Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mnufaika uhitimu masomo,lipa mkopo wako kwa wakati

 


Na Dk. Reubeni Lumbagala 






SERIKALI kupitia Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inawajibika kupokea maombi ya mikopo na kutoa mikopo kwa waombaji waliokidhi vigezo vilivyowekwa. Bodi ya Mikopo ambayo sasa imetimiza miaka 20 tangu kuanzishwa kwake mwaka 2004, hadi Februari 2025, HESLB inajivunia kutoa takribani shilingi trilioni 8.2 kwa waombaji mbalimbali zaidi ya 830,000 ambao sasa si waombaji tena bali ni wanufaika wa mikopo hiyo. 


Kiukweli, fedha hizi ni nyingi sana ambazo zimetolewa na serikali kwa nia njema ya kuwasaidia wanafunzi ambao kutokana na hali za kiuchumi wao na familia zao hawawezi kugharamia gharama za elimu ya juu, hivyo kuhitaji kuwezeshwa raslimalifedha ili kumudu kulipa ada, malazi, kununua chakula, vitabu, kuhudhuria mafunzo kwa vitendo na masuala mengineyo.


Ni muhimu kwa wanufaika wa mikopo ya elimu ya juu kufahamu kuwa mikopo waliyokopeshwa na serikali kupitia Bodi ya Mikopo inapaswa kurejeshwa pindi wanapohitimu masomo yao hasa baada ya kuwa na kipato ili kuwawezesha waombaji wengine kunufaika nayo. 
Takwimu zilizotolewa Okotba mwaka juzi 2023, zilikuwa zinaonesha kwamba shilingi trilioni 1.34 kati ya shilingi trilioni 2.1 zinazodaiwa, sawa na asilimia 64 zilikuwa zimekusanywