Skip to main content

Posts

Showing posts from June 9, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

WAGANGA WA TIBA ASILI NA MBADALA HAPA NCHINI WASHAURIWA KUSAJILI NA KUSALIMISHA NYARA

Na Mwandishi wetu Jovina Massano Waganga wa tiba asili na mbadala hapa nchini washauriwa kusalimisha na kusajili nyara wanazotumia katika shughuli zao ili kuepuka adhabu na kukamatwa. Hayo yamesemwa na Katibu Mtendaji wa Umoja wa Machifu Tanzania Mtemi Nyamilonda wa tatu Harun Mkomangwa jijini Mwanza mbele ya Mhifadhi mkuu Kituo Cha TAWA Mwanza kamanda Venance Mkamwa wakati wa zoezi la utoaji elimu ya uhifadhi iliyotolewa na Mamlaka ya Usimamizi wa wanyamapori Tanzania (TAWA). Mtemi Nyamilonda wa tatu amesema kumiliki nyara kihalali kutasaidia kuepuka adhabu za kukamatwa na faini kwa watumiaji zitakazopelekea kuwaondolea hofu katika uteketezaji wa majukumu yao. Aidha amewasisitiza viongozi walioshiriki katika zoezi hilo la elimu kuhakikisha wanawaelimisha waganga wa tiba asili na mbadala ambao hawakuweza kufika ili nao waweze kunufaika na umiliki nyara kihalali na kufuata miongozo taratibu na sheria zilizowekwa. "Tunaishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuweza kutusikiliza ...

MSD YAIHAKIKISHIA KAMATI YA BUNGE UBORA WA HUDUMA KATIKA UTEKELEZAJI WA BIMA YA AFYA KWA WOTE

 Dodoma. Bohari ya Dawa (MSD) imeihakikishia Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI kuwa itaendelea kuimarisha upatikanaji wa bidhaa za afya zenye ubora, kwa wakati na kwa kiwango kinachohitajika kuelekea utekelezaji wa awamu ya pili ya Bima ya Afya kwa Wote. Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Mavere Tukai, mbele ya Kamati hiyo Juni 9, 2026 mara baada ya wajumbe wa Kamati hiyo kufanya ziara katika Ghala Kuu la MSD Dodoma kwa lengo la kujionea shughuli za kila siku za taasisi hiyo katika uzalishaji, ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za afya. “Sisi tumeshajipanga, na utayari wetu unategemea kwa kiasi kikubwa upatikanaji wa rasilimali. Tayari tumewasilisha mahitaji yetu Serikalini kwa ajili ya kuwezesha utekelezaji wa mpango wa Bima ya Afya kwa Wote na kuhakikisha wananchi wanapata huduma zinazostahili,” amesema Mavere. Amesema MSD inaendelea kujiandaa kukidhi ongezeko la mahitaji ya bidhaa za afya litakalotokana na utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wo...

DK SAMIA: TANZANIA HAIFUNGAMANI NA UPANDE WOWOTE, INASAKA FURSA ZA KIUCHUMI KILA PEMBE YA DENIAL

Na Beda Msimbe, TBN, aliyekuwa Petersburg, Urusi Ulimwengu wa sasa wa diplomasia ya kijiografia unatawaliwa na ushindani mkubwa wa nguvu za kisiasa na kiuchumi kati ya mataifa makubwa ya Magharibi na yale ya Mashariki.  Katika mazingira haya, mataifa yanayoendelea mara nyingi hujikuta yakitazamwa kwa darubini ya shaka pale yanapochukua hatua za kimkakati kupanua wigo wa washirika wao wa kimaendeleo.  Ziara ya hivi karibuni ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan nchini Urusi, imezua minong'ono na hisia mbalimbali miongoni mwa wachambuzi wa mambo, wengi wao wakihofia kuwa huenda Tanzania sasa inabadili mwelekeo wake wa sera ya mambo ya nje kwa kuitupa mkono Magharibi na kugeukia upande wa Mashariki.  Hofu hii haina msingi wowote, kwani majibu thabiti na ya kizalendo aliyoyatoa Rais Samia mbele ya waandishi wa habari pembezoni mwa Jukwaa la Kimataifa ya Uchumi la St. Petersburg (SPIEF) nchini Urusi, yanadhihirisha ukomavu wa diplomasi...

