Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

#top_stories

MARA YAJIPANGA KUNUFAIKA NA FURSA ZA KONGAMANO LA TAIFA LA KILIMO MISITU

Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mheshimiwa Kanali Evans Alfred Mtambi, leo tarehe 21 Agosti 2026, amewapokea na kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka Vi Agroforestry kuhusu maandalizi ya Kongamano la 11 la Taifa la Kilimo Misitu, litakalofanyika kuanzia tarehe 19 hadi 21 Oktoba 2026 katika Kituo cha Mafunzo cha Agroforestry (ATC), Bweri, Manispaa ya Musoma. Mazungumzo hayo yalijikita katika maandalizi ya kongamano hilo, ambalo linalenga kuhamasisha kilimo misitu kama nyenzo ya kuongeza uzalishaji, kuhifadhi mazingira, kuimarisha usalama wa chakula na kuinua uchumi wa wananchi. Akizungumza katika kikao hicho, Mheshimiwa Kanali Mtambi amewashukuru Vi Agroforestry kwa juhudi wanazozifanya kila msimu katika kuhakikisha vijana na Watanzania kwa ujumla wanaelewa fursa zilizopo katika sekta ya kilimo.  Aidha, ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Mara, hususan vijana, kujitokeza kwa wingi kushiriki katika kongamano hilo ili kujifunza, kubadilishana uzoefu na kuibua wigo mpya wa fursa za maendeleo ya k...
Recent posts

MASWI, DKT. KIDA WAJADILI UFUNGAMANISHAJI JAMII AJENDA NA DIRA 2050

 Katibu Mkuu @maendeleoyajamii, Eliakimu Maswi na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Tausi M. Kida, leo Agosti 20, 2026 wamejadiliana kuhusu ufungamanishaji wa Ajenda ya Kitaifa ya Mageuzi ya Kijamii na Maendeleo ya Mtaji Watu katika Kufikia Malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na Dira 2050. Majadiliano yao yamejikita katika umuhimu wa kuhakikisha mipango na mikakati ya kisekta hususani sekta ya maendeleo ya Jamii, inaendana na vipaumbele vya Taifa vilivyowekwa katika Dira 2050 na mipango ya maendeleo ya muda mrefu na muda wa kati, ili iweze kutoa mchango unaopimika katika kufikia malengo ya Taifa. Dkt. Kida amesema baada ya Dira 2050 kuzinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Julai 17, 2025, na kuzinduliwa kwa nyenzo za utekelezaji wake Agosti 3, 2026, ni muhimu kila taasisi na mdau kuhakikisha mikakati na programu zake zinafungamana na malengo ya Dira hiyo. “Nikupongeze Katibu Mkuu Maswi kwa kuchukua hatua ya kuoanisha m...

WAZIRI OMAR ASHUKURU IMF KWA USHIRIKIANO WA MUDA MREFU NA TANZANIA

 Na. Benny Mwaipaja, Dar es Salaam Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, amelishukuru Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kwa mchango wake kwa Tanzania tangu kuanza kwa ushirikiano kati yake na Shirika hilo, akieleza kuwa ushirikiano huo umeendelea kuwa muhimu katika kuimarisha uchumi na utekelezaji wa ajenda za maendeleo nchini. Ametoa Shukran hizo wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Mwakilishi mpya wa IMF nchini Tanzania, Bi. Jana Bricco, ambaye ameanza rasmi majukumu yake nchini, ambapo walijadili masuala mbalimbali yanayohusu ushirikiano kati ya Tanzania na IMF, ambao umedumu kwa zaidi ya miongo sita tangu uanzishwe miaka ya 1960. Mhe. Balozi Omar amesema Serikali itaendelea kuimarisha ushirikiano na IMF katika kufanikisha ajenda ya maendeleo ya Tanzania, ikiwemo utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 pamoja na mwelekeo wa kimkakati wa Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano unaofuata ambayo ni maeneo yenye manufaa kwa pande zote na yanayochangia utekeleza...

