Skip to main content

Posts

Showing posts from June 2, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

WALIMU ZAIDI YA 3,000 WAONESHA UMAHIRI KATIKA MASHINDANO YA KITAIFA YA UFUNDISHAJI

 Serikali imeendelea kuimarisha juhudi za kuboresha ubora wa elimu nchini kwa kuhamasisha ubunifu na umahiri wa walimu, ambapo walimu 3,153 wamejisajili kushiriki Shindano la Taifa la Stadi za Ufundishaji la mwaka 2026, linalolenga kuibua mbinu bunifu za ufundishaji na kujifunzia ili kuongeza matokeo bora ya elimu. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma kuelekea hafla ya utoaji wa tuzo kwa washindi wa mashindano hayo, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Afidhi Ameir, amesema shindano hilo ni sehemu ya utekelezaji wa mageuzi ya sekta ya elimu pamoja na Mpango Mkakati wa Kisayansi wa Kujenga Umahiri wa Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK) kwa watoto wa elimu ya awali na wanafunzi wa madarasa ya chini. Amesema serikali inalichukulia shindano hilo kama jukwaa muhimu la kuwapa walimu nafasi ya kuonesha uwezo wao, kubadilishana uzoefu na kuibua mbinu mpya zinazoweza kuimarisha ufundishaji darasani. "Shindano hili linatoa fursa kwa walimu kuonesha umahiri wao, kuba...

VYUO VIKUU VYA MALAYSIA VYAANZA MAONESHO YA ELIMU DAR

 Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam** Tanzania na Malaysia zimefungua ukurasa mpya wa ushirikiano katika elimu ya juu kupitia ubia wa vyuo vikuu, tafiti za pamoja, ubadilishanaji wa wanafunzi na wahadhiri, ufadhili wa masomo pamoja na ushirikiano katika sayansi na teknolojia wakati vyuo vikuu tisa vikianza maonesho ya elimu leo katika hoteli ya Serena. Akizungumza katika kikao cha Kuimarisha Ushirikiano wa Elimu ya Juu Kati ya Tanzania na Malaysia** kilichofanyika katika Hoteli ya Serena, Dar es Salaam, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, **Prof. Daniel Mushi**, amesema ujio wa ujumbe wa elimu kutoka Malaysia ni wa wakati muafaka wakati Tanzania ikiendelea kuimarisha na kutangaza kimataifa mfumo wake wa elimu ya juu. Kikao hicho kiliandaliwa na kuratibiwa na **Education Malaysia Global Services (EMGS)**, chini ya Wizara ya Elimu ya Juu ya Malaysia, kwa kushirikiana na **Global Education Link Ltd (GEL)**. Prof. Mushi amesema ujio wa ujumbe huo umevitambulisha ...

WALIMU ZAIDI YA 3,000 WAONESHA UMAHITI KATIKA MASHINDANO YA KITAIFA YA UFUNDISHAJI

Serikali imeendelea kuimarisha juhudi za kuboresha ubora wa elimu nchini kwa kuhamasisha ubunifu na umahiri wa walimu, ambapo walimu 3,153 wamejisajili kushiriki Shindano la Taifa la Stadi za Ufundishaji la mwaka 2026, linalolenga kuibua mbinu bunifu za ufundishaji na kujifunzia ili kuongeza matokeo bora ya elimu. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma kuelekea hafla ya utoaji wa tuzo kwa washindi wa mashindano hayo, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Afidhi Ameir, amesema shindano hilo ni sehemu ya utekelezaji wa mageuzi ya sekta ya elimu pamoja na Mpango Mkakati wa Kisayansi wa Kujenga Umahiri wa Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK) kwa watoto wa elimu ya awali na wanafunzi wa madarasa ya chini. Amesema serikali inalichukulia shindano hilo kama jukwaa muhimu la kuwapa walimu nafasi ya kuonesha uwezo wao, kubadilishana uzoefu na kuibua mbinu mpya zinazoweza kuimarisha ufundishaji darasani. "Shindano hili linatoa fursa kwa walimu kuonesha umahiri wao, kubad...

