Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

JESHI LA KENYA LABEBA HATIMA YA RAIS RUTO UCHAGUZI MKUU 2027

MIEZI 14 kabla ya uchaguzi mkuu wa 2027, Rais William Ruto anategemea Jeshi la Ulinzi la Kenya (KDF) kusimamia utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo inayochukuliwa kuwa nguzo muhimu katika kampeni yake ya kutafuta muhula wa pili.

Kuanzia ujenzi wa viwanja vya michezo 27 kote nchini, hospitali, viwanja vya ndege, daraja hadi mradi wa kufufua Mto Nairobi, jeshi limepewa jukumu la kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati na kwa viwango vinavyohitajika.

Hatua hiyo inaonekana kuashiria imani kubwa ya Rais Ruto kwa nidhamu, utaalamu na uwezo wa jeshi kusimamia miradi mikubwa ikilinganishwa na baadhi ya wizara ambazo zimelaumiwa kwa kuchelewesha utekelezaji wa miradi ya serikali.

Miongoni mwa miradi inayosimamiwa na KDF ni Uwanja wa Talanta Sports City unaogharimu Sh48 bilioni jijini Nairobi, ambao sasa umepewa jina la Raila Amollo Odinga International Stadium.

Uwanja huo wenye uwezo wa kuketi mashabiki 60,000 unatarajiwa kuwa moja ya miundombinu muhimu wakati Kenya itakapoandaa michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) mwaka 2027.

Mradi mwingine mkubwa ni Hospitali ya Rufaa na Mafunzo ya Matibabu ya Kisasa mjini Eldoret inayogharimu Sh50 bilioni na yenye uwezo wa kuhudumia wagonjwa 4,000.

Hospitali hiyo inajengwa kwa awamu mbili na inatarajiwa kuwa mojawapo ya hospitali kubwa zaidi barani Afrika.

Pia kuna mradi wa kufufua Mto Nairobi wenye thamani ya Sh50 bilioni unaolenga kubadilisha mazingira ya mto huo kwa kujenga nyumba za kijamii, njia za watembea kwa miguu, njia za baiskeli, mifumo ya maji taka, daraja na maeneo ya burudani.

Katibu katika Wizara ya Ulinzi, Dkt Patrick Mariru, alisema serikali imeamua kutumia utaalamu wa KDF katika uhandisi na usimamizi wa miradi ili kuhakikisha miradi ya kitaifa inakamilika kwa wakati uliowekwa.

“Chini ya uongozi wa Rais, jeshi linasimamia ujenzi wa miradi ya maji, afya, barabara na michezo ili kusaidia kufanikisha maono ya kuifanya Kenya kuwa taifa lenye uchumi wa kiwango cha juu,” alisema.

Aliongeza kuwa jukumu la KDF si kutoa zabuni wala kupanga bajeti, bali ni kusimamia utekelezaji na kuhakikisha ubora wa kazi unaafikiwa.

Mbunge wa Belgut na Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi katika Bunge la Kitaifa, Nelson Koech, alisema kuhusishwa kwa jeshi katika miradi hiyo ni ishara kuwa baadhi ya wizara zimeshindwa kutekeleza miradi kwa ufanisi.

“Kwa jeshi kupewa jukumu hili ni lawama ya moja kwa moja kwa baadhi ya wizara. Inaonyesha kuwa kuna changamoto za ufanisi na ndiyo maana serikali imeamua kutumia uwezo wa KDF kuhakikisha miradi inakamilika,” alisema.

Kwa mujibu wa Bw Koech, jeshi lina sifa ya nidhamu, uwajibikaji na kutovumilia ufisadi, jambo ambalo limefanya serikali kuliamini katika kusimamia miradi yenye thamani ya mabilioni ya pesa.

Wakili Kipkirui Kemboi Kap Telwa, alisema hatua ya Rais Ruto kupatia KDF jukumu kubwa katika miradi ya maendeleo inaonyesha jinsi anavyotaka kuona ahadi alizotoa kwa wananchi zikitimizwa kabla ya uchaguzi mkuu ujao.

“Hii inaonyesha kuwa Rais ameona changamoto zilizopo katika baadhi ya idara za serikali na ameamua kuamini jeshi kusimamia utekelezaji wa miradi hiyo,” alisema.

Hata hivyo, alionya kuwa serikali inapaswa kuwa makini ili kuepuka kuingiza jeshi katika siasa za uchaguzi.

“Ni jambo jema kutumia uwezo wa KDF, lakini ni muhimu kuhakikisha jeshi halihusishwi katika siasa kwa sababu limeendelea kuwa taasisi inayoheshimika nchini na barani Afrika,” alisema.

Miongoni mwa miradi mingine inayosimamiwa na jeshi ni Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Bomas (BICC) kinachogharimu Sh42 bilioni, uwanja wa ndege wa Lokichogio Turkana, hospitali mpya katika Kaunti ya Narok na viwanja kadhaa vya michezo katika kaunti mbalimbali.

Dkt Mariru alisema viwanja 27 vya michezo nchini kwa sasa viko chini ya usimamizi wa jeshi, hatua ambayo haijawahi kushuhudiwa katika historia ya Kenya.

“Katika miezi miwili ijayo tutakuwa tumekamilisha na kukabidhi Uwanja wa Talanta kwa Rais. Huu ni ushahidi wa umakini wa jeshi katika kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati,” alisema.

Kwa sasa, viwanja vya michezo katika maeneo ya Kericho, Bomet, Nandi, Kisii, Nyamira, Nakuru, Siaya, Lodwar, Kitale, Eldoret, Meru, Mavoko, Kilifi, Busia, Kakamega, Vihiga, Maua, Wajir na Mandera ni miongoni mwa vinavyosimamiwa na KDF. 

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...