Skip to main content

Posts

Showing posts from July 10, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

HISTORIA MPYA MAFINGA: SHULE YA SEKONDARI NDOLEZI YAANZA KUPOKEA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO

  Na Mwandishi Wetu, Mafinga SHULE ya Sekondari Ndolezi iliyopo Halmashauri ya Mji Mafinga, Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, imeandika historia mpya baada ya kuanza rasmi kupokea wanafunzi wa Kidato cha Tano kwa mara ya kwanza. Hatua hii inatajwa kuwa ukombozi mkubwa utakaopanua fursa za elimu ya sekondari ya juu (A-Level) katika eneo hilo. Akizungumza na wanafunzi wa kwanza waliowasili shuleni hapo, Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Mji Mafinga, Mwalimu Stephen Shemdoe, amesema lengo kuu la Halmashauri ni kuhakikisha wanafunzi kutoka maeneo mbalimbali nchini wanapata elimu bora itakayowezesha kupata matokeo mazuri na kuchangia maendeleo ya Taifa. Mwalimu Shemdoe amebainisha kuwa Serikali imefanya uwekezaji mkubwa katika ujenzi wa miundombinu na kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia. Kutokana na uwekezaji huo, amewataka wanafunzi kutumia fursa hiyo adhimu kusoma kwa bidii, kutunza mali za shule, na kuzingatia nidhamu ya hali ya juu. "Matamanio ya Serikali ni kuona...

JAKAYA KIKWETE,BAN KI-MOIN WAIBUA DIRA MPYA YA KUINUA ELIMU DUNIANI

 Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, amefanya mazungumzo ya ngazi ya juu na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Ban Ki-moon, yaliyolenga kuimarisha ushirikiano wa kimataifa katika kuboresha elimu ya awali na msingi kwa mamilioni ya watoto duniani. Mazungumzo hayo yamefanyika jijini Seoul, Korea Kusini, ambapo Dkt. Kikwete yupo katika ziara ya kikazi kama Mwenyekiti wa Bodi ya Global Partnership for Education (GPE), taasisi ya kimataifa inayoratibu juhudi za kuongeza fursa za elimu katika zaidi ya nchi 90 duniani. Katika mkutano huo, Dkt. Kikwete alimpongeza Ban Ki-moon kwa kuendelea kuwa kinara wa kuhamasisha utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs), hususan kuhakikisha kila mtoto anapata elimu bora bila kujali mazingira anayokulia. Aidha, alimshukuru kwa mchango wake katika kuimarisha ushirikiano kati ya GPE na Serikali ya Korea Kusini, ambayo imeendelea kuwa miongoni mwa wadau muhimu wanaofadhili miradi ya elimu duniani. Ak...

WAKULIMA WA MARA WAHIMIZWA KUFUATA KALENDA ZA MAZAO YA BIASHARA KUONGEZA TIJA

 Adeladius Makwega – Serengeti, Mara, Tanzania Wakulima wa Mkoa wa Mara wametakiwa kuzingatia kalenda za mazao ya biashara, hususan zao la tumbaku, ili kuongeza tija, kuboresha kipato chao na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa. Wito huo umetolewa Julai 10, 2026, wilayani Serengeti na Mkuu wa Wilaya ya Rorya, Mheshimiwa Alfa Haule, alipokuwa akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kanali Evans Alfred Mtambi, katika mkutano wa WAMACU unaowakutanisha wadau wa zao la tumbaku mkoani hapa. Akizungumza katika mkutano huo, mheshimiwa Haule alisisitiza kuwa sekta ya kilimo ni mhimili muhimu wa uchumi, unaogusa moja kwa moja maisha ya wananchi kuanzia ngazi ya mtu mmoja mmoja hadi taifa. “Sekta ya kilimo ni chanzo kikubwa cha mapato. Ina uwezo wa kuinua kipato cha mtu mmoja mmoja, kaya, kijiji, kata, tarafa, wilaya, mkoa na taifa kwa ujumla. Ni wajibu wa wananchi kuongeza juhudi katika sekta hii huku serikali ikiendelea kuwapa ushirikiano,” alisema Haule. Aidha, aliwataka wakulima kuzingatia mi...

KITABU CHA FALSAFA YA SHERIA YA MAMA SAMIA KUBORESHA MAGEUZI YA KIUCHUMI NA KIJAMII

 SERIKALI imesema, Sheria zinapaswa kutumika kama nyenzo ya maendeleo ya taifa kwakuwa ubora wa Sheria hupimwa kwa matokeo yake katika kuboresha maisha ya wananchi, kuvutia uwekezaji, kuimarisha utawala bora na kuchochea ukuaji wa uchumi. Hayo yamesemwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe.Hemed Suleiman Abdullah alipomuwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, katika Uzinduzi wa Kitabu cha Falsafa ya Sheria ya Mama Samia uliofanyika katika Ukumbi wa Maktaba mpya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), tarehe 10 Julai, 2026.  Aidha, Mhe. Abdulla,amempongeza Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza S. Johari kwa kutoa wazo la kuandikwa kwa Kitabu cha Falsafa ya Sheria ya Mama Samia (Mama Samia Doctrine of Law): Utekelezaji Wake katika Mageuzi ya Kiuchumi na Kijamii.  “Nitoe pongezi za dhati kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza Said Johari, kwa kuja na wazo hili muhimu la kuandaa Kitabu hiki...