TANZANIA, QATAR ZAFUNGUA FURSA MPYA SEKTA YA MADINI

 ✅Al Mansour Group Yaonesha Nia Kuwekeza kwenye Uongezaji Thamani wa Dhahabu, Nikeli, Kobalti na Chuma ✅Teknolojia, Mitambo, Mafunzo na Uzalishaji wa Mbolea Vyatajwa Maeneo Muhimu ya Ushirikiano ✅Wachimbaji Wadogo Waguswa 📍 Doha, Qatar Tanzania imeendelea kupanua wigo wa ushirikiano wa kimataifa katika Sekta ya Madini baada ya Timu ya Wataalam kutoka Wizara ya Madini ikiongozwa na Kamishina Msaidizi wa Madini anayesimamia Uongezaji Thamani wa Madini, Mhandisi Modest Apolinary, kufanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Kampuni ya Al Mansour Group, Mhe. Sheikh Mansour Bin Jabour Bin Jassim Al Thani, ambaye pia ni Mwanafamilia wa Kifalme wa Qatar. Mazungumzo hayo yaliyofanyika Juni 1, 2026 yalilenga kujadili fursa za uwekezaji na maeneo ya ushirikiano katika Sekta ya Madini nchini Tanzania, ikiwa ni mwendelezo wa jitihada za Serikali za kuvutia uwekezaji wa kimkakati kufuatia ziara ya Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, aliyoifanya nchini Qatar mwezi Februari 2026. Katika kikao hicho,...

YANGA YAONDOLEWA KIKWAZO CHA FIFA, YATHIBITISHA HAINA DENI

 Klabu ya Young Africans SC (Yanga) sasa ipo huru kufanya usajili wa wachezaji wapya kwa ajili ya mashindano mbalimbali ya ndani na kimataifa, ikiwemo Ligi ya Mabingwa Afrika, baada ya uongozi wa klabu hiyo kuthibitisha kuwa hakuna deni lolote linaloizuia kusajili. Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Yanga, Rogers Gumbo, amesema changamoto iliyosababisha klabu kuonekana kwenye orodha ya FIFA ya vilabu vilivyofungiwa usajili ilitokana na kutokamilika kwa baadhi ya taarifa na nyaraka zilizokuwa zinahitajika na FIFA pamoja na CAF, na si deni la kifedha kama ilivyodhaniwa na wengi.  Kwa mujibu wa Gumbo, Mei 31, 2026 ilikuwa siku ya mwisho ya muda wa ziada uliotolewa kwa klabu zilizokuwa na mashauri ya malipo, ambapo Yanga imefanikiwa kutimiza matakwa yote yaliyokuwa yanahitajika. Awali, kupitia orodha ya FIFA ya vilabu vilivyowekewa zuio la usajili, jina la Yanga lilionekana tangu Mei 3, 2026, jambo lililozua mjadala mkubwa miongoni mwa wadau wa soka nchini. Hata hivyo, taarifa ...

JESHI LA KENYA LABEBA HATIMA YA RAIS RUTO UCHAGUZI MKUU 2027

MIEZI 14 kabla ya uchaguzi mkuu wa 2027, Rais William Ruto anategemea Jeshi la Ulinzi la Kenya (KDF) kusimamia utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo inayochukuliwa kuwa nguzo muhimu katika kampeni yake ya kutafuta muhula wa pili. Kuanzia ujenzi wa viwanja vya michezo 27 kote nchini, hospitali, viwanja vya ndege, daraja hadi mradi wa kufufua Mto Nairobi, jeshi limepewa jukumu la kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati na kwa viwango vinavyohitajika. Hatua hiyo inaonekana kuashiria imani kubwa ya Rais Ruto kwa nidhamu, utaalamu na uwezo wa jeshi kusimamia miradi mikubwa ikilinganishwa na baadhi ya wizara ambazo zimelaumiwa kwa kuchelewesha utekelezaji wa miradi ya serikali. Miongoni mwa miradi inayosimamiwa na KDF ni Uwanja wa Talanta Sports City unaogharimu Sh48 bilioni jijini Nairobi, ambao sasa umepewa jina la Raila Amollo Odinga International Stadium. Uwanja huo wenye uwezo wa kuketi mashabiki 60,000 unatarajiwa kuwa moja ya miundombinu muhimu wakati Kenya itakapoandaa mi...

