Skip to main content

Posts

Showing posts from June 3, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Waziri Mchengerwa Awafunda Walimu

  Na John Mapepele  Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa ametoa rai kwa walimu nchini kuwa wazalendo na kuzingatia weledi ili kuongeza ufaulu wa wanafunzi.  Mhe. Mchengerwa ametoa rai hiyo kwenye mkutano wa walimu na wadau wa elimu  wa Wilaya ya Rufiji uliofanyika kwenye ukumbi wa shule ya Sekondari ya Wasichana Bibi Titi Mohamed, ambapo yeye mwenyewe pia alitunukiwa tuzo ya heshima ya kutambua mchango wake katika sekta ya elimu wilayani Rufiji. "Katika hali ya kawaida  Serikali imeboresha mazingira na miundombinu ya sekta ya elimu kilichobaki ni kwa sisi walimu kutanguliza uzalendo ili kuinua kiwango cha elimu katika ngazi zote" . Amesisitiza Mhe. Mchengerwa  Aidha, amesisitiza walimu kutambua wajibu wao na kwamba Serikali haitaweza kusita kuwachukulia hatua za kinidhamu  Walimu na Maafisa Elimu ambao watakuwa wazembe katika utekelezaji wa majukumu yao. Katika taarifa ya Wilaya ya Rufiji kwa Mhe. Waziri, iliyoandaliwa na...

Dkt. Nindi: Tume ya Umwagiliaji ipanue wigo wa huduma nchini

📍 NIRC Dodoma.  Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo anayeshughulikia Ushirika na Umwagiliaji, Dkt. Stephen Nindi, ameitaka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kutanua wigo wa kazi zake kwa kuwafikia wadau jumuishi wa sekta nyingine lengo likiwa ni  kuhakikisha kilimo cha umwagiliaji kinakuwa na tija katika maendeleo ya jamii.   Nindi amesema hayo alipotembelea banda la Tume ya Taifa ya Umwagiliaji viwanja vya Jakaya Kikwete jijini Dodoma katika maadhimisho ya wiki ya Mazingira Duniani. Dkt. Nindi amesema kuwa pamoja na kazi nzuri inayofanywa na Tume, ni vyema taasisi hiyo muhimu katika sekta ya kilimo ikaendelea kutanua wigo ili kuwafikia wadau wengine, mbali na wakulima wa mazao pekee. “Wakulima wa umwagiliaji si tu wanajikita kwenye kilimo, bali pia wanajihusisha na uvuvi, ufugaji na matumizi ya maji ya nyumbani. Ni muhimu kuweka mikakati inayozingatia uhitaji huu mtambuka ili kuongeza tija na matumizi endelevu ya rasilimali," amesema Dkt. Nindi.   Katika kuende...

Dkt.Kijaji Awaonya Wananchi Uharibifu Wa Mazingira na Athari za Mifuko ya Plastiki

Na Mwandishi wetu Jovina Massano. Watanzania wameonywa kuachana na matumizi ya mifuko ya plastiki kwani athari zake ni kubwa kwa afya ya binadamu na viumbe hai pamoja na mazingira kwa ujumla. Wito huo umetolewa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji alipotembelea mabanda ya maonesho wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani Juni 2, 2025 yanayoendelea kwenye Viwanja vya Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete jijini Dodoma. Mhe. Dkt. Kijaji alisema kuwa mifuko ya plastiki isipodhibitiwa ikitupwa ovyo na kuingia kwenye vyanzo vya maji vikiwemo bahari na maziwa ina athari kubwa kwa samaki na mazalia yake. “Sote tutatambue mifuko hii si salama kwa maisha yetu pamoja na mifugo na samaki, kwa mfano inapoingia baharini samaki wenyewe wakimeza mifuko hii ya plastiki haiwezi kumeng’enywa na mwisho wake hufa". Aidha Waziri Dkt. Kijaji ametoa wito kwa wafugaji wote nchini kuzingatia ufugaji ulio endelevu usioweza kuharibu mazingira ikiwemo kukata miti ovyo kwa ajili ya m...

