Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mheshimiwa Kanali Evans Alfred Mtambi, leo tarehe 21 Agosti 2026, amewapokea na kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka Vi Agroforestry kuhusu maandalizi ya Kongamano la 11 la Taifa la Kilimo Misitu, litakalofanyika kuanzia tarehe 19 hadi 21 Oktoba 2026 katika Kituo cha Mafunzo cha Agroforestry (ATC), Bweri, Manispaa ya Musoma. Mazungumzo hayo yalijikita katika maandalizi ya kongamano hilo, ambalo linalenga kuhamasisha kilimo misitu kama nyenzo ya kuongeza uzalishaji, kuhifadhi mazingira, kuimarisha usalama wa chakula na kuinua uchumi wa wananchi. Akizungumza katika kikao hicho, Mheshimiwa Kanali Mtambi amewashukuru Vi Agroforestry kwa juhudi wanazozifanya kila msimu katika kuhakikisha vijana na Watanzania kwa ujumla wanaelewa fursa zilizopo katika sekta ya kilimo. Aidha, ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Mara, hususan vijana, kujitokeza kwa wingi kushiriki katika kongamano hilo ili kujifunza, kubadilishana uzoefu na kuibua wigo mpya wa fursa za maendeleo ya k...
Katibu Mkuu @maendeleoyajamii, Eliakimu Maswi na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Tausi M. Kida, leo Agosti 20, 2026 wamejadiliana kuhusu ufungamanishaji wa Ajenda ya Kitaifa ya Mageuzi ya Kijamii na Maendeleo ya Mtaji Watu katika Kufikia Malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na Dira 2050. Majadiliano yao yamejikita katika umuhimu wa kuhakikisha mipango na mikakati ya kisekta hususani sekta ya maendeleo ya Jamii, inaendana na vipaumbele vya Taifa vilivyowekwa katika Dira 2050 na mipango ya maendeleo ya muda mrefu na muda wa kati, ili iweze kutoa mchango unaopimika katika kufikia malengo ya Taifa. Dkt. Kida amesema baada ya Dira 2050 kuzinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Julai 17, 2025, na kuzinduliwa kwa nyenzo za utekelezaji wake Agosti 3, 2026, ni muhimu kila taasisi na mdau kuhakikisha mikakati na programu zake zinafungamana na malengo ya Dira hiyo. “Nikupongeze Katibu Mkuu Maswi kwa kuchukua hatua ya kuoanisha m...