BUNGE LA UGANDA LAKATAA KUIDHINISHA UTEUZI WA WAZIRI WA MAMBO YA NDANI

Kampala, Uganda Kamati ya Uteuzi ya Bunge la Uganda imekataa kumuidhinisha Dk. Lawrence Muganga kuwa Waziri wa Nchi katika Wizara ya Mambo ya Ndani, katika hatua inayotajwa kuwa pigo kwa mabadiliko ya hivi karibuni ya serikali yaliyofanywa na Rais Yoweri Museveni. Dk. Muganga, ambaye ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Victoria University jijini Kampala, alikuwa miongoni mwa majina mapya yaliyowasilishwa bungeni kwa ajili ya kuhakikiwa na kuidhinishwa kabla ya kuapishwa kuingia serikalini. Hata hivyo, safari yake ya kuingia katika Baraza la Mawaziri ilisimama baada ya Kamati ya Uteuzi kueleza kutoridhishwa na maelezo aliyoyatoa kuhusu hali yake ya uraia. Kamati hiyo, iliyoongozwa na Spika wa Bunge la Uganda Jacob Oboth  Oboth, ilimtaka Muganga kutoa ufafanuzi kuhusu madai kwamba anahusishwa na uraia wa Uganda, Canada na Rwanda. Wakati wa usaili wake, Muganga alikiri kuwa na uraia wa Uganda na Canada lakini akakanusha madai ya kuwa raia wa Rwanda. Akijitetea mbele ya wajumbe wa kam...

RAIS SAMIA NI RAIS WA PILI WA TANZANIA KUFANYA ZIARA NCHINI URUSI

 Na Beda Msimbe, TBN, Moscow Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Vnukovo, uliopo Jijini Moscow kwa ajili ya Ziara ya Kitaifa, nchini Urusi Katika ziara hii ya kihistoria ikifanywa kwa mara ya pili katika historia ya uhusiano wa Tanzania na Urusi, ya kwanza ilikuwa ni miaka ya 1960 iliyofanywa na baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, Rais Samia anaendeleza kampeni kubwa ya kuhakikisha Tanzania inanufaika pia kiuchumi na uhusiano mzuri na mataifa mbalimbali  Kwa mujibu wa shughuli atakazofanya Rais Samia akiwa hapa nchini kwa lengo la kuimarisha uhusiano wa Kidiplomasia, kisiasa, kiuchumi na kihistoria baina ya Tanzania na Urusi,Rais amekuja kuiweka Tanzania katika ramani ya uwekezaji kwa ushiriki wake katika mkutano mkubwa wa uwekezaji jijini St Petersburg na pia kuona namna ya kutengeneza raslimali watu ambayo taifa inahitaji sana katika kufanikisha utekelezaji wa dira ya maendeleo ya 2050....

BEI YA PETROLI YASHUKA, SERIKALI YAWEKA RUZUKU KWENYE DIZELI

 Watumiaji wa petroli wamepata afueni mwezi Juni 2026 baada ya bei ya mafuta hayo kushuka ikilinganishwa na mwezi uliopita. Kwa Dar es Salaam, petroli sasa itauzwa kwa bei kikomo ya shilingi 4,086 kwa lita, hatua inayotarajiwa kupunguza gharama kwa watumiaji wa kawaida na baadhi ya shughuli za usafiri. Kwa upande wa dizeli, watumiaji wanakabiliwa na ongezeko dogo la bei, ambapo kwa Dar es Salaam bei kikomo imefikia Shilingi 4,333 kwa lita. Ongezeko hilo limechangiwa na kupanda kwa gharama za mafuta katika soko la dunia pamoja na kuongezeka kwa gharama za uagizaji wa bidhaa hiyo. Licha ya changamoto hizo za kimataifa, Serikali imeendelea kuchukua hatua za kulinda uchumi na wananchi kwa kuweka ruzuku ya Shilingi 534.91 kwa kila lita ya dizeli. Hatua hiyo imelenga kupunguza athari za ongezeko la bei kwa sekta muhimu kama usafirishaji, viwanda na huduma za kijamii. Mabadiliko haya yameathiriwa kwa kiasi kikubwa na vita vinavyoendelea Mashariki ya Kati, vinavyohusisha Marekani, Israeli ...

WAITARA: WALA FEDHA ZA UMMA WACHUKULIWE HATUA NA IKIBIDI WANYONGWE

 Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijijini mkoani Mara, Mwita Waitara, ameibua hisia kali Bungeni baada ya kuhoji namna ambavyo baadhi ya wananchi wanaendelea kuteseka kwa kukosa huduma muhimu huku fedha za umma zikidaiwa kutafunwa na wachache wasiowajibika. Akichangia Bajeti ya Wizara ya Fedha leo Juni 2, 2026, Jijini Dodoma, Waitara amesema ni jambo linaloumiza kuona wananchi wakihangaika kutafuta fedha za matibabu na dawa hospitalini, wakati ripoti za ukaguzi zinaendelea kuonyesha uwepo wa matumizi mabaya ya fedha za umma katika baadhi ya taasisi za Serikali. Kwa sauti ya msisitizo, Waitara ameeleza kuwa fedha zinazotengwa na Bunge zinapaswa kuwafikia wananchi na kuleta maendeleo yaliyokusudiwa, badala ya kupotea mikononi mwa watu wachache wanaokwamisha juhudi za Serikali na matarajio ya wananchi. “Leo hii kuna mwananchi anaondoka hospitalini bila dawa kwa sababu hakuna fedha za kutosha. Wakati huo huo, ripoti za ukaguzi zinaonyesha kuna watu wamechezea fedha za umma. Hili halipaswi ku...

