Kwa miezi kadhaa sasa, siasa za Uganda zimeendelea kutikiswa na wimbi la tuhuma, uchunguzi wa kifedha na vita ya chini kwa chini ya kuwania madaraka ndani ya Bunge la taifa hilo, huku jina la Spika Anita Among likiendelea kutawala mijadala ya kisiasa nchini humo. Among, ambaye kwa muda mrefu alionekana kuwa mmoja wa wanasiasa wenye nguvu kubwa ndani ya utawala wa Rais Yoweri Museveni, sasa anakabiliwa na presha kubwa kisiasa kufuatia tuhuma za ufisadi, matumizi mabaya ya fedha za umma pamoja na uchunguzi unaodaiwa kuwagusa baadhi ya viongozi waandamizi serikalini. Kupanda kwake kisiasa kulikuwa kwa kasi kubwa. Baada ya kifo cha aliyekuwa Spika Jacob Oulanyah mwaka 2022, Anita Among alichaguliwa kuongoza Bunge na haraka akajijengea ushawishi mkubwa ndani ya chama tawala cha NRM pamoja na miongoni mwa wabunge. Uwezo wake wa kusimamia mijadala ya Bunge kwa msimamo mkali ulimfanya kuwa mmoja wa watu muhimu zaidi ndani ya mfumo wa utawala wa Museveni. Lakini nyuma ya nguvu hiyo y...
Marato tv - Sauti ya Jamii