APANDISHWA KIZIMBANI AKIDAIWA KUMUUA MAMA YAKE MZAZI

 Na: Dawati la Habari Polisi Geita Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita limemfikisha mahakamani Lufuta Magoma (40) Mganga wa Kienyeji na mkazi wa kijiji cha Rutunguru akituhumiwa kwa mauaji ya Dotto Magoma Nyara (70) ambaye ni mama yake mzazi. Mshtakiwa huyo amepandishwa kizimbani leo Ijumaa Julai 10, 2026, katika Mahakama ya Wilaya ya Chato na kusomewa shtaka la Mauaji. ​Akisoma shauri hilo la jinai namba 15471 la mwaka 2026 mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Chato, Mhe. Erick Kagimbo, Wakili wa Serikali Mashaka Said, aliieleza mahakama kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo mnamo tarehe 04.06.2026 katika Kijiji cha Rutunguru, wilaya ya Geita. ​Mshtakiwa akiwa katika eneo la Rutunguru anadaiwa kumshambulia na kumuua Mama yake mzazi kinyume na kifungu cha 196 na 197 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, Sura ya 16 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2023. ​Hata hivyo, mshtakiwa huyo hakutakiwa kujibu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kisheria ya kusikiliza mashauri y...

SMAUJATA KUFANYA ZIARA YA KUPINGA UKATILI MKOANI MARA

 Leo Julai 10,2029, Viongozi pamoja na watendaji wa Taasisi isiyo ya kiserikali SMAUJATA ( Shujaa wa maendeleo na ustawi wa jamii Tanzania) Wamefika katika ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Evans Mtambi kwaajili yakumsalimia pamoja na kumueleza kuhusu ziara yao mkoa wa Mara yenye lengo kutoa elimu ya kupinga ukatili kwa watoto, wanawake na wababa mkoani hapo yenye kauli mbiu isemayo " Kataa ukatili, wewe ni shujaa", wakiwa wameambatana na wawakilishi vya mikoa mingine iliyopo kanda ya Ziwa.

SOYA ONE, ELIAKIMU MASWI WAPONGEZWA KWA KUUNGA MKONO JUHUDI ZA RAIS SAMIA KUBORESHA ELIMU TARIME

 Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Meja Edward Gowele, ameipongeza Kampuni ya Soya One Limited pamoja na Eliakim Maswi kwa kujitolea kutoa vifaa vya TEHAMA kwa shule za sekondari wilayani humo, akisema mchango huo ni kielelezo cha uzalendo na unaunga mkono juhudi za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuboresha sekta ya elimu nchini. Akizungumza katika hafla ya kukabidhi vifaa hivyo, Meja Gowele amesema Serikali ya Wilaya inaamini maendeleo ya elimu hayawezi kuachwa mikononi mwa Serikali pekee, bali yanahitaji ushirikiano wa wadau wote wakiwemo wawekezaji, wafanyabiashara, viongozi wa kisiasa na wananchi. Amesema kila mwenye uwezo anapaswa kuchangia maendeleo ya elimu kwa kiwango anachoweza, akisisitiza kuwa hakuna mchango mdogo unapolenga kuboresha maisha ya watoto na mustakabali wa Taifa. "Sio lazima uwe na uwezo mkubwa ndiyo uchangie elimu. Hata mchango mdogo unaweza kuleta mabadiliko makubwa. Tunawapongeza Soya One Limited na Eliakim Maswi kwa moyo wao wa kujitolea. Huu ni mfano mzuri u...

BMH YAREJESHA TABASAMU KWA WATOTO WA BURUNDI BAADA YA UPASUAJI WA MOY

 Watoto watatu kati ya sita kutoka nchini Burundi wenye matatizo ya matundu ya moyo wamefanyiwa upasuaji wa kuziba matundu hayo kwa mafanikio katika Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH), hatua inayodhihirisha uwezo wa Tanzania katika huduma za kibingwa na kuimarisha ushirikiano wa afya katika ukanda wa Afrika Mashariki. Huduma hiyo imetolewa kupitia ushirikiano kati ya Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH), Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) na wataalamu wa afya kutoka Burundi, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kukuza tiba utalii na kubadilishana utaalamu wa kitabibu. Akizungumza na waandishi wa habari Julai 9, 2026 jijini Dodoma, Mkurugenzi Mtendaji wa BMH, Prof. Abel Makubi, alisema watoto wote waliopatiwa matibabu wanaendelea vizuri na wameonyesha maendeleo ya kuridhisha baada ya kufanyiwa upasuaji huo. “Mafanikio haya yanaonyesha uwezo wa taasisi zetu za afya kushirikiana kutoa huduma za kibingwa zinazokidhi viwango vya kimataifa. Ushirikiano huu pia umefungua fursa ya kubadilishana ...