RAIS SAMIA KUWAREJESHA NYUMBANI WATANZANIA 669 KUTOKA AFRIKA KUSINI

 WATANZANIA 669 waliopo Afrika Kusini wanatarajiwa kurejea nchini kwa hiari yao kwa msaada wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kufuatia maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwawezesha kurejea nyumbani na kuungana na familia zao. Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, James Bwana, ameyasema hayo leo kuwa utekelezaji wa mpango huo utaanza na kundi la kwanza la Watanzania 241 kutoka Durban, Jimbo la KwaZulu-Natal, watakaorejea nchini Agosti 26, 2026 kwa ndege ya Air Tanzania. Kwa mujibu wa Balozi Bwana, Watanzania hao watafanyiwa uhakiki Agosti 25 na 26 kwa kushirikisha Ubalozi wa Tanzania na mamlaka za Afrika Kusini, kabla ya kuanza safari ya kurejea nchini. Amesema mpango huo umeanza baada ya Watanzania hao kuomba kwa hiari yao msaada wa Serikali ili waweze kurejea Tanzania, baada ya kuishi Afrika Kusini kwa muda mrefu. “Mheshimiwa Rais amewakaribisha tena nyumbani na amenielekeza kama Balozi wake hapa Afrika Kusini kuhakikisha Watanzania walio tayari kurejea...

DKT. MWIGULU ATOA MAELEKEZO VIWANJA VYA AFCON

▪︎ Ataka kazi ifanyike usiku na mchana inapowezekana ▪︎ Asisitiza mashindano hayo ni fursa kubwa ya kiuchumi kwa Tanzania WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba ameagiza kuongezwa kasi ya ujenzi wa viwanja vya mazoezi vitakavyotumika katika mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027, ili vikamilike kwa wakati na kukidhi viwango vinavyotakiwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF). Amesema kazi hiyo inapaswa kufanyika kwa kasi, ikiwemo kuongeza muda wa kufanya kazi pale inapobidi, ili viwanja vikamilike kwa wakati na Tanzania iwe tayari kabla ya ukaguzi wa maandalizi unaotarajiwa kufanywa na CAF. Waziri Mkuu ametoa maelekezo hayo leo (Ijumaa, Agosti 21, 2026) baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa viwanja vya mazoezi vya Farasi na Leaders Club jijini Dar es Salaam, ambavyo ni miongoni mwa viwanja vitakavyotumika katika maandalizi ya mashindano ya AFCON 2027 yatakayofanyika kwa ushirikiano wa Tanzania, Kenya na Uganda. Amesema Tanzania haipaswi kusubiri hadi dakika za mwisho...

DC CHIKOKA AWAKUMBUSHA WAJUMBE WA KAMATI YA AFYA MSINGI (PHC)KUFANYA KAZI KWA UFANISI KUELEKEA ZOEZI LA UTOAJI CHANJO YA POLIO

 Na Mwandishi wetu Jovina Massano MKUU wa Wilaya ya Musoma mkoani Mara Juma Chikoka awakumbusha wajumbe wa kamati ya Afya ya msingi(PHC) Kufanya kazi kwa ufanisi kuelekea zoezi la chanjo ya Polio ya matone(nOPV2) linalitarajia kufanyika Agosti 27-30. Ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa wajumbe hao katika ukumbi wa Manispaa ya Musoma ikiwahusisha washiriki kutoka halmashauri ya Musoma vijijini na halmashauri Manispaa ya Musoma. Chikoka amesema kuwa katika halmashauri ya Musoma vijijini wanatarajia kuwafikia watoto walio chini ya miaka 10 wapatao 118,936 huku halmashauri ya Manispaa ya Musoma inatarajia kuwafikia watoto wapatao 66,176. Amesema atahakikisha hamasa na elimu ya kutosha itatolewa kwa jamii ili kuwajengea uelewa wa kutosha kuhusu chanjo hii ambayo inakwenda kuondoa changamoto ya ulemavu kwa watoto. "Tutaendelea kufanya ushirikishwaji na kushirikiana ili kuleta mapokeo na matokeo makubwa na kila mmoja atimize wajibu wake,"amesema Chikoka. Ili kufikia ma...