Na Angela Sebastian ;Muleba Kituo cha Kusukuma Mafuta Ghafi namba Tatu (PS3) kinachojengwa katika Kijiji cha Kikagate, Kata ya Mubunda, Wilaya ya Muleba mkoani Kagera, kimefikia asilimia 88 ya ujenzi na kinatarajiwa kukamilika mwishoni mwa Agosti au mwanzoni mwa Septemba mwaka huu. Kituo hicho ni sehemu ya Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP), unaounganisha maeneo ya uzalishaji mafuta nchini Uganda na Tanzania. Mkurugenzi wa Mipango na Uwekezaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Derick Moshi, aliyemwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa TPDC, amesema kukamilika kwa asilimia 88 ya ujenzi wa PS3 ni hatua kubwa katika utekelezaji wa mradi huo. Moshi amesema ziara ya wabia na wadau wa mradi huo katika kituo hicho imelenga kujionea maendeleo ya ujenzi na hatua zilizofikiwa pia kuweka msisitizo wa kuhakikisha vituo vyote vya kusukuma mafuta vya mradi huo vikikamilika ifikapo Desemba mwaka hatua itakayosaidia katika kukamilisha maandalizi ya uendeshaj...
Marato tv - Sauti ya Jamii