SERIKALI YAWEKA MIKAKATI MIPYA YA KUCHOCHEA UCHUMI, KULIPA MADENI NA KUIMARISHA USIMAMIZI WA FEDHA ZA UMMA

SERIKALI imeanika vipaumbele vinane vya kimkakati vinavyolenga kuujenga uchumi imara, kuimarisha uwajibikaji wa kifedha na kuongeza kasi ya maendeleo ya Taifa katika mwaka wa fedha 2026/27. Akiwasilisha Bajeti ya wizara ya Fedha Kwa mwaka wa Fedha 2026/2027 leo Jun 2,2026 Bungeni Jijini Dodoma, Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb.), amesema Serikali itaendelea kusimamia kwa umakini uchumi wa Taifa kwa lengo la kufikia ukuaji wa asilimia 6.3, kudhibiti mfumuko wa bei katika kiwango cha tarakimu moja na kuhakikisha akiba ya fedha za kigeni inaendelea kuwa katika viwango vinavyokidhi mahitaji ya nchi. Katika kuimarisha nidhamu ya matumizi ya fedha za umma, Serikali imepanga kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato, ugawaji wa rasilimali na usimamizi wa bajeti ili kuhakikisha fedha za wananchi zinatumika kwa tija na kuleta matokeo yanayokusudiwa. Hatua nyingine muhimu ni kuendelea kulipa kwa wakati madeni ya Serikali, ambapo zaidi ya Shilingi trilioni 15.1 zimetengwa kw...

MAPATO YA MICHEZO YA KUBAHATISHA YAFIKIA SH. BILIONI 18.76, BAHATI NASIBU YA TAIFA YAZALISHA AJIRA 484

 Serikali imeendelea kuimarisha usimamizi wa sekta ya michezo ya kubahatisha nchini, hatua iliyowezesha ukusanyaji wa Shilingi bilioni 18.76 hadi Aprili 2026 pamoja na kudhibiti kwa ufanisi shughuli haramu zinazohusiana na sekta hiyo. Akiwasilisha Bungeni jijini Dodoma mapitio ya utekelezaji wa mpango na bajeti ya mwaka 2025/26 pamoja na makadirio ya mwaka 2026/27, Waziri wa Fedha, Khamis Mussa Omar, amesema Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania imefanikiwa kutoa leseni 7,747, kufanya kaguzi tisa za kiudhibiti na kutekeleza operesheni tatu maalumu za kukabiliana na michezo haramu ya kubahatisha. Waziri Omar amesema mafanikio hayo yanaenda sambamba na juhudi za kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kucheza kwa uwajibikaji kupitia kampeni za “Elimika na GBT”, “Mkeka Unachana” na “Wakati Wao Bado”, ambazo zimeendelea kuwafikia wananchi katika maeneo mbalimbali nchini. Aidha, amesema Bahati Nasibu ya Taifa iliyoanzishwa Aprili 2025 imeendelea kuwa chachu ya maendeleo ya kijamii na kiuch...

SERIKALI KUIMARISHA MIFUMO YA USIMAMIZI WA MAAF

 Na mwandishi wetu, Morogoro SERIKALI imeendelea kuimarisha mifumo ya uratibu, kujiandaa na kukabiliana na maafa ili kuhakikisha misaada ya kibinadamu inayotolewa inawafikia walengwa kwa wakati, ufanisi na kwa kuzingatia viwango vya kimataifa. Hayo yameelezwa leo tarehe 02 Juni, 2026 na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Usimamizi wa Maafa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Kanali Selestine Masalamado, wakati wa ufunguzi wa warsha ya zoezi la uigaji la uratibu wa utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji wakati wa dharura, mkoani Morogoro. Amesema utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji wa dharura ni nguzo muhimu zinazowezesha kuokoa maisha ya wananchi walioathiriwa na maafa, kupunguza mateso ya waathirika na kuharakisha urejeshaji wa hali za kawaida katika maeneo yaliyoathirika. “Kwa kutambua umuhimu huo, Serikali imeendelea kuimarisha mifumo ya uratibu, kujiandaa na kukabiliana na maafa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakiki...