Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Serikali yavuna sh Bilioni 726,219 sekta ya madini

 


• *Ni kuanzia Julai 2024, hadi Aprili 2025*

• *Vibali 9,540 vya usafirishaji madini nje ya nchi vyatolewa*

• *Matumizi ya Baruti yaongezeka*

WIZARA ya Madini kupitia Tume ya Madini imefanikiwa kukusanya jumla ya Shilingi 726,219,317,398.14 ambapo Shilingi 612,593,046,886.50 ni malipo ya mrabaha na Shilingi 113,626,270,511.64 ni malipo ya ada ya Ukaguzi.

Akizungumza Bungeni leo Mei 2, 2025 Waziri wa Madini Mheshimiwa Anthony Mavunde (MB) wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2025/2026 amesema makusanyo hayo ni katika kipindi cha Julai 2024 hadi Machi 2025 ambapo madini yenye thamani ya Shilingi 11,376,270,882,758.50 yalizalishwa na kuiwezesha serikali kupata kiasi hicho cha fedha.

*USIMAMIZI, UKAGUZI NA BIASHARA YA MADINI*:

Waziri Mhe. Mavunde amesema katika kipindi cha Julai 2024 hadi Machi 2025, vituo vipya saba vya ununuzi wa madini vilianzishwa ambavyo ni Nhungwiza - Geita, Nachingwea, Liwale, Likofia - Lindi, Mugumu, Serengeti – Mara na Ikinabusu - Simiyu. 

Mheshimiwa Mavunde amesema ongezeko hilo linafanya idadi ya vituo vya ununuzi wa madini kufikia 109. 

Aidha, amesema katika kipindi husika, Wizara imeyatambua na kuzipa hadhi vituo vya ununuzi jumla ya maeneo 142 yanayotumika kufanyia biashara ya madini kwa wingi (bulk minerals) kupitia Gazeti la Serikali Na. 906 ya 15 Novemba 15, 2024.


Amesema, Tume ya Madini kwa kushirikiana na Mamlaka mbalimbali za Serikali ziliendelea kusimamia uendeshaji wa masoko na vituo vya ununuzi wa madini, kupitia usimamizi huo, kwa kipindi cha Julai 2024 hadi Machi 2025 mauzo ya shilingi 2,819,220,651,824.38 yalifanyika katika masoko ikilinganishwa na mauzo shilingi 1,930,698,791,589.30 yaliyofanyika katika kipindi cha Julai 2023 hadi Machi 2024. 

“Kutokana na mauzo hayo, Serikali imekusanya kiasi cha shilingi 182,043,495,150.21 ikiwa ni tozo ya mrabaha na ada ya ukaguzi ikilinganishwa na Shilingi 136,731,358,413.41 zilizokusanywa katika kipindi kama hicho cha mwaka 2023/2024,”amesema Mhe. Mavunde.

*UTAMBUZI NA UTHAMINISHAJI WA MADINI*

Mheshimiwa Waziri Mavunde amesema kuwa Tume ya Madini imeendelea kusimamia shughuli za uchambuzi na uthaminishaji wa madini yote yaliyozalishwa na kutoa vyeti vya uthaminishaji wa madini pamoja na vibali vya usafirishaji na uingizaji madini. 

Amesema, katika kipindi cha kuanzia Julai 2024 hadi Machi 2025, jumla ya vibali 9,540 vya usafirishaji madini nje ya nchi vilitolewa ikilinganishwa na vibali 8,809 vilivyotolewa katika kipindi kama hicho mwaka 2023/2024 huku thamani ya madini kwa vibali hivyo ni Shilingi 9,252,791,412,068.11.

Aidha, jumla ya vibali 116 vya uingizaji madini nchini vilitolewa ambapo madini yenye thamani ya dola za Marekani 14,813,664.38 yaliruhusiwa kuingia nchini. 

*UKAGUZI WA HESABU ZA FEDHA NA KODI*

Waziri Mavunde amesema katika kipindi cha Julai 2024 hadi Machi 2025, Tume ya Madini imefanya ukaguzi kwa kampuni 21 za uchimbaji, miradi ya barabara na biashara ya madini. 

Amesema, kati ya kampuni hizo, sita ni za uchimbaji madini ya dhahabu, 11 miradi ya barabara ambayo inatumia madini ujenzi, moja ni ya uchimbaji madini ujenzi, moja ni ya uchimbaji wa madini ya Almasi, moja ni ya umwagiliaji ambayo inatumia madini ujenzi na moja ni kiwanda cha kusafisha dhahabu. 


Mhe. Mavunde amesema kaguzi hizo zimewezesha kuibua hoja mbalimbali zinazohusiana na kutolipwa kwa malipo ya Serikali shilingi 1,255,950,666.52. Kati ya fedha hizo, shilingi 576,917,781.17 zimelipwa baada ya ukaguzi. Kampuni tano zinazodaiwa shilingi 676,032,885.35 zimeahidi kuendelea kulipa deni kwa awamu.

“ Sambamba na hilo, Tume ya Madini imeendelea kufanya jitihada mbalimbali za kuhakikisha deni lote linalipwa kupitia vikao vya maridhiano na pale inapobidi kuchukua hatua kwa mujibu wa Sheria ya Madini Sura 123,”amesema.

*SHUGHULI ZA UKAGUZI WA MIGODI, MAZINGIRA NA USIMAMIZI WA BARUTI*

Aidha, amesema shughuli za Ukagauzi wa Migodi, Mazingira na Usimamizi wa Baruti, katika kipindi cha Julai 2024 hadi Machi 2025, migodi mikubwa saba ilikaguliwa, Migodi hiyo ni Dangote Cement Co. Ltd, Williamson Diamond Ltd, El-Hillal Minerals, North Mara Gold Mine, Geita Gold Mine, STAMIGOLD na Bulyanhulu Gold Mine.

