Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Kasi ndogo ya utekelezaji wa mradi wa umeme wa Chalinze - Dodoma wamkasirisha Dkt Biteko

📌 Asikitishwa mradi huo aliouzindua Novemba 2024 kuwa nyuma kwa asilimia Saba

📌 Asema Rais Samia alitoa agizo mradi usichezewe kutokana na umuhimu wake katika mikoa mbalimbali ikiwemo ya Magharibi

📌 Asema sababu zilizotolewa na mkandarasi  (TBEA) za kusuasua kwa mradi hazikubaliki

📌 Atoa maagizo kwa Mkandarasi kuwasilisha mpango kazi mpya kwa Katibu Mkuu Wizara ya Nishati  ili kufidia muda uliopotezwa

📌 Aagiza TANESCO kutumia mapato ya ndani kulipa fidia wananchi wanaopisha mradi

Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amekagua mradi wa njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovolti 400 kutoka Chalinze  hadi Zuzu Dodoma na kueleza kutoridhishwa kwake na utekelezaji wa mradi huo ambao  ulipaswa kuwa umefikia asilimia 31 lakini kwa sasa  umefikia asilimia 24 tangu kuzinduliwa kwake Novemba mwaka 2024. 

Hali ya kusuasua kwa mradi imebainika wakati Dkt. Biteko akikagua mradi huo katika Kijiji cha Manchali wilayani Chamwino mkoani Dodoma tarehe 20 Agosti 2025 ambapo Dkt. Biteko amemuagiza mkandarasi kampuni ya TBEA ya China kuhakikisha kuwa anafidia muda wa kazi uliopotezwa wa asilimia Saba ili mradi ukamilike kwa wakati kutokana na umuhimu wake nchini.



Mwezi Novemba, 2024 Serikali ilikubaliana na mkandarasi kuwa mradi huo ufanyike ndani ya miezi 19 tu badala ya miezi 22 kwani wakati mradi unazinduliwa tayari kazi kubwa za awali zilikuwa zimeshafanyika ikiwemo za upembuzi yakinifu na utoaji wa maeneo. 

“ Leo ni miezi saba imepita tangu tuzindue mradi sawa na asilimia 32 ya muda wote tuliokuwa tunahitaji  kutekeleza mradi huu, na tulitegemea mradi kwa sasa ufikie asilimia 31 lakini katika hali ya kushangaza mradi umefikia asilimia 24 tu jambo ambalo halikubaliki.” Amesema Dkt. Biteko


Dkt. Biteko ameeleza kuwa, sababu zilizotolewa na Mkandarasi za kuchelewesha mradi ikiwemo ya wananchi kugoma kutoa maeneo kwa madai ya fidia na kukutana na miamba katika mkuza wa mradi hazikubaliki kwani  wananchi  hao wana haki na  lazima walipwe fidia.

Kutokana na hali hiyo, ameagiza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO)  kutumia mapato yake ya ndani kulipa fidia wananchi waliopisha mradi.

Dkt. Biteko ametanabaisha kuwa mkandarasi alishaagizwa asiutekeleze mradi huo kwa mazoea kutokana na umuhimu wake kwani kwa sasa  miundombinu inayosafirisha umeme kwenda  Dodoma kutoka mradi wa Julius Nyerere (JNHPP) kupitia kituo cha  Chalinze  inabeba umeme kidogo kwa takriban megawati 240 tu ambayo ni sawa na mashine moja tu kati ya mashine 9 za JNHPP hivyo njia hiyo mpya ya umeme ya kV 400 inayojengwa ni muhimu.

Amesisitiza kuwa njia mpya ya umeme ya kV 400 ni muhimu kwani katika Mkoa wa Dodoma mahitaji ya umeme yanaongezka kila siku huku mkoa huo pia ukiwa ni kitovu cha usambazaji umeme katika mikoa yote ya Magharibi ikiwemo Singida, Tabora, Shinyanga Mara na Kigoma ambayo inategemea utulivu wa umeme katika Mkoa wa huo na kwamba  Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan alishaagiza kuwa mradi huo usichezewe hivyo Mkandarasi ahakikishe kuwa anaupa umakini  mkubwa.

Kutokana na mradi huo kuwa nyuma katika utekelezaji,  Dkt. Biteko  amemuagiza Mkandarasi kuja na mpango mpya wa utekelezaji wa kazi ukiwemo wa kufidia muda uliopotezwa ambapo ametoa siku nne mpango wa fidia ya muda uwasilishwe kwa Katibu Mkuu Wizara ya Nishati.

Vilevile, Dkt. Biteko ameagiza mkandarasi kuongeza nguvu kazi ya watu ili minara 917 ya umeme inayopaswa kujengwa kwenye mradi huo ijengwe kwani kwa sasa mkandarasi amechimba takriban  mashimo 100 tu kwa ajili ya usimikaji wa minara. Pia amemtaka Mhandisi mshauri wa mradi kuhakikisha anasimamia mradi huo kwa ufanisi na aeleze ukweli pale anapoona kuwa hauendi sawa.

Aidha amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, kutengeneza timu itakayoungana na TANESCO kuusimamia mradi huo na kila wiki taarifa itolewe kuwa umefikia wapi.

Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko amewaasa Wananchi kutozuia utekelezaji wa miradi pale inapopita kwenye maeneo yao na Serikali kwa upande wake itahakikisha kuwa wanapata haki wanazostahili kwani Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshaelekeza kuwa hataki wananchi wafanyiwe dhuluma ambapo wasaidizi wake wanahakikisha kuwa agizo hilo linatekelezwa.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amesema  mradi huo wa usafirishaji umeme wa kV 400 kunaenda kuifanya Dodoma kuwa kitovu cha usambazaji umeme nchini.


Aidha, ameahidi kuyasimamia maelekezo yote yaliyotolewa na Dkt. Biteko ya kuhakikisha kuwa mradi huo unakamilika kwa wakati ili kuwezesha umeme huo utakaofikishwa Dodoma, kusambazwa pia kwenye maeneo mengine nchini.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Lazaro Twange amesema Mradi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 400 kutoka Chalinze hadi Dodoma unakusudia kusafirisha umeme wote unaozalishwa kutoka katika Bwawa la kuzalisha umeme la Julius Nyerere (Megawati  2,115) na kuingiza kwenye gridi ya Taifa kisha  kuufikisha kwenye maeneo yote yenye mahitaji ya umeme.

Amesema mkataba na mkandarasi kampuni ya TBEA ulisainiwa mwaka 2024 na mradi kuanza kutekelezwa mwezi Novemba 2024 ambapo mkandarasi ameshalipwa awamu ya kwanza ya malipo ambayo ni shilingi za kitanzania bilioni 107 na mhandisi mshauri ameshalipwa asilimia 15 ya malipo yake.

Ameeleza kuwa maagizo yote yaliyotolewa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa  Nishati yatafanyiwa kazi ikiwemo ya kuhakikisha kuwa mradi unakamilika mwezi Juni au kabla ya Juni 2026 kwa mujibu wa mkataba.

Aidha, Ameishukuru Serikali chini ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa shilingi bilioni 513 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo ambao utakuwa na urefu wa kilometa 345 na kuhusisha minara ya umeme ipatayo 917 kutoka Chalinze mkoani Pwani hadi Zuzu mkoani Dodoma.

Mwisho

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...