Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Wafahamu wabunge Watano wa Kenya waliouawa mitaani Tangu Mwaka 2008


Katika historia ya taifa la Kenya, vifo vya viongozi mashuhuri wa kisiasa vinavyotokea kwa njia ya kutatanisha vimeacha makovu ya kudumu kwenye dhamira ya wananchi.

Mauaji haya mara nyingi hutokea nyakati za misukosuko ya kisiasa, yakihusisha siasa za kiimla, uhasama wa uongozi, na migawanyiko ya kitaifa.

Matukio haya ya kikatili yaliwafanya wananchi kutokuwa na imani na serikali zilizokuwa madarakani, huku yakiibua majonzi, hasira, na hofu iliyoenea miongoni mwa wananchi.

Kila tukio la mauaji halikubaki kama tukio la kipekee bali liliibua athari za kina kuimarisha migawanyiko ya kisiasa, mianya ya usalama na wito wa uwajibikaji hasa katika idara za kijasusi.

Wabunge waliopigwa risasi na kuuawa katika mazingira tatanishi baadhi walihusishwa na maono ya mabadiliko au msimamo wa wazi dhidi ya mifumo ya utawala, huku wengine wakionekana kuangukia mikononi mwa wahalifu.

Katika taarifa hii tuwaangazia wabunge saba ambao walifariki ghafla baada ya kumiminiwa risasi wakiwa katika shughuli zao za kawaida mitaani.


1. Charles Ogondo - Mbunge wa Kabondo Kasipul


Kisa cha hivi punde ni cha mauaji ya Mbunge wa eneo bunge la Kabondo Kasipul katika jimbo la Homa Bay Charles Ong'ondo.

Mbunge huyu alikuwa ametoka bungeni muda mchache tu kabla ya kushambuliwa akiwa ndani ya gari lake kwenye barabara iiliyo na shughuli nyingi mjini Nairobi.

Polisi wamesema gari la Mbunge Charles Ong'ondo liliandamwa na watu wawili waliokuwa wakiendesha pikipiki kisha mmoja wao akasimama na kumfyatulia risasi kadhaa.

Dereva wake alinusurika shambulio hilo.

Marehemu ni mbunge wa chama cha Orange Democratic Movement(ODM) kinachoongozwa na mwanasiasa mkongwe Raila Odinga.

Polisi wangali wanachunguza kisa hicho huku waliotenda uhalifu huo wakiwa bado hawajakamatwa na chanzo ya mauaji hayo hakijabainika mara moja.

Dereva wa gari na abiria wa kiume, ambao hawakujeruhiwa walifanikiwa kumkimbiza mbunge huyo katika Hospitali ya Nairobi, ambapo alithibitishwa kuwa amefariki wakati anawasilishwa.

Katika taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Polisi Muchiri Nyaga, alithibitisha kwamba Mbunge huyo aliuawa kwa kupigwa risasi Jumatano jioni kando ya Barabara ya Ngong karibu na mzunguko wa chumba cha kuhifadhi maiti cha City na mtu aliyekuwa na bunduki.

"Kuna uwezekano marehemu alilengwa na mauaji yake yalipangwa," Msemaji wa Polisi aliongezea.

Muchiri alisema makamanda wakuu wa polisi na wapelelezi walitembelea eneo hilo kuchunguza kilichotokea.

Huduma ya Polisi ililaani kitendo hicho cha ufyatuaji risasi na kukitaja kama "uhalifu mbaya na usio na maana" na kuhakikishia umma kwamba hakuna kitakachozuia uchunguzi.


2. George Muchai - Mbunge wa Kabete. 

Tarehe 7 mwezi Februari mwaka 2015, Mbunge George Muchai eneo bunge la Kabete alipigwa risasi na kuuawa pamoja na walinzi wake wawili na dereva wao katikati ya jiji la Nairobi.

Sanduku na bunduki mbili za walinzi ziliibiwa katika tukio hilo.

Muchai ambaye alikuwa mbunge wa chama cha Jubilee alikuwa amehudumu kwa miaka miwili tangu achaguliwe kwa mara ya kwanza.

Wakati huo, alikuwa akirudi baada ya chakula chajio na familia yake.

Familia yake ilikuwa mbele yao katika gari jingine ambapo binti yake alieleza walikuwa wametoka eneo la Westlands.

Mbunge huyo alikuwa amenusurika jaribio lingine la mauaji mnamo mwaka 2011, jambo lililoonyesha wazi kulikuwa na njama ya kumuangamiza.


3.Mugabe Were - Mbunge wa Embakasi

Melitus Mugabe Were, mbunge wa Embakasi kupitia chama cha kisiasa cha ODM, aliuawa mwezi Januari 29, 2008 katikati ya ghasia za baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007.

Alipigwa risasi nje ya makazi yake katika mtaa wa Woodley, Nairobi.

Mauaji ya Mugabe Were yalishtua taifa lote na kuwa mfano wa hatari ya siasa za chuki.

Baada ya kesi iliyodumu miaka saba, mahakama iliwahukumu James Omondi (Castro), Wycliffe Simiyu (Zimbo), na Paul Omondi (Papa) kunyongwa kwa kosa hilo la mauaji.


5. David Kimutai Too - Mbunge wa Ainamoi

Aliyekuwa mbunge wa Ainamoi, David Too, aliuawa kwa kupigwa risasi Januari 2008 huko Eldoret, eneo la West Indies, Kaunti ya Uasin Gishu.

David Too alikuwa mwanachama wa chama cha ODM, aliuawa siku chache tu baada ya mwenzake wa Embakasi Melitus Were kupigwa risasi na kuuawa nje ya nyumba yake jijini Nairobi.

Too aliuawa pamoja na afisa wa polisi wa trafiki wa kike, na hivyo kuchochea madai kwamba kifo chake kinaweza kuwa ni masuala ya wivu wa mapenzi.

Kifo cha Too kilizua hali ya wasiwasi kote nchini huku wafuasi wa upinzani wakidai njama fiche kutokana na mauaji hayo mawili yenye utata yaliyotokea wiki moja.

Mshukiwa mkuu wa mauaji hayo Andrew Moeche Omwenga, afisa wa polisi, alidai alijitetea baada ya kushambuliwa na Kimutai pamoja na afisa mwenzake Eunice Chepkwony.

Moeche alihusishwa kimapenzi na Chepkwony, ambaye alikuwa mjane wa askari mwingine.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...