Naibu Katibu Mkuu (ELIMU) Ofisi ya Rais TAMISEMI Dkt. Charles Msonde amewataka Watendaji wa Mikoa, Halmashauri na ngazi ya msingi kuwa waadilifu, kujiamini na kufuatilia miradi ya maendeleo ili kuleta ufanisi na kulinda thamani ya fedha za Serikali. Dkt. Msonde ametoa kauli hiyo leo tarehe 31 Julai, 2024 Chuo Cha Ualimu Patandi Jijini Arusha wakati akifunga mafunzo ya siku 3 kwa Maafisa Elimu Mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Manyara na Tanga, Maafisa TEHAMA na Waratibu wa Mradi ngazi ya Mkoa, Maafisa Elimu Sekondari, Maafisa Manunuzi na Ugavi ngazi ya Halmashauri, Waratibu wa mradi ngazi ya Halmashauri na Wakuu wa Shule kuhusu utekelezaji wa miradi ya shule za sekondari (SEQUIP). “niwatake wasimamizi na wataalamu wote wa elimu na Idara mwambata katika usimamizi wa Miradi mkaimarishe usimamizi na kuongeza ubunifu katika utatuzi wa changamoto zinazoathiri shughuli za ujenzi wa miundombinu ya shule. Aidha, mkasimamie vema utekelezaji wa maboresho yanayofanyika mara kwa mara katika...
Marato tv - Sauti ya Jamii