Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

JKCI, HTAF waanzisha shindano la insha shuleni kuhusu magonjwa ya moyo


Na Mwandishi Wetu

TAASISI ya Moyo ya Jakata Kikwete (JKCI), kwa kushirikiana na Heart Team Africa (HTAF) wameanzisha shindano la insha shuleni ikiwa ni mkakati wa kuhakikisha watanzania wanatambua hatari ya magonjwa ya moyo tangu wakiwa wadogo.

Shindano hilo lilizinduliwa Leo  na Kamishna wa Elimu, Wizara ya Elimu, Dk Lyabwene Mtahabwa kwenye ofisi za HTAF jijini Dar es Salaam ambapo pia alikuwepo Mkurugenzi Mtendaji wa (JKCI), Dk Peter Kisenge na mratibu wa shindano hilo, Mwalimu Matuha Massati.

Akizungumza kwenye mkutano huo, Dk Kisenge alisema kwenye shindano hilo, mshindi wa kwanza ataaondoka na 3,000,000 na kompyuta mpakato, mshindi wa pili kompyuta mpakato na 2,000,000, mshindi wa tatu atapata kishikwambi na 1,000,000.

Dk Kisenge alisema mshindi wanne atapata Sh 500,000 na cheti wakati mshindi wa tano atapata shilingi 300,000 na cheti.

Dk Kisenge alisema thamani ya shindano hilo ni kubwa sana hasa ikizingatiwa kuwa gharama za matibabu ya moyo ni kubwa na watu wengi hawana uwezo wa kumudu matibabu.

Alisema shindano hilo litasaidia kuhamasisha watu kutambua umuhimu wa kulinda afya ya moyo kuanzia wadogo hali ambayo itasaidia kupunguza mzigo serikali wa kutibu wagonjwa wa moyo.

Kamishna wa Elimu wa Wizara ya Elimu, Dk Lyabwene Mtahabwa, alisema katika miaka 10 ya utoaji wa huduma za magonjwa ya moyo na mishipa hapa nchini, Taasisi hii imebaini changamoto mbalimbali katika utoaji na ufikiaji wa huduma ya moyo na mishipa.

Alisema ili  kukabiliana na hali hiyo, Taasisi imekuwa ikichukua hatua mbalimbali kwa mfano, kutoa elimu kwa umma kuhusu huduma za matibabu na namna ya kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza kupitia matembezi.

Alisema JKCI ilianzisha miradi mbalimbali iliyolenga kujenga uelewa kwa umma kama Mradi wa “Moyo Wangu, Afya Yangu”.

 “Moyo Wangu, Afya Yangu" ni mradi wa miaka mitatu (miezi 36) unalenga kuongeza uelewa na kukuza kinga ya Magonjwa yasiyo ya kuambukiza (NCDs) - hususani magonjwa ya moyo na mishipa ya damu kwa watoto wenye umri wa kwenda shule.

“Kwa msingi huo, shindano hili linalenga kutoa elimu na kuwafikia wanafunzi wa shule za msingi na sekondari na utatumia mbinu mbalimbali ili kuhakikisha kuwa utoaji wa elimu unakuwa endelevu na wanafunzi wengi wanafikiwa kulingana na mazingira halisi ya shule zetu hapa nchini,” alisema

Alitaja njia zitakazotumika kuwa ni pamoja na vilabu vya afya shuleni, vipeperushi, elimu ya afya shuleni, vijarida, mabango, mashindano ya uandishi wa insha, midahalo, kampeni za afya na usafi wa mazingira nk.

Alisema mbinu hizo zote zitatumika kama majukwaa ya kuelimisha na kuwashirikisha wanafunzi ili kuwajengea uwezo na hatimaye waweze kuelimishana wao kwa wao(mwanafunzi kwa mwanafunzi) kupitia Klabu zao za Afya.

Mkurugenzi Mkuu wa HTAF, Dk Naizihijwa Majani alisema shindano hilo litawashirikisha wanafunzi wa kuanzia Kidato cha kwanza hadi kidato cha sita ambao watapewa zawadi mbalimbali.

Alisema mbali na zawadi hizo pia watajengewa uwezo ili wawe waelimisha rika katika shule zao na shule jirani pia na kwamba litafanyika kuanzia tarehe 08 Oktoba hadi tarehe 01 Novemba, 2025.

Mratibu wa shindano hilo kutoka Wizara ya Elimu, Mwalimu  Matuha Massati, alisema mada itakayochaguliwa ili wanafunzi waandikie insha zao itatangazwa katika mitandao ya kijamii na ya taasisi ya JKCI, Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia na  Ofisi ya Rais TAMISEMI.

Alisema mada zitatangazwa pia kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar na kupitia barua zitakazosambazwa kupitia Ofisi ya Rais TAMISEMI na Maafisa Elimu Mikoa na Halmashauri.

“Washindi wa shindano hili watatangazwa kupitia vyombo vya habari na mawasiliano yatafanyika kupitia mikoa, halmashauri na shule husika,” alisema

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...