Na MASHAKA MHANDO, Tanga VYAMA vya siasa mkoani Tanga, vimetakiwa kufuata kanunu, taratibu na Sheria ya uchaguzi kuchagua wanaendesha kampeni zenye na upendo ili uchaguzi wa Oktoba 29 mwaka huu ufanyike kwa amani. Akizungumza katika semina ya siku moja iliyofanyika katika ukumbi wa Jiji la Tanga Leo Septemba 11, Ofisa Mwandamizi wa ofisi ya Msajili wa vyama vya Siasa nchini, Edna Assey alisema vyama vinapaswa kufuata Sheria na waepuke kampeni zenye viashiria vya uvunjigu wa amani nchini. Alisema kuwa wajibu wa vyama vya siasa ni uchaguzi na kushinda baada ya wananchi kuridhika na sera za vyama vyao wanazofanya mikutano ya kampeni. Ofisa huyo alisema viongozi hao wafuate taratibu za uchaguzi ambazo ni mbili za Vyama vya siasa Sheria namba 257 na Sheria namba 278 za gharama za uchaguzi. "Najua viongozi mnajua Sheria hizi, mtazifuata lakini mtafanya kampeni za kistaarabu ambazo zitasababisha uchaguzi wetu unafanyika kwa Amani na haki," alisema. Pia aliwataka kuhakikisha kuwa end...
Marato tv - Sauti ya Jamii