi kubwa kwenye sekta ya afya na elimu pamoja na kuwajengea nyumba watu wenye uhitaji. Zile nyumba tunazoziona anawakabidhi watu kumbe tayari kuna nyingine zimejengwa Uyole,” amesema Dkt. Biteko. Amesisitiza “ Nataka niwaambie hakuna sadaka kubwa kama kusaidia wahitaji na sisi wengine tunajifunza kupitia wewe Dkt...
Marato tv - Sauti ya Jamii