RAIS SAMIA : TANZANIA INATAFUTA WASHIRIKA WA KIUCHUMI, HAIEGEMEI UPANDE WOWOTE

 Na Beda Msimbe, TBN,  Petersburg, Urusi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amezitaka nchi za Magharibi na wachambuzi wa mambo ya kisiasa kuondoa hofu yoyote ile kuhusu ushirikiano wa nchi yake na Urusi, akisisitiza kuwa Tanzania ni nchi isiyofungamana na upande wowote na inaongozwa na diplomasia ya kiuchumi yenye kulinda maslahi ya taifa kwanza. Kauli hiyo imekuja kufuatia maswali na hisia zilizoibuka kuhusu ziara yake nchini Urusi, ambapo baadhi ya waandishi wa habari walieleza uwepo wa dhana kwamba Tanzania huenda inaikabili mgongo nchi za Magharibi na kugeukia upande wa Mashariki kiitikadi.  Akizungumza pembezoni mwa Jukwaa la Uchumi la Kimataifa la St. Petersburg (SPIEF), Rais Samia alifafanua kuwa Tanzania haihamishi nguvu zake kutoka upande mmoja kwenda mwingine, bali inatanua wigo wa washirika ili kukuza uchumi na kuinua maisha ya wananchi wake. Rais alieleza kuwa msimamo huu una mizizi mirefu ya kihistoria tangu enzi za ...

TUNAAMUA MAMBO YETU KWA MASLAHI YA NCHI-WASIRA

 Aelezea ziara ya Rais Samia nchini Urusi Na MWANDISHI WETU SAME - Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Stephen Wasira, amesema ziara ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan nchini Urusi inathibitisha dhamira ya Tanzania kutofungamana na upande wowote. Akizungumza na wanachama wa CCM na wananchi wilayani Same mkoani Kilimanjaro Juni 9, 2026 wakati wa kuhitimisha ziara ya kukagua uhai wa Chama na utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi, Wasira alisema waasisi wa Taifa wakiongozwa na Mwalimu Julius Nyerere waliitaka Tanzania kukaa katikati pale pande mbili zinapogombana. “Tulitaka tuwe huru na uhuru uwe wa kudumu. Kazi yetu ni kudumisha uhuru na kudumisha uhuru ni kutupa haki ya kuamua mambo tunayoona yanatufaa sisi, sio kutegemea wengine wakuambie mfanye nini,” alisema. Akizungumzia maswali kuhusu ziara ya Rais Samia Urusi, Wasira alidai: “Na juzi Rais wetu ameenda Urusi wengine wanauliza ameenda kufanya nini. Mbona alivyoenda China hamkuuliza, mbona alipoenda Marekani hamkuuliza. Akienda Urusi...

TANZANIA NA SINGAPORE ZAKUBALIANA KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI

 Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, na Rais wa Singapore, Tharman Shanmugaratnam, wamekubaliana kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi, biashara na uwekezaji ili kuongeza manufaa kwa wananchi wa mataifa hayo mawili kupitia miradi mbalimbali ya maendeleo. Kupitia makubaliano hayo, yalitofanyika mapema hii leo June 9, Ikulu jijini Dar es Salaam, Rais samia ameeleza kuwa licha ya ukuaji wa biashara kati ya Tanzania na Singapore, kiwango cha sasa cha dola milioni 299 za Marekani bado hakijafikia matarajio ya pande zote. Kwa sasa Singapore imewekeza katika miradi 36 nchini Tanzania, huku makubaliano yaliyofikiwa yakilenga kuongeza uwekezaji, biashara na fursa mpya za ushirikiano katika sekta mbalimbali za uchumi. Tanzania pia imeiomba Singapore kufungua ubalozi wake nchini ili kuimarisha zaidi mahusiano ya kidiplomasia na kiuchumi, pamoja na kuanzisha mfumo wa mashauriano ya mara kwa mara kwa ajili ya kuratibu maeneo ya ushirikiano. Katika sekta ya kilimo, nchi hizo zimeonyesha nia ya k...

