📌 Asema suala la Tanzania kuwa na nishati ya uhakika si la kusubiri 📌 Taasisi ya Kimataifa ya Umeme Jua (ISA) yaonesha nia ya kuwekeza 📌 Kituo cha umahiri wa umeme jua kuzinduliwa Arusha Juni mwaka huu Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Kimataifa ya Kuendeleza Nishati ya Jua (ISA), Dkt. Ajay Mathur yenye Makao Makuu yake nchini India ambaye ameeleza nia ya ISA kuwekeza katika miradi ya umeme jua nchini. Mazungumzo kati ya Dkt. Biteko na Dkt. Mathur yamefanyika jijini New Delhi nchini India ambapo Dkt. Biteko alishiriki Wiki ya Nishati India ambayo ilienda sambamba na mikutano mbalimbali kuhusu nishati. “ Tunawaalika mje kuwekeza Tanzania kwani tunahitaji kuwa na miradi mingi ya umeme kutoka vyanzo tofauti ili kuweza kutosheleza mahitaji ya watu wetu na kinachotupa msukumo zaidi kwa sasa ni mpango mahsusi wa misheni 300 tuliousaini mwezi Januari 2025 ambapo Tanzania tunapaswa kup...
Marato tv - Sauti ya Jamii