Skip to main content

Posts

Showing posts from June 3, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

MWIGULU:USHIRIKIANO WA WANANCHI NI MUHIMU KUDHIBITI EBOLA NCHINI

 Waziri Mkuu wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema Serikali imeendelea kuimarisha tahadhari na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu ugonjwa wa Ebola ili kuzuia hatari ya ugonjwa huo kuingia na kusambaa nchini. Akijibu maswali ya Papo kwa Papo Bungeni jijini Dodoma leo Juni 4, 2026, Dkt. Mwigulu alisema Tanzania inaendelea kuwa na mahusiano ya karibu na mataifa jirani kupitia shughuli za kijamii, kiuchumi na kiutamaduni, hali inayochochea mwingiliano wa watu kuvuka mipaka na hivyo kuhitaji umakini mkubwa katika kudhibiti magonjwa ya mlipuko. Amesema Serikali imechukua hatua mbalimbali za kinga ikiwemo kuendelea kutoa elimu kwa umma kupitia majukwaa tofauti, kuhamasisha wananchi kuzingatia tahadhari za kiafya na kuimarisha ufuatiliaji katika maeneo ya mipakani na sehemu nyingine muhimu. “Tanzania si kisiwa. Kila mwananchi ana wajibu wa kushiriki katika mapambano dhidi ya Ebola kwa kuzingatia tahadhari na kutoa taarifa mapema pale anapoona dalili zinazoweza kuashiria ugonjwa huo,” ame...

TANZANIA NA URUSI ZIPO KATIKA HATUA ZA MWISHO MAKUBALIANO KUHUSU MATUMIZI YA FEDHA

 Na Beda Msimbe TBN Moscow.      Tanzania na Urusi zipo katika hatua za mwisho za majadiliano za matumizi ya fedha za malipo kwa lengo la kuimarisha biashara baina yao.         Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais -Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo kwenye mahojiano na waandishi wa habari waliopo katika msafara wa ziara ya kitaifa ya Rais Samia Suluhu Hassan nchini Urusi.        Alisema mataifa hayo mawili yatasaini hati za makubaliano kabla kumalizika kwa ziara.                                 Alisema kuna urari wa biashara wa Dola za Marekani milioni 200 hivyo hatua hiyo ya kufikia makubaliano itafungua njia ya ushirikiano kwenye ufanisi katika masuala ya uwekezaji na biashara.                              Alifafanua kuwa makuba...

TIMU KUTOKA OFISI YA WAZIRI MKUU YAFANYA MAZUNGUMZO NA KATIBU TAWALA MWANZA KUHUSU MASUALA YA USIMAMIZI WA MAAFA

 Na, mwandishi wetu - Mwanza Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa Mwanza Bw. Henry Mwaijega amekutana na kufanya mazungumzo timu ya Idara ya Usimamizi wa Maafa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu walipomtembelea ofisini kwake leo 04 Juni, 2026 Jijini Mwanza. Timu hiyo ipo mkoani Mwanza kwa lengo la kuongoza mafunzo ya usimamizi wa maafa kwa Kamati za Usimamizi wa Maafa mkoa pamoja na wadau mbalimbali, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha utayari, uratibu na uwezo wa kukabiliana na majanga katika ngazi ya mkoa. Pamoja na mafunzo hayo, wanatarajia kuzindua Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura cha mkoa wa mwanza tarehe 05 juni, 2026.

