Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Waziri Mkuu Aweka Jiwe la Msingi Ujenzi wa Hosteli Nelson Mandela


*Asifu maono ya Rais Dkt. Samia kuhimiza sayansi, atoa maagizo sita

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba ametoa wito kwa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Kampasi ya Tengeru ihakikishe inakuwa kitovu cha ubora wa kitaaluma na utafiti bunifu unaolenga kutatua changamoto halisi za dunia ya leo.

Ametoa wito huo leo (Jumapili, Februari 22, 2026) wakati akizungumza na viongozi wa mkoa wa Arusha, wanachuo na wakazi wanaoishi jirani na taasisi hiyo waliofika kushuhudia uwekaji wa jiwe la msingi katika hafla iliyofanyika kwenye Kampasi ya Tengeru, wilayani Arumeru, mkoani Arusha. 



“Tumeona tumeona chanjo ya samaki, tumeona mbolea inayozalishwa kwa kutumia mwani. Tumeona ndege nyuki ya kupanda mazao shambani, hii itaokoa muda wa unaotumika kupanda mazao. Hizi bunifu zote zinaundwa ili kurahisisha kazi kwani zinatatua mambo mengi kwenye shughuli za kila siku za maisha yetu,” amesema.

Aidha, ameitaka taasisi hiyo ihakikishe mafunzo yatakayotolewa, yanazingatia zaidi ujuzi wa vitendo, ubunifu na ujasiriamali ili wahitimu waweze kujiajiri, kuajiri wengine na kuwa sehemu ya suluhu ya changamoto ya ajira, badala ya kusubiri ajira serikalini pekee.



Ameutaka uongozi wa taasisi hiyo, kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, uhakikishe matumizi ya TEHAMA, mifumo ya kisasa ya kufundishia na kujifunzia, pamoja na usimamizi madhubuti wa rasilimali ili Kampasi hiyo iwe endelevu na shindani kimataifa.

Amewataka kwa wananchi wa Mkoa wa Arusha na mikoa jirani wakilinde na kukimiliki chuo kama rasilimali yao ya maendeleo kwa kushirikiana na Chuo katika kutoa huduma, mazingira rafiki na ushiriki wa kijamii.

Akisisitiza ukamilishaji wa hosteli hiyo, Waziri Mkuu amesema: “Kutokana na umuhimu wa hosteli hakikisheni hosteli hii inakamilika kwa wakati, kwa ubora unaokusudiwa, na inaanza kutoa huduma ili matunda ya uwekezaji huu yaanze kuonekana mapema kwa wananchi na Taifa kwa ujumla.”

Amesema ujenzi wa hosteli hiyo unaakisi dhamira ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuendeleza elimu ya juu na kuongeza nafasi za masomo katika nyanja ya sayansi kama nyenzo kuu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Kuhusu upatikanaji wa mikopo ya elimu ya juu, Waziri Mkuu amesema Serikali imeendelea kuimarisha Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu kwa kuongeza bajeti yake kutoka sh. bilioni 464 mwaka 2020/2021 hadi sh. bilioni 916.7 mwaka 2025/2026, hatua ambayo amesema imewezesha vijana wengi zaidi kutoka familia za kipato cha chini kupata fursa ya kujiendeleza kielimu.

“Hatua hiyo imewezesha idadi ya wanufaika kuongezeka kutoka 177,925 mwaka 2021/2022 hadi 252,773 mwaka 2025/2026 sawa na ongezeko la asilimia 42.1. Sambamba na hilo, Serikali imeboresha mifumo ya utoaji mikopo kwa kuzingatia vipaumbele vya Taifa katika sayansi, teknolojia, uhandisi, tiba na sasa kilimo cha kisasa.”

Akimkaribisha kuzungumza na hadhira hiyo, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda alisema chuo hicho ni cha kipekee kwa sababu kinahusika na utoaji wa masomo ya sayansi na teknolojia tu na pia kinatoa shahada za Uzamili na Uzamivu tu.

“Chuo hicho kinakidhi maelekezo ya Mheshimiwa Rais ya kutoa ufadhili kamili kwa wanafunzi wanaofanya vizuri sana. Hawa Serikali inawalipia gharama zote kwa asilimia 100. Mheshimiwa Rais pia alielekeza tuwapeleke kusoma nje ya nchi vijana waliofanya vizuri sana.”

“Tulianza na vijana 50. Kati yao, vijana 16 walikuja hapa Nelson Mandela kupata mafunzo maalum na sasa wako Afrika Kusini. Hawa vijana 34 waliokuja awamu ya pili, wanapatiwa mafunzo na wao ikifika Septemba wataenda Ireland kuanza masomo yao,” alisema wakati akielezea mpango huo.

Mapema, Mwenyekiti wa Baraza la Chuo hicho, Balozi Maimuna Tarishi alisema ujenzi wa mabweni ya wanafunzi katika Kampasi ya Tengeru, unalenga kuongeza uwezo wa malazi wa wanafunzi kutoka 600 mwaka 2021 hadi 1,000 mwaka 2026. 

“Mradi unajumuisha jengo lenye ghorofa tatu katika mabawa matano ambalo lilikamilika litakuwa na vyumba 184. Kati ya hivyo, vyumba 160 ni self-contained, vyumba 20 ni  maalum kwa wanafunzi wa kike wenye watoto au mahitaji maalum na vinne vitakuwa kwa ajili ya matumizi mtambuka (common rooms).

Alisema mabawa matatu yako kwenye hatua ya umaliziaji na mawili yako kwenye hatua ya upauaji. “Ili kukamilisha ujenzi huu, zinahitajika sh. bilioni 1.88. Makadirio ya fedha hizo yako kwenye bajeti ya mwaka 2026/2027 na kama fedha yote itapatikana, tunatarajia ifikapo Desemba, 2026 majengo yote yatakuwa yamekamilika,” alisema.


Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...