Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Wizara ya Viwanda na Biashara Yaahidi Kuendelea Kukuza Ubunifu na Ujasiriamali Kwa Vijana


Na MATUKIO DAIMA APP MOROGORO 

Serikali kupitia Wizara ya Viwanda na Biashara imeahidi kuendelea kuweka mazingira rafiki yatakayowawezesha vijana nchini kukuza vipaji vyao vya ubunifu pamoja na shughuli za ujasiriamali, hatua inayolenga kuongeza ajira, kuimarisha uchumi wa mtu mmoja mmoja na kuchochea maendeleo ya taifa kwa ujumla.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Aristides Mbwasi, amesema hayo wakati alipomwakilisha Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Judith Kapinga, katika hafla ya kufunga maadhimisho ya Siku ya Mzumbe sambamba na Kambi ya Ujasiriamali iliyofanyika katika Chuo Kikuu Mzumbe.

 Mbwasi amesema Serikali inatambua mchango mkubwa unaotolewa na vijana katika kukuza uchumi kupitia bunifu mbalimbali wanazoziibua kila siku, hivyo itaendelea kushirikiana kwa karibu na taasisi za elimu ya juu pamoja na wadau wengine wa maendeleo ili kuhakikisha ubunifu huo unakuwa na tija kwa jamii na taifa.

Amesema kuwa katika kipindi hiki ambacho dunia imejaa ushindani mkubwa wa kiuchumi na kiteknolojia, vijana wanapaswa kupewa nafasi pana zaidi ya kuonyesha uwezo wao kwa kuanzisha biashara, viwanda vidogo na miradi ya ubunifu itakayoweza kuzalisha ajira na kuongeza kipato.

“Serikali inaendelea kuweka mikakati madhubuti ya kukuza uchumi wa viwanda na biashara nchini. Hivyo, tunatambua kuwa vijana wabunifu ni nguzo muhimu katika safari hii ya maendeleo. Ndiyo maana tunaendelea kushirikiana na vyuo vikuu pamoja na taasisi mbalimbali ili kuhakikisha vijana wanapata elimu, maarifa na fursa zitakazowasaidia kufikia ndoto zao,” amesema Mbwasi.

Aidha, amezitaka taasisi zilizo chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara, ikiwemo Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) pamoja na Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO), kuendelea kuwa karibu zaidi na vijana wabunifu na wajasiriamali chipukizi ili kuwasaidia kurasimisha biashara zao, kupata elimu ya biashara na kuendeleza bunifu zao.

Mbwasi amesema ushirikiano huo utasaidia kuongeza thamani ya bunifu zinazobuniwa na vijana, kuwajengea uwezo wa kushindana katika masoko ya ndani na nje ya nchi, pamoja na kuongeza mchango wao katika pato la taifa.

“Tunataka kuona vijana wengi zaidi wakitoka kwenye mawazo ya ubunifu na kuyageuza kuwa biashara rasmi zinazoweza kuajiri watu wengine na kuongeza mapato ya Serikali kupitia shughuli za uzalishaji na biashara,” ameongeza.

Katika hatua nyingine, amewapongeza viongozi wa Chuo Kikuu Mzumbe kwa kuendelea kuandaa programu na majukwaa yanayowapa wanafunzi na vijana nafasi ya kujifunza kuhusu ujasiriamali, ubunifu na matumizi ya teknolojia katika kujikwamua kiuchumi.

Akizungumza kwa niaba ya Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Willam Mwegoha, Meneja wa Kitengo cha Ubunifu, Ujasiriamali na Mahusiano ya Kitasnia chuo kikuu Mzumbe Prof. Allen Mushi amesema chuo hicho kimeendelea kuweka mazingira yanayowasaidia wanafunzi kubadili maarifa wanayopata darasani kuwa miradi halisi ya biashara na ubunifu yenye manufaa kwa jamii.

Profesa Mushi amesema kupitia Kitengo cha Ubunifu, Ujasiriamali na Mahusiano ya Kitasnia, chuo hicho kimefanikiwa kuibua na kusaidia kuanzishwa kwa zaidi ya makampuni 100 yanayofanya shughuli zake katika maeneo mbalimbali nchini.

Amesema mafanikio hayo yamekuwa na mchango mkubwa katika kupunguza changamoto ya ajira kwa vijana, kwani baadhi ya wahitimu wamefanikiwa kujiajiri wenyewe huku wengine wakitoa ajira kwa Watanzania wenzao kupitia biashara na kampuni walizoanzisha.

“Tunajivunia kuona vijana wetu wakitumia elimu wanayoipata chuoni kuanzisha miradi yenye tija kwa jamii. Hii ni ishara kuwa elimu ya juu inaweza kuwa nyenzo muhimu katika kuchochea maendeleo ya uchumi na kuibua kizazi cha vijana wabunifu na wenye uwezo wa kujitegemea,” amesema Profesa Mushi.

Amesema Mzumbe imeendelea kushirikiana na sekta binafsi, taasisi za fedha na wadau wa maendeleo ili kuwajengea vijana uwezo wa kubuni biashara endelevu zinazoweza kukua na kushindana katika soko.

Ameeleza kuwa kupitia kambi mbalimbali za ujasiriamali zinazoandaliwa na chuo hicho, vijana wamekuwa wakipata mafunzo ya vitendo kuhusu usimamizi wa biashara, matumizi ya teknolojia, ubunifu wa bidhaa pamoja na mbinu za kutafuta masoko.

Maadhimisho ya Siku ya Mzumbe na Kambi ya Ujasiriamali yamewakutanisha wanafunzi, wadau wa elimu, taasisi za Serikali, sekta binafsi pamoja na wabunifu mbalimbali kwa lengo la kujadili namna bora ya kutumia ubunifu na ujasiriamali kama nyenzo ya maendeleo ya kiuchumi nchini.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...