Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

 Na Angela Sebastian;Bukoba

SERIKALI ya mkoa wa Kagera imepokea miradi miwili ya kinga dhidi ya virusi vya Ukimwi (VVU) kupitia tohara kwa wanaume na wavulana (VMMC) na uwekezaji kwa wasichana na wanawake (Dreams) ambayo ilikuwa inafadhiliwa na shirika lisilo la kiserikali linaloshughulikia Afya ya jamii katika kuzuia VVU,huduma na matibabu (MDH).

Akipokea miradi hiyo  kwa niaba Serikali,katibu tawala msaidizi utawala na rasilimali watu Bwahi Biseko mjini Bukoba amesema, miradi hiyo aliyoipokea ilikuwa ikidhaminiwa kupitia mpango wa dharula wa Rais wa Marekani wa kukabiliana na Ukimwi (PEPFAR) ambayo kwanza ni mradi wa tohara ambao umefikia  wanaume na wavulana 539,835 katika mkoa wa Kagera.

Amesema takwimu hiyo ni  sawa na asilimi 95 ya waliolengwa tangu mwaka 2016 hadi sasa toka mradi huo ulipoanzishwa kwa lengo la kupambana na maambukizi mapya ya VVU ambapo Serikali imejipanga vyema kuiendeleza.

"Sasa kama tumekwishaingizwa katika huduma za kawaida inamaana tunatakiwa kuzingatia mifumo iliyopo katika kuhakikisha kwamba tunandelea na huduma za tohara ili kuhakikisha huduma zinapatikana na kutolewa kama ilivyokuwa kabla ya mfadhiri kumkabidhi miradi hii kwetu"

 Amesema amefuatilia na kuambiwa kuwa sasa huduma iko chini sana  ukiangalia vituo vilivyokuwa vinajaza watu wakati wa mradi huu kutokana na huduma kuwa bure ambapo takwimu ya mwezi walikuwa wakitoa huduma kwa watu 200 hadi 500 sasa hivi wana takwimu ya moja au mbili.

Amesema hicho ni kiashiria kwao kama viongozi na watekelezaji wa huduma kwenda kuzingatia kwa kupambana na yanayowarudisha nyuma kwa kuhakikisha huduma hiyo inakuwa endelevu na inaendelea kutolewa kwa watu wa mkoa wa Kagera.

Amesema Serikali imeishajipanga kuendeleza miradi hiyo kutoa huduma stahiki kama ilivyokuwa hapo awali bila kukwama hivyo akawashauri wananchi kuondoa wasiwasi na hofu ya kukosa huduma.

Adha amesema kuwa mradi wa wasichana na wanawake kujikwamua kiuchumi na kupunguza athari ya mambukizi ya VVU kwa kuboresha maisha yao wa dreams umefikia wanawake na wasichana wapatao 54,000 wa Manispaa ya Bukoba na Muleba.

Amesema mradi huo umesababisha kupiga hatua kubwa ambapo tangu miaka sita ulipoanzishwa mpaka sasa wameanzisha  miradi mikubwa inayowafanya watumie muda mwingi kijishughulisha kuliko kujiingiza katika vishawishi vinavyoweza kuwaingiza katika maambukizi ya VVU.

Pia amewataka vijana walioko katika mradi wa huo kutengeneza na kuzalisha bidhaa zenye ubora ili kwendana na ushindani wa soko la sasa.

Kwa upande wa MDH kutoka makao makuu Dk.Emmanuel Sima amesema katika mradi huo asilimi 60 ya waliotahiriwa walitafutwa kupitia maeneo mbalimbali na asilimi 40 wakifika kwenye vituo vya kutolea huduma.

Aidha amesema kukabidhiwa kwa miradi hiyo miwili kwa Serikali siyo mwisho wa utoaji huduma za MDH katika mkoa wa Kagera, bali wataendelea kuwepo na  kuunga mkono juhudi za Serikali katika kutoa huduma mbalimbali katika sekta ya afya kama ilivyo kawaida yao.

Leonida Rweyemamu ni mmoja wa wauguzi walioanza na mradi wa Tohara mwaka 2016 ulipoanzishwa ameeleza kuwa wakati mradi unaanza jamii haukupokea huduma hiyo 

kwa usahii kutokana na imani na mira zao kwamba mwenye wajibu wa kutahiriwa  ni lazima awe muislam.

"Tulipowafuata baadhi ya wanaume waliowengi walisema nchi imekuja na mbinu ya kubadilisha watu kuwa waislam hivyo hari hiyo ilisababisha kukosa wateja, naipongeza juhudi za MDH na Serikali walibuni njia mbalimbali za kutoa ujumbe kupitia vyombo vya habari,mikutano ya adhara,kuongea na vijana shule,viongozi wa dini na Serikali kuelimisha jamii"amesema Rweyemamu 

Amesema wanaume walifundishwa kuhusu faida za kutahiriwa ikiwemo kupunguza maambukizi ya VVU kwa asilimia 60,usafi na kusaidia akina mama kuepuka kupata kansa ya kizazi hivyo, siku zilivyokuwa zinaenda ndivyo wateja waliongezeka ambapo kwa mwezi waweza kutahiri wanaume na wavulana kati ya 200 na kuendelea waliofika vituoni na waliiofuatwa katika maeneo kupata huduma.

Adelitus Mulokozi ni mkazi wa Manispaa ya Bukoba mmoja wa wanaume waliopata tohara kwa kipndi cha mradi huo amesema wao tangu wakiwa watoto walielezwa kuwa mwanaume anayetahiriwa ni wa dini ya kislam hari iliyosababisha wanaume wa mkoa huo walio wengi kutopata huduma hiyo kama ilivyo kwa mikoa mingine.

"Nashukuru Serikali na wadau wetu wa MDH kuleta huduma hii ambapo  tulielimishwa mimi, nilipata kujua faida za tohara hivyo nikashawishika na kujitokeza pia vijana wangu wawili nao niliwapeleka kisha kupata huduma hiyo kwanza inasaidia kupunguza maambukizi ya VVU kwa kiwango kikubwa pia inasaidia wake zetu kuepukana na maambukizi ya saratani ya kizazi "ameeleza Mulokozi 

Dilica Deogratias ni binti ambaye amenufaika na mradi wa dream baada ya kupata elimu kupitia kituo kilochotengwa cha Sido Kagera ambapo kwa sasa anaweza kutengeneza sabuni na batiki na kuuza kisha kujiingizia kipato.

"Mradi wa dream umenisaidia kuepuka na utegemezi na ombaomba kwa ndugu,jamaa na marafiki ambapo wengine hawana nia nzuri pia kuepukana na vishawishi vinavyoweza kuniingiza katika mazingira yasiyo mazuri ambayo yanasabisha kujiingiza katika ngono zisizo salama"ameeleza Deogratias

Amesema kwasasa anatumia muda mwingi na wanakikundi wenzake kuzalisha na kutafuta wateja kwa ajili ya bidhaa zao hari inayowasaidia kujiepusha na maambukizi ya VVU.





Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...