WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MKUU WA MAJESHI WA MALAWI
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Dkt. Rhimo Nyansaho (Mb), tarehe 20 Agosti 2026, amekutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi wa Malawi, Jenerali George Jaffu, ambaye yupo nchini kwa ziara rasmi ya kikazi. Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Upanga, jijini Dar es Salaam, ambapo viongozi hao wamejadili masuala mbalimbali yanayohusu ushirikiano wa kiulinzi na kijeshi kati ya Tanzania na Malawi. Katika mazungumzo hayo, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa ameeleza kuridhishwa na uhusiano mzuri na wa muda mrefu uliopo kati ya Majeshi ya Tanzania na Malawi. Amesisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha na kudumisha uhusiano huo wa kihistoria kwa manufaa ya nchi na wananchi wa mataifa hayo mawili. Kwa upande wake, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi wa Malawi, Jenerali George Jaffu, ametoa shukrani kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa msaada mbalimbali ambao umekuwa ukitolewa kwa Malawi k...