RC MARA AWAPOKEA MAOFISA WA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA, AWAHAKIKISHIA HALI YA USALAMA NI SHWARI

Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Kanali Evans Mtambi, leo Juni 09, 2026 amekutana na kuzungumza na ujumbe wa maofisa kutoka Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (MMUT), Jeshi la Wananchi wa Tanzania walioko mkoani humo kwa kazi ya ukaguzi wa utayari wa ulinzi wa mipaka. Ujumbe huo uliongozwa na Mkurugenzi wa Operesheni Jeshini, Kanali Victor Magare pamoja na Mkurugenzi wa Mawasiliano Jeshini, Kanali Herry Juma Masokola, ambao wamefika mkoani Mara kufanya tathmini ya hali ya kiusalama na kuangalia namna vikosi vilivyo tayari kulinda mipaka ya nchi. Akizungumza wakati wa mapokezi hayo, Mhe. Mtambi aliwakaribisha wageni hao na kuwahakikishia kuwa Mkoa wa Mara uko salama, huku wananchi wakiendelea na shughuli zao za kiuchumi na kijamii bila hofu. Ameongeza kuwa Serikali ya Mkoa itaendelea kushirikiana kwa karibu na vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikisha amani na utulivu vinaendelea kudumishwa, hususan katika maeneo ya mipakani. Ujumbe huo wa MMUT unaendelea na ziara yake ya kikazi mkoani Mara kwa le...

WANANCHI WATAKIWA KUTHAMINI FEDHA ZA SERIKALI.

  Na Mwanamkuu Mwandoro, Tanga  WANANCHI mkoani tanga wametakiwa kuthamini fedha zinazowekezwa na serikali katika ujenzi wa miundombinu hasa barabara. Wito huo umetolewa na meneja wa TARURA mkoa wa Tanga George Tarimo alipokuwa akitoa taarifa ya miradi ya barabara inayotarajiwa kuzinduliwa na mwenge wa uhuru na mingine kuwekewa jiwe la msingi. "Gharama zinatotumika ni kubwa sana sasa ni vema wananchi Kila mmoja akawa milinzi wa mwingine,kutotupa taka katika mitaro ambayo husababisha mitaro hiyo kuziba na kuharibika Kwa Barbara kitu ambacho ni hasara Kwa serikali",alisema Tarimo.  Aidha Tarimo alisema kuna miradi nane ambayo itapitiwa na mwenge wa uhuru mwaka huu ambayo ipo katika wilaya ya Kilindi,Pangani Handeni ,Korogwe, Lushoto,Bumbuli Muheza na Tanga jiji. Pamoja na hayo pia mradi wa Kilindi Dc ni Daraja ambalo lipo kwenye (hatua ya Box), na barabara ya mapanga Mlingotini ambayo gharama yake ni milioni 22.5 ambayo inajengwa na mkandasi Negron Buiders Company limited ...

BUTIAMA KUNUFAIKA NA MPANGO WA UJENZI WA SOKO LA KIABAKARI

 Serikali imeeleza mpango wake wa kuendelea kuisaidia Halmashauri ya Wilaya ya Butiama katika jitihada za kuboresha miundombinu ya biashara, hususan ujenzi wa soko katika eneo la Kiabakari, linalokua kwa kasi kiuchumi. Akijibu swali la Mbunge wa Butiama, Mheshimiwa Charles Mahera leo Jun 9,2026 Bungeni Jijini Dodoma,Naibu Waziri wa TAMISEMI, Dkt. Festo Dugange amesema kuwa Butiama ni miongoni mwa halmashauri zenye mapato ya ndani ya chini, hivyo Serikali inaendelea na mkakati wa kuziwezesha halmashauri hizo kuongeza vyanzo vya mapato. Dkt. Dugange amebainisha kuwa eneo la Kiabakari tayari limetengwa kwa ajili ya ujenzi wa soko, ambalo litakuwa na manufaa makubwa kwa wananchi, hususan wanawake wanaojishughulisha na biashara katika eneo hilo, pamoja na kuongeza mapato ya ndani ya halmashauri. Aidha, Serikali imeitaka Halmashauri ya Butiama kuanza kutenga fedha ndani ya bajeti yake kwa ajili ya kuanzisha ujenzi wa soko hilo, huku ikiahidi kuendelea kusaidia mradi huo kadri ya upatika...