Skip to main content

Posts

Showing posts from July 9, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

CHATANDA: MARIDHIANO CCM NA ACT-WAZALENDO YAMEZINGATIA MASLAHI YA ZANZIBAR

 NA: MWANDISHI WETU, DODOMA Maridhiano baina ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Alliance For Change and Transparency (ACT-Wazalendo) kuelekea uundwaji wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK) Zanzibar, umepongezwa kwani umezingatia maslahi ya nchi ambayo ni muhimu kuliko maslahi binafsi ya wanasiasa. Hayo yameelezwa na Mbunge wa Viti Maalum CCM na Mwenyekiti Taifa wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Mary Chatanda, Julai 9, 2026, Jijini Dodoma. Akitoa maoni yake baada ya kumalizika hafla hiyo ya Tamko la Pamoja la Maridhiano ya Kisiasa baina ya vyama hivyo, Chatanda amesema, Wazanzibar wameshasahau siasa za chuki, kipaumbele chao sasa ni umoja, mshikamano na maendeleo. "Wazanzibar ni watu rahimu sana, wao wanataka amani, mshikamano na maendeleo na kitendo cha vyama hivi viwili kufikia muafaka, ni ishara ya ukomavu wa kisiasa na kuzingatia maslahi ya nchi," amesema Chatanda. Aidha, amesema maridhiano hayo yana maana kubwa katika kuhakikisha SUK inaundwa kwa ukamilifu wake kwani SUK ...

PENYE SIASA ZA CHUKI NA MIVUTANO, BARAKA ZA MAENDELEO HUPOTEA," RAIS SAMIA ATOA ONYO KWA WANAOCHOCHEA VITENDO VYA UGAIDI

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali haitasita kuchukua hatua dhidi ya vitendo vya uvunjifu wa amani, uharibifu wa mali, miundombinu na mienendo yoyote inayolenga kuyumbisha amani na usalama wa nchi pamoja na wananchi. Amesema maslahi ya kisiasa, kiitikadi au kidini, havipaswi kutumiwa kama mwavuli wa vitendo vya kigaidi vyenye lengo la kutishia raia, kuharibu mali au kudhoofisha heshima ya nchi, akisisitiza kuwa maslahi ya watu wachache hayawezi kuwekwa juu ya usalama wa Watanzania. Rais Dkt. Samia ameyasema hayo leo wakati akishuhudia utiaji saini wa Tamko la Pamoja la Maridhiano ya Kisiasa Zanzibar, kati ya Chama cha Mapinduzi na Chama cha ACT Wazalendo, akisema hatua hiyo ni alama muhimu ya kuimarisha amani, umoja na utulivu wa Zanzibar na Taifa kwa ujumla. Amempongeza Rais wa Zanzibar na Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, na Mwenyekiti wa ACT Wazalendo kwa kutanguliza maslahi ya nchi katika kutafuta muafaka wa pamoja k...

CCT YAWEKEZA BILLIONI 3.8 DODOMA

 Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule, amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeendelea kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji na kukuza sekta binafsi, ikiwemo uwekezaji unaofanywa na Taasisi za Dini kutokana na mchango wake mkubwa katika kukuza uchumi wa Nchi. Mhe. Senyamule ameyasema hayo leo Julai 09, 2026, wakati wa hafla ya uzinduzi wa jengo la kitega uchumi la Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT Complex), hafla iliyoambatana na Mkutano wa 60 wa Halmashauri Kuu ya Jumuiya hiyo, uliofanyika katika ukumbi uliopo ndani ya jengo hilo. "Serikali imeendelea kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji na kukuza sekta binafsi, ikiwemo Taasisi za Dini. Tunatambua mchango mkubwa wa taasisi hizi katika utoaji wa elimu, huduma za afya, kujenga maadili ya jamii na kuchochea maendeleo ya kiuchumi," amesema Mhe. Senyamule. Ameongeza kuwa miradi ya uwekezaji kama huo ni mfano mzuri wa namna Taasisi z...

KAMISHNA WA UHIFADHI TANAPA AANZA KAZI KWA MAAGIZO SITA YA WAZIRI KIJAJI

 Na. Calvin Katera - Arusha. Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) ametoa maagizo sita kwa Kamishna wa Uhifadhi TANAPA Massana Mwishawa leo Julai 09, 2026, jijini Arusha alipokuwa akiongoza zoezi la uapisho kwa aliyekuwa Naibu Kamishna wa Uhifadhi baada ya kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan Julai 02, 2026 kuchukua nafasi ya Kamishna wa Uhifadhi (Mstaafu) CPA Musa Nassoro Kuji aliyemaliza muda wake. Akizungumza katika hafla ya uapisho huo Waziri Kijaji amemwelekeza Kamishna Mwishawa kusimamia miundombinu ya hifadhi, kuvutia wawekezaji, kubuni bidhaa mpya za utalii, kusimamia mapato, kuimarisha uhusiano na jamii zinazozunguka maeneo ya hifadhi bila kusahau nidhamu, uadilifu, weledi, ustawi wa watumishi na kusimamia maslahi yao kwa wakati. Naye, Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini TANAPA, Mkuu wa Majeshi (Mst.) Jenerali George Waitara alieleza kuwa Bodi itaendelea kutoa ushirikiano wa dhati na ushauri wakati wote ili kufanik...

CP KAVIRONDO ASISITIZA UBUNIFU NA UBORA KATIKA MIRADI YA UJENZI YA JESHI LA MAGEREZA

 Na. Ssgt Mawazo Mtondo - DODOMA. Kamishna wa Huduma za Urekebu Jeshi la Magereza, CP Amina Kavirondo, Julai 8, 2026, alifanya ziara ya kukagua maendeleo ya miradi mbalimbali ya ujenzi inayotekelezwa na Jeshi la Magereza Jiji la Dodoma. Katika ziara hiyo, CP Kavirondo alikagua eneo linalotarajiwa kujengwa Ofisi za Makao Makuu ya Jeshi la Magereza lililopo NCC Ntyuka lenye ukubwa wa hekari 7.3, eneo la ujenzi wa nyumba ya Mkuu wa Jeshi la Magereza lililopo Itega lenye ukubwa wa hekari 4 na eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za Makamishna lililopo Msalato.  Aidha, alikagua mradi wa ukarabati wa Gereza Maalum lililopo eneo la Isanga, mradi wa ujenzi wa Gereza Jipya linaloendelea kujengwa katika eneo la Msalato, ujenzi wa jukwaa la uwanja wa gwaride pamoja na jengo la kubadilishia nguo katika viwanja vya michezo vilivyopo eneo la Makao Makuu ya Jeshi la Magereza Msalato Jijini Dodoma. Akiwa katika ukaguzi wa ujenzi wa Gereza Jipya la Msalato, CP Kavirondo alisisitiza...