“Kufuatia ukaguzi huo mapungufu mbalimbali yalibainika ikiwemo kutokuwepo kwa Mipango ya Ufungaji Mgodi (Mine Closure Plans), Mipango ya uchimbaji Madini (Mine Plans), kutokuwepo kwa maeneo maalum yaliyotengwa kwa ajili ya kuhifadhia miambataka (waste rock dumps), uwepo wa visima vya ufuatiliaji wa ubora wa maji (monitoring boreholes) vilivyoharibiwa kutokana na uvamizi pamoja na upanuaji wa mabwawa la topetaka. Migodi ilielekezwa kurekebisha mapungufu hayo na tayari wamerekebisha.,”amesema.



Amesema, ukaguzi katika Migodi ya Wachimbaji wa kati katika kipindi cha Julai 2024 hadi Machi 2025, jumla ya migodi 53 ya uchimbaji wa kati ilikaguliwa katika sehemu mbalimbali nchini. 

Amesema, kaguzi hizo mapungufu mbalimbali yalibainika ikiwemo kukosekana kwa taarifa za usanifu wa maeneo ya kuhifadhi miambataka pamoja na mabwawa ya topetaka. 

Waziri Mavunde amesema wahusika walielekezwa kurekebisha mapungufu yaliyojitokeza kwa kuzingatia Sheria ya Madini, Sura 123 na Sheria ya Usimamizi wa Mazingira, Sura 191 ambapo migodi husika imerekebisha mapungufu yaliyobainika.

Kwa upande wa ukaguzi katika Migodi ya Wachimbaji Wadogo, Waziri Mavunde amesema 

katika kipindi cha Julai 2024 hadi Machi 2025, ukaguzi ulifanyika kwenye migodi ya wachimbaji wadogo 14,847 katika mikoa 30 ya kimadini nchini. 

Amesema katika kaguzi hizo baadhi ya mapungufu yaliyobainika ni pamoja na kutofukiwa kwa mashimo ya uchimbaji yasiyotumika (abandoned pits), kutotumika kwa vifaa kinga, matumizi hafifu ya vifaa kinga na uhifadhi usio salama wa baruti na kukosekana kwa Mipango ya utunzaji wa mazingira (Environmental Protection Plan - EPP). 

Amesema, wahusika walielekezwa kufanyia kazi mapungufu yaliyobainika ili kuwa na uchimbaji salama, endelevu na wenye tija.

*UKAGUZI WA MAGHALA, STOO NA MASANDUKU YA KUHIFADHIA BARUTI*


Mheshimwa Mavunde amesema, kuhusu ukaguzi wa Maghala, Stoo na Masanduku ya Kuhifadhia Baruti katika kipindi cha Julai 2024 hadi Machi 2025, jumla ya maghala 164, Stoo 268 na masanduku 207 yalikaguliwa katika mikoa yote ya kimadini. 

Amesema, kaguzi hizo zilibaini uwepo wa mpangilio hatarishi wa vilipuzi, ukosefu wa leseni za uendeshaji wa maghala na kutokulipwa kwa ada za mwaka za leseni za maghala. Aidha, wahusika walirekebisha mapungufu hayo kama walivyoelekezwa.

*MAHITAJI YA BARUTI YAONGEZEKA*:


Waziri Mavunde amesema mahitaji na matumizi ya baruti kwa sasa yameongezeka kutokana na kuimarika kwa shughuli za uchimbaji wa madini na ujenzi wa miundombinu mbalimbali. 

“Katika kipindi cha Julai 2024 hadi Machi 2025, vibali 267 vya kuingiza, kupitisha, kutengeneza na kuuza baruti nchini pamoja na vibali vya kusafirisha baruti nje ya nchi vimetolewa. Fedha zilizopatikana kupitia utolewaji wa vibali hivyo ni jumla ya dola za Marekani 133,438.,”amesema.

Aidha, amesema Tume ya Madini ilifanya ukaguzi kwenye maeneo yaliyoombewa kujengwa maghala ya kuhifadhi baruti ambapo maeneo yaliyofanyiwa ukaguzi ni Indo African Explosives Limited (Dar es salaam); Lindi Jumbo Limited (Lindi); AECI Mining Tanzania Ltd kwa mgodi wa Shanta Singida Gold Mine, Williamson Diamond Limited Shinyanga, Shanta New Luika Gold Mine Songwe; Ruvuma Coal Limited (Ruvuma); na East Africa Harmony Mining Co. Ltd (Tanga). 

Amesema, ukaguzi huo ulibaini kuwa maeneo hayo yalikidhi matakwa ya Sheria ya Baruti, Sura 45 na hivyo kupewa vibali vya ujenzi wa maghala ya kuhifadhi baruti.

Pia, amesema Tume ya Madini imetoa vibali kwa ujenzi wa maghala ya kuhifadhia baruti ambapo maghala nane ni mapya ya kuhifadhi baruti yamejengwa na kampuni za Heshem Tanzania Co. Ltd (Chunya), China Civil Engineering Construction Corporation (Nzega), Ideal Detonators Tanzania Limited (Pwani), Canuck Company Limited (Kahama), Sekenke One Mining Cooperative Society Limited (Singida), Esap Mining Services Limited (Songwe) na Tianpin (T) Investment Management Limited (Kahama). Aidha, maghala hayo yatasaidia katika utoaji wa huduma za uchimbaji katika maeneo husika.

………………………..

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...