WABUNGE WALIOKWENDA MOROCCO BILA KIBALI KUJIELEZA

 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mussa Hazan Zungu, ameeleza kusikitishwa na kuongezeka kwa utoro wa baadhi ya wabunge na viongozi wa Serikali ndani ya Bunge, akisema hali hiyo inashusha hadhi ya Bunge na kudhoofisha uwajibikaji kwa wananchi waliowachagua. Akizungumza Bungeni Jijini Dodoma leo Juni 4, 2026, Spika Zungu amesema baadhi ya wabunge wamekuwa wakikosa vikao bila sababu za msingi au kusafiri nje ya maeneo yao ya kazi bila kufuata taratibu na kupata vibali vinavyotakiwa kutoka Ofisi ya Spika. Kutokana na hali hiyo, Spika Zungu amemuagiza Katibu wa Bunge kufanya uchambuzi wa kina wa mahudhurio ya wabunge na kuwasilisha taarifa rasmi itakayobainisha wabunge wote wenye utoro wa mara kwa mara ili hatua stahiki zichukuliwe kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za Bunge. Aidha, amemtaka Katibu wa Bunge kutumia mifumo ya kisasa ya ufuatiliaji na mawasiliano iliyopo kubaini mahali walipo wabunge wanaokosa vikao bila taarifa rasmi, akisisitiza kuwa teknolojia ...

DKT. MAHERA; BUTIAMA KUNUFAIKA NA MIRADI YA AFYA

 Mbunge wa Jimbo la Butiama, Dkt. Charles Mahera , amesema Bajeti ya Wizara ya Afya kwa mwaka wa Fedha 2026/27 pamoja na fedha zinazotolewa kupitia Ofisi ya Rais TAMISEMI zimeendelea kuonesha mwelekeo chanya wa Serikali katika kuimarisha huduma za afya ngazi ya msingi, huku Wilaya ya Butiama ikitarajiwa kunufaika na miradi mikubwa ya miundombinu ya afya. Akizungumza leo Jun 3,2026 Katika Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma, Dkt. Mahera amesema uwekezaji huo utaongeza upatikanaji wa huduma bora, karibu na wananchi, na kupunguza changamoto ya umbali wa kufuata huduma za afya. Amesema katika mgawanyo wa fedha hizo, Hospitali ya Wilaya ya Butiama imepangiwa Shilingi milioni 500 kutoka Serikali Kuu kwa ajili ya ujenzi na upanuzi wa majengo, hatua inayolenga kuongeza uwezo wa hospitali hiyo kuhudumia wagonjwa wengi zaidi na kuboresha utoaji wa huduma za kitaalamu. Aidha, Serikali imetenga Shilingi milioni 300 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa vituo viwili vya afya, ambapo Kituo cha Afya But...

MAHERA: UWEKEZAJI WA RAIS SAMIA ELIMU NA AFYA WALETA MAGEUZI MAKUBWA BUTIAMA

  Mbunge wa Jimbo la Butiama, Dkt. Charles Mahera, amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuleta mapinduzi makubwa katika sekta za elimu na afya kupitia uwekezaji wa mabilioni ya shilingi unaolenga kuboresha huduma za kijamii na kuinua maisha ya wananchi. Akizungumza leo Jun 3,2026 katika Viwanja Jijini Dodoma,Dkt. Mahera amesema katika sekta ya elimu, Serikali imeendelea kuimarisha miundombinu ya vyuo vya VETA nchini kwa kujenga na kuendeleza vyuo katika maeneo ambayo bado hayajafikiwa na huduma hiyo, sambamba na kusambaza vifaa vya kisasa vya kufundishia na kujifunzia ili kuongeza ufanisi wa mafunzo kwa vijana. Ameeleza kuwa Jimbo la Butiama limeendelea kunufaika na fedha za maendeleo zilizotolewa na Serikali, ambapo zaidi ya shilingi milioni 524 zimeelekezwa katika kuboresha miundombinu ya shule mbalimbali ikiwemo ujenzi wa madarasa, nyumba za walimu na mazingira bora ya kujifunzia. "Leo tunashuhudia matokeo ya dhamira ya ...

MAHERA AIPONGEZA SERIKALI KWA UWEKEZAJI WA MABILIONI KATIKA BARABARA NA MADARAJA BUTIAMA

 Mbunge wa Jimbo la Butiama, Dkt. Charles Mahera, ameipongeza Serikali kwa kuendelea kuwekeza katika maendeleo ya miundombinu ya barabara na madaraja, akisema hatua hiyo inaendelea kubadilisha maisha ya wananchi na kufungua fursa mpya za kiuchumi katika jimbo hilo. Akizungumza na Waandishi wa Habari katika Viwanja vya Bunge leo Jun 3,2026, Dkt. Mahera amesema Jimbo la Butiama limetengewa shilingi bilioni 2.2 kwa ajili ya ujenzi na uboreshaji wa barabara za kiwango cha changarawe pamoja na madaraja yaliyoathiriwa na mafuriko, huku zaidi ya shilingi bilioni 2.5 zikielekezwa katika miradi ya TARURA. Amesema uwekezaji huo unaashiria dhamira ya dhati ya Serikali ya kuhakikisha wananchi wanapata miundombinu bora inayorahisisha usafiri, usafirishaji wa mazao na upatikanaji wa huduma za kijamii. "Bajeti hii imeleta matumaini makubwa kwa wananchi wa Butiama. Barabara nyingi ambazo zilikuwa ndoto kwa muda mrefu sasa zinaenda kutekelezwa na kufungua fursa mpya za maendeleo," amesema Dkt...

WFP KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KATIKA MASUALA YA USIMAMIZI WA MAAFA NCHINI

 Na mwandishi wetu – Morogoro Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula la Duniani (World Food Programme -WFP) limesema litaendeleza mashirikiano na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuhakikisha masuala ya menejimenti ya maafa yanaendelea kutekelezwa kwa tija na malengo yaliyokusudiwa kwa kuimarisha uwezo wa kitaalamu na Kiteknolojia kwa kutumia teknolojia za kisasa. Hayo yameelezwa na Naibu Mkurugenzi wa WFP Tanzania Bi. Christine Mendes wakati wa ufunguzi wa warsha ya zoezi la uigaji la uratibu wa utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji wakati wa dharura inayoendelea mkoani Morogoro. Bi.Christine alisema ushirikiano hususan katika kuwezesha utekelezaji wa Mradi wa Field-Based Preparedness Project (FBPP), ambapo katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, mradi huo umechangia kwa kiasi kikubwa kuimarisha uwezo wa taifa katika sekta ya utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji. Aidha, alieleza kuwa zoezi la uigaji la uratibu wa utoaji wa misaada...

RAIS SAMIA, PUTIN WAKUBALIANA KUIMARISHA USHIRIKIANO KWA MAENDELEO ENDELEVU

  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ameanza rasmi ziara yake ya kiserikali nchini Urusi kwa kufanya mazungumzo ya ngazi ya juu na mwenyeji wake, Vladimir Putin, katika Ikulu ya Kremlin jijini Moscow. Katika mazungumzo hayo, viongozi hao walijadili namna ya kuimarisha ushirikiano wa muda mrefu kati ya Tanzania na Urusi katika sekta mbalimbali za kimkakati zenye mchango mkubwa kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Rais Dkt. Samia amesema ziara hiyo ni ya kihistoria na inaashiria mwanzo wa hatua mpya ya ushirikiano wenye tija kwa wananchi wa mataifa hayo mawili. Amesema Tanzania inaendelea kuona fursa kubwa za ushirikiano katika sekta ya kilimo, hususan uzalishaji wa mbolea, kilimo cha biashara na uongezaji thamani wa mazao ili kuongeza uzalishaji, ajira na ukuaji wa uchumi. Viongozi hao pia walijadili maeneo ya teknolojia za kidijitali, serikali mtandao, akili bandia (AI), sayansi ya anga na mafunzo ya teknolojia za kisasa kwa vijana na wataalamu wa Tanzan...

MAONESHO VYUO VIKUU MALAYSIA YAIBUA FURSA NYINGI KWA WANAFUNZI

 Na Mwandishi Wetu WAZAZI na wanafunzi nchini wamefurahishwa na maonesho ya vyuo vikuu Malaysia ambavyo vimewapa fursa mbalimbali za masomo nchini humo kwenye maonesho yaliyofanyika jana. Akizungumza kwenye maonesho hayo, Mratibu wa maonesho, ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Elimu Vyuo Vikuu, Global Education Link, (GEL), Abdulmalik Mollel, alisema maonesho yametoa fursa nyingi kwa vijana. Alisema vijana kutoka maeneo mbalimbali nchini wamefika kwenye maonesho hayo na kwamba kama kuna waliokosa nafasi wafike Global Education Link ambako watapatiwa fursa kama hiyo ya kuvijua vyuo hivyo “GEL inawahimiza wanafunzi, wazazi na walezi waliokosa kuhudhuria Maonesho ya Study in Malaysia katika Hoteli ya Serena kufika ofisi za GEL, ambako huduma za ushauri, udahili, scholarship na mwongozo wa kusoma Malaysia zinaendelea kutolewa kama ilivyokuwa kwenye maonesho,” alisema Mollel. Mollel alisema maonesho hayo ya Study in Malaysia yamefungua fursa za Scholarship kwa wanafunzi wa Tanzania ...

TANZANIA YAALIKWA KUWA MWENYEJI WA MAONESHO YA UFUGAJI NYUKI AFRIKA 2028

  Taasisi ya Maonesho ya Ufugaji wa Nyuki barani Afrika ijulikanayo kama Africa Bee Expo, imeialika Tanzania kuwa mwenyeji wa Maonesho ya Tano ya Ufugaji wa Nyuki Afrika yatakayofanyika mwaka 2028 na kujumuisha wafugaji wa nyuki kutoka takribani nchi 50. Mwaliko huo ulitolewa leo na Mwenyekiti wa taasisi hiyo, Bw. Fatah Ben Chouia wa Algeria, alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Mobhare Matinyi, kwenye ofisi za Ubalozi wa Tanzania jijini Algiers. Pamoja na mwaliko huo, Bw. Chouia aliwasilisha pia mwaliko wa Tanzania kuwa mgeni rasmi katika Maonesho ya Nne ya Ufugaji wa Nyuki Afrika yatakayofanyika jijini Algiers, Algeria, tarehe 3-6 Septemba, 2026, na kuziomba taasisi za serikali na watu binafsi wa Tanzania kushiriki. Balozi Matinyi aliishukuru taasisi hiyo kwa kuipa Tanzania heshima ya ugeni rasmi mwaka 2026 na uenyeji mwaka 2028 na kuahidi kwamba Serikali itaifanyia kazi mialiko hiyo kwa manufaa ya sekta hiyo ambayo hutoa fursa ya ajira mil...

MAHERA: VIJANA WA BUTIAMA WAJIPANGE KUNUFAIKA NA BILIONI 200 ZA SAMIA

 Mbunge wa Jimbo la Butiama, Dkt. Charles Mahera, amewataka vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kujipanga kikamilifu ili kunufaika na fursa mbalimbali za kiuchumi zinazotolewa na Serikali, ikiwemo fedha za Shilingi bilioni 200 zilizotengwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa ajili ya kuwawezesha vijana na wanawake nchini. Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Jun 3,2026 katika Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma Dkt. Mahera amesema Serikali inaendelea kutekeleza mipango mbalimbali ya kuinua uchumi wa wananchi kupitia mikopo na miradi ya maendeleo, huku Halmashauri ya Butiama ikiendelea kusimamia utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa makundi maalumu, ambapo asilimia 4 hutolewa kwa wanawake, asilimia 4 kwa vijana na asilimia 2 kwa watu wenye ulemavu. "Vijana wetu wanapaswa kujipanga vizuri ili waweze kunufaika na fedha hizi zinazolenga kuwawezesha kiuchumi na kuboresha maisha yao," amesema Dkt. Mahera. Mbali na mikopo hiyo, amesema wizara mba...