Balozi Nchimbi Msibani kwa Mzee Mongella

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, akisaini kitabu cha maombolezo na kumpatia pole, Mama Gertrude Ibengwe Mongella, familia yake na waombolezaji wengine, kwa msiba wa Mzee Silvin Ibengwe Emmanuel Mongella, ambaye ni mwenza wa Mama Mongella, leo Jumanne, tarehe 3 Juni 2025, eneo la Makongo juu, jijini Dar Es Salaam.  Marehemu Mzee Mongella (85), ambaye pia ni baba mzazi wa John Mongella, Naibu Katibu Mkuu wa CCM (bara), alifariki tarehe 31 Mei 2025, na mazishi yake yamepangwa kufanyika huko Mwanza, tarehe 7 Juni 2025.

Mabilionea Watatoka Mara Kupitia Sekta ya Madini" Rc Mtambi"

Na Shomari Binda-Musoma MKUU wa mkoa wa Mara Kanali Evans Mtambi amesema kama ataendelea kuwepo mkoa wa Mara atahakikisha wanapatikana mabilionea kupitia sekta ya madini. Kauli hiyo ameitoa leo juni 3,2025 kwenye uwanja wa shule ya msingi Mukendo wakati wa ufunguzi wa maonyesho na kongamano kuhusu masuala ya madini. Amesema mkoa wa Mara una hazina kubwa ya rasilimali nyingi lakini upande wa madini wataibuka mabilionea watakao uinua juu zaidi mkoa huo. Kanali Mtambi amewaambia wachimbaji wadogo na wakubwa wanaofanya shughuli za uchimbaji kwenye mkoa huo kuwa watumie fursa ya madini yaliyopo mkoani Mara kujiinua kiuchumi. Amesema ndani ya siku 4 za maonyesho na kongamano la madini kuzitumia kujifunza teknolojia bora ya uchimbaji na kuchimba kwa tija. Mkuu huyo wa mkoa wa Mara amesema hakuna shaka ya kupatikana kwa mabilionea hao kwa kuwa madini yapo na yakichimbwa kwa tija mafanikio yataonekana. Amesema vijana wasidanganywe na mtu yoyote wakiwemo wanasiasa kwani serikali ipo karibu nao n...

Waziri Mkuu Ahani Msiba Wa Mdogo wa Waziri Lukuvi

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Juni 3, 2023 amehani msiba wa  marehemu Mtwa Xaviery Lukuvi ambaye ni mdogo wa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera,Bunge na Uratibu , William Lukuvi (kulia), nyumbani kwa marehemu, Mbezi Beach jijini Dar es salaam.

Rweyemamu wa Bukoba Alambwa Kifungo Cha Maisha Kwa Kosa la Kubaka na Kulawiti

 Na Angela Sebastian ;Bukoba RWEYEMAMU Kashunja (35) bodaboda mkazi wa Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera na mwenzake wamehukumiwa kifungo cha maisha jera na mwingine mmoja akihukumiwa kufungwa miaka 30 kutokana na makosa ya ubakaji na ulawiti. Amon Mang’era ni wakili wa Serikali ameeleza hayo wakati akiongea na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali ofisini kwakwe mjini Bukoba ambapo alimtaja Rweyemamu maarufu kama baba P ametiwa hatiani na mahakama ya hakimu mkazi Wilaya ya Bukoba,kwa kosa la kumlawiti mtoto wa miaka sita baada ya mahakama hiyo kulidhika na ushahidi wa upande wa Jamhuri pasipo kuacha shaka. “Kati ya mwezi Aprili na Mei mwaka jana mshitakiwa Rweyemamu alimlawiti mtoto wa miaka mitano kwa wakati huo ambapo kwa sasa ana umri wa miaka sita na wakati shauri likiendelea mtuhumiwa na mdhamini wa kwanza ambaye ni mke wake walitoroka ambapo kesi iliendelea ambapo Mei 30 mwaka huu mahakama ilitoa hukumu na kumtia hatiani kwa kufungwa jera maisha kutokana na kifungu cha 1...