Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Rweyemamu wa Bukoba Alambwa Kifungo Cha Maisha Kwa Kosa la Kubaka na Kulawiti


 Na Angela Sebastian ;Bukoba

RWEYEMAMU Kashunja (35) bodaboda mkazi wa Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera na mwenzake wamehukumiwa kifungo cha maisha jera na mwingine mmoja akihukumiwa kufungwa miaka 30 kutokana na makosa ya ubakaji na ulawiti.

Amon Mang’era ni wakili wa Serikali ameeleza hayo wakati akiongea na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali ofisini kwakwe mjini Bukoba ambapo alimtaja Rweyemamu maarufu kama baba P ametiwa hatiani na mahakama ya hakimu mkazi Wilaya ya Bukoba,kwa kosa la kumlawiti mtoto wa miaka sita baada ya mahakama hiyo kulidhika na ushahidi wa upande wa Jamhuri pasipo kuacha shaka.

“Kati ya mwezi Aprili na Mei mwaka jana mshitakiwa Rweyemamu alimlawiti mtoto wa miaka mitano kwa wakati huo ambapo kwa sasa ana umri wa miaka sita na wakati shauri likiendelea mtuhumiwa na mdhamini wa kwanza ambaye ni mke wake walitoroka ambapo kesi iliendelea ambapo Mei 30 mwaka huu mahakama ilitoa hukumu na kumtia hatiani kwa kufungwa jera maisha kutokana na kifungu cha 154(1) (a) na (2) cha kanuni ya adhabu sura ya 16 marejeo 2022” ameeleza

Amesema mshitakiwa Rweyemamu na mke wake Anchira Gozibart ambaye ni mdhamini wa kwanza wanatafutwa na mahakama ili wakatumikie adhabu zinazowakabili huku mdhamini wa pili aitwaye Nelson Mutagaywa akiendelea kutumikia kifungo cha nje cha miezi sita.

Amesema katika shauri hilo pia lilihusisha watoto wawili ambao walitenda kosa la ulawiti kwa mtoto huyo mwezi Desemba mwaka jana ambapo walikiri kosa na mahakama kutoa adhabu kulingana na sheria ya mtoto sura ya 13 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2019 ambapo wamepelekwa ustawi wa jamii ili kupewa ushauri nasaha na uangalizi.

Pia mahakama hiyo imemhukumu Abdul Selemani (30) mfanyabiashara wa samaki mkazi wa Bukoba kwenda jera maisha baada ya kumbaka mtoto wa miaka saba.

Mang’era amesema hukumu hiyo ilitolewa Mei 28 mwaka huu mshitakiwa ametiwa hatiani baada ya mahakama kujiridhisha pasipo na shaka kutokana na ushahidi uliotolewa na upande wa Jamhuri kwamba Abdul alimbaka mtoto huyo kwa mara tatu mfululizo hivyo kutokana na kanuni ya adhabu kifungu cha sheria namba 131 (3)sura ya 16 marejeo ya 2022 na cha kosa 130 (1) na (2)e ambavyo ameshitakiwa navyo.

“Kati ya mwezi Aprili na Mei mwaka jana mshitakiwa Abdul alimchukua mtoto huyo wa miaka saba wakati akitoka shule na kumuingiza ndani ya jumba chakavu ambalo haishi mtu na kumbaka mara tatu kwa nyakati tofauti ambacho ni kitendo cha kinyama ambapo dada wa kazi aligundua tatizo hilo na kisha kumjulisha mama wa mtoto ndipo hatua zikachukuliwa” ameeleza Mang’era

Katika tukio jingine mshitakiwa katika mahakama ya Wilaya Bukoba imemhukumu kwenda jera miaka 30 Valentine Buberwa (41)mkazi wa Manispaa ya Bukoba maarufu kama baba mzazi kwa kosa la kumbaka mtoto wa jirani yake mwenye umri wa miaka mitatu.

Wakili Mang’era amesema tukio hilo lilitokea Oktoba 25 mwaka jana ambapo mshitakiwa aliwakuta watoto watatu wakicheza na kumchukua mmoja ambaye ni mhanga na kumuingiza ndani ya nyumba yake alimokuwa akiishi mwenyewe na kuanza kumbaka ambapo wale ndugu wa mhanga waliamua kufuatilia na kumkuta Valentine akiendelea kumbaka ndipo walipiga kelele zilizosababisha mshitakiwa kukamatwa.

“Kutokana na ushahidi uliotolewa na Jamhuri mahakama imelidhika pasipo shaka na mwezi Mei 30 mwaka huu ilitoa hukumu na kumtia hatiani mshitakiwa Valentine kufungwa miaka 30 jera kutokana na kifungu cha sheria namba 131 (3) sura ya 16 marejeo ya 2022”

Mang’era alisema kesi zote zilisikilizwa mbele ya hakimu mkazi mwandamizi wa mahakama ya Wilaya ya Bukoba Flora Kaijage na kijiridhisha na ushahidi uliotolewa na mashahidi upande wa Jamhuri pasipo shaka na kisha kutoa hukumu hizo wka washitakiwa zilizowatia hatiani.








Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...