Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Vitendo Vya Ukatili wa Kijinsia Mkoa wa Mara Ukiwemo na Ukeketaji Vimeshuka Hadi Kufikia Asilimia 28






Fresha Kinasa- Mara

WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Makundi Maalum Dkt.  Dorothy Gwajima amesema mkoa wa Mara umeendelea kupiga hatua katika kupambana na vitendo vya Ukatili wa Kijinsia ukiwemo ukeketaji ambao umeshuka  hadi asilimia  28, na kutoka nafasi ya kwanza  kama ulivyokuwa  hapo awali.   Huku mikoa ya Arusha na Manyara ikiitaja  kuongoza hapa nchini  kwa kufungana kwa  kuwa na asilimia 43.  

Waziri Dkt.  Gwajima ameyasema hayo Dicemba 9, 2024, katika kilele cha maadhimisho ya siku 16 za kupinga vitendo vya ukatili wa Kijinsia Kitaifa  zilizofanyika Uwanja wa shule ya Sekondari Ingwe  Nyamongo Wilayani Tarime Mkoani Mara. Huku akisema ukeketaji umepungua kwa kiwango Cha asilimia 2 kitaifa.

Ambapo wadau mbalimbali kutoka Serikalini, Mashirika ya Kiraia, Taasisi za Dini, Wazee wa Kimila, na Wananchi wameshiriki  katika kilele hicho chini ya kauli mbiu   ya mwaka huu isemayo "kuelekea miaka 30 ya Beijing chagua kutokomeza ukatili wa Kijinsia'' 

Dkt.  Gwajima amesema, Mkoa wa Mara kwa sasa umeendelea kupiga hatua tofauti na awali ambapo vitendo hivyo vilikuwa vimeshika kasi. Huku akihimiza Wananchi kuendelea kuachana na mila na desturi zinazochochea  vitendo hivyo ambavyo vinarudisha nyuma juhudi za maendeleo.

"Ukeketaji  Mara umeendelea kupungua kwa mujibu wa Tafiti za  kitaifa za Idadi  ya Watu na Afya Tanzania  za mwaka 2022, Mkoa wa Mara una asilimia 28, maeneo mengine umeshuka asilimia   kwa asilimia 2 na maeneo mengine umepanda,  wakati Mkoa wa Arusha una asilimia 43, Manyara asilimia 43, Singida asilimia 20, Tanga asilimia 19, na Dodoma asilimia 18. Napongeza Mkoa Mara kuendelea kufanya juhudi kupunguza kiwango Cha  ukeketaji."amesema Dkt. Gwajima.  

"Mambo ya  ukatili, Tuanze kuiondoa  Mara kwenye sura ya ukatili wameshaitikia, elewa pasi na shaka kwa sababu ya Viongozi wenu wakuu wote wanashirikiana pamoja na Jamii na Wazee wetu wa kimila."amesema Dokt.  Gwajima. 

Aidha, ameyataka Mashirika ya Kiraia  na Wadau wa mapambano ya Ukatili wa Kijinsia kuongeza Kasi ya utoaji wa elimu hasa kwa wanawake wanaoishi Vijijini kwani ndiko idadi kubwa ya vitendo vya Ukatili vimekuwa vikifanywa na Serikali itazidi kushirikiana na taasisi zote na Jamii nzima kujenga Taifa imara lisilo vitendo vya ukatili.  

Aidha amewashukuru Wazee wa Kimila kutoka Koo 12 za kabila la kikurya kwa kuendelea kuiunga mkono Serikali kupiga vita vitendo vya ukeketaji na amewahimiza kuzidi kutoa elimu katika Jamii akisema madhara ya ukatili yanarudisha nyuma juhudi na jitihada za maendeleo na kuhatarisha afya na usalama wa wanawake hasa wanaokumbana na ukeketaji, vipigo ndoa za utotoni na ukatili mwingine.  

Kwa upande wake  Mark Njera Ambaye ni  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara amesema kuwa "Msimu huu ni wa ukeketaji,  Koo tisa Kati ya Koo 12 zinakeketa.  Kwa kutambua jambo hilo kipindi hiki cha siku 16 za kupinga ukatili wa Kijinsia elimu imetolewa na Maofisa wa Polisi Dawati la Jinsia na Watoto wapatao 150 kutoka Mikoa yote ya Tanzania ambapo walianza kitoa elimu hiyo kuanzia Dicemba 3, 2024,  hadi Decemba 9, 2024."amesema na kuongeza kuwa.

"Elimu imetolewa kwa wanafunzi wa shule za  Msingi   wapatao 13,000, wanafunzi wa  shule za Sekondari 11,000, kata 48, minada, makanisa na  vikundi. Na katika kipindi hicho Wasichana 113, wameokolewa katika hatari ya kukeketwa, tunaomba serikali iweze kutunga sheria ya kushughulikia ukeketaji."amesema Kamanda Njera.  

Naye Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijiji Mwita Waitara amesema ili kumaliza tatizo la ukeketaji ni vyema elimu inayotolewa iwe shirikishi kutokana na jambo hilo kuwa ni la kimila na pia mfumo dume bado upo. Huku akikiri ukatili kwa sasa umepungua kwani awali matukio mengi ya ukatili yalishamiri sana na wakati mwingine yalifanywa  hadharani.  

 Apolinary Lyambiko  ni Meneja Mkuu wa Mgodi wa Barick North Mara amesema kuwa Mgodi huo umeendelea kushirikiana na Serikali na Wadau mbalimbali katika kupambana na ukatili wa Kijinsia ikiwemo kutoa elimu kwa Jamii na kuweka kipaumbele katika masuala ya Jinsia ili kuimarisha usawa wa Kijinsia katika Jamii.





Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...