*Na: Dawati la Habari Polisi Mwanza* -Wananchi Misungwi wadai mitandao ya kijamii inadhoofisha maadili ya vijana, Polisi waahidi kuwachukulia hatua wahalifu wa mtandaoni Baadhi ya wananchi mkoani Mwanza wameiomba Serikali kuimarisha udhibiti wa matumizi ya mitandao ya kijamii kwa kuweka mikakati madhubuti ya kisheria, wakieleza kuwa baadhi ya matumizi yake yameanza kuhatarisha maadili ya vijana na kuchochea taharuki katika jamii. Ombi hilo limetolewa na Katibu wa Maafisa Usafirishaji wa Kata ya Usagara, Wilaya ya Misungwi, Thomas Michael, wakati wa mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza kwa lengo la kusikiliza na kutatua changamoto za kiusalama katika eneo hilo. Katika mkutano huo uliowahusisha wananchi pamoja na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Wilbrod Mutafungwa, Michael alisema licha ya manufaa ya mitandao ya kijamii, baadhi ya watumiaji wamekuwa wakiitumia vibaya kwa kusambaza taarifa zisizo sahihi na maudhui yanayodh...
Marato tv - Sauti ya Jamii