Skip to main content

Posts

Showing posts from June 17, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

WANANCHI WAMKATAA DIWANI MBELE YA VIONGOZI WA CCM KATA YA ZUZU DODOMA

 Wananchi wa Kata ya Zuzu, Jijini Dodoma, wameibuka na malalamiko makali yenye hisia nzito na machungu makubwa, wakimlenga Diwani wa kata hiyo kwa kumtuhumu kuhusika katika kufungwa kwa eneo la uchimbaji wa kokoto na mchanga ambalo lilikuwa mkombozi wao wa maisha kwa zaidi ya wananchi 300. Kwa sauti zilizotawaliwa na huzuni, hasira na wakati mwingine machozi yakibubujika, wananchi hao wamesimulia jinsi maisha yao yalivyoporomoka ghafla kufuatia kufungwa kwa eneo hilo, wakisema walikuwa wakitegemea uchimbaji huo kama chanzo kikuu cha kipato cha kila siku. Wamesema kupitia shughuli hizo walikuwa wakigharamia mahitaji ya familia, ada za shule za watoto na matumizi ya msingi ya nyumbani, lakini sasa wamebaki wakikabiliwa na hali ngumu ya maisha isiyo na uhakika wala matumaini. Kwa hisia kali na maumivu ya wazi, wananchi hao wamedai kuwa uamuzi wa kufungwa kwa eneo hilo ulifanyika bila kushirikishwa wala kufanyika mkutano wa pamoja wa wananchi, jambo ambalo wamesema limeongeza hasira, m...

RAIS DKT. MWINYI AWASILI JIJINI MOMBASA, KENYA

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Moi, jijini Mombasa, Kenya, leo tarehe 17 Juni 2026, kwa ziara ya kikazi ya siku mbili. Rais Dkt. Mwinyi ameambatana na ujumbe wake, wakiwemo Mhe. Mama Mariam Mwinyi na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Ngwaru Maghembe. Rais Dkt. Mwinyi amepokelewa uwanjani hapo na Waziri wa Michezo, Uchumi Ubunifu na Vijana wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Salim Mvurya Mgala, Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi, Mhe. Masoud Ali Mohamed, pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Dkt. Bernard Yohana Kibesse. Katika ziara hiyo, Rais Dkt. Mwinyi atamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika Mkutano wa 11 wa Masuala ya Bahari (11th Our Ocean Conference).

WADAU WA MADINI WAKUMBUSHWA KUZINGATIA SHERIA KUONGEZA MANUFAA KWA TAIFA

 📍DODOMA Wadau wa Sekta ya Madini wamehimizwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zinazosimamia shughuli za madini ili kuhakikisha rasilimali hizo zinaendelea kuchangia maendeleo ya taifa na kunufaisha wananchi. Mwanasheria wa Tume ya Madini, Janeth Kanyasu, amesema hayo kwenye Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park mkoani Dodoma, ambapo Tume inaendelea kutoa elimu kwa wananchi na wadau mbalimbali kuhusu masuala ya Sekta ya Madini. Amesema elimu hiyo inahusu Sheria ya Madini Sura ya 123 na kanuni zake, ikijumuisha utoaji wa leseni mbalimbali, biashara ya madini, uwekezaji, shughuli za uchimbaji na usimamizi wa mazingira ili kuhakikisha rasilimali za madini zinatumika kwa tija na kwa kuzingatia matakwa ya sheria. “Kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwa ni msingi wa kuhakikisha Sekta ya Madini inaendeshwa kwa uwazi, uadilifu na kuendelea kutoa manufaa kwa taifa na wananchi,” amesema Kanyasu. Amesema pia wananchi wanaelimishwa kuhus...