Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa, Ndugu Stephen Wasira, amewasili leo mkoani Kilimanjaro kwa ziara rasmi ya kikazi ya siku 5 Mkoani humo. Ndg Wasira amepokelewa na viongozi mbalimbali wa chama wakiongozwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro, Ndugu Patrick Boisafi, alipowasili Katika Ofisi za CCM Mkoani hapo Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa, Ndugu Wasira anatarajiwa kukutana na kuzungumza na viongozi na wanachama wa CCM ngazi zote ndani ya mkoa huo. Lengo ni kuimarisha mshikamano na kupata uelewa wa changamoto zinazowakabili. Kilele cha ziara hiyo kitakuwa tarehe 8 Juni, 2026 ambapo anatarajiwa kuongoza mkutano wa hadhara na wananchi wa Wilaya ya Same.
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa washiriki wa kozi kutoka Chuo cha Ulinzi cha Taifa cha India walipotembelea Ofisi za iliyokuwa Makao Makuu ya Jeshi Upanga Jijini Dar es Salaam leo tarehe 05 Juni 26. Akizungumza na washiriki wa kozi hiyo, Jenerali Mkunda amesisitiza kuendelea kwa ushirikiano wa kimafunzo kati ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania na Jeshi la India ili kuwajengea uwezo kijeshi wanajeshi wa nchi mbili hizi. "Tunashuru kwa kuja kuitembelea Tanzania kwa ziara ya kimafunzo, hii inaonesha jinsi diplomasia ya kijeshi inavyochangia kuongeza weledi na ujuzi kijeshi. Naye, Mkuu wa msafara wa washiriki wa kozi hiyo Rear Admiral…amesema kuwa, kundi la washiriki wa kozi ya NDC India wamejionea jinsi JWTZ linavyoboresha mafunzo yake, na kupongeza maendeleo ya kimafunzo kwa Chuo cha Ukamanda na Unadhimu (Command and Staff Collage) kilichopo Duluti Jijini Arusha. Aidha, Rear Admiral…alipongeza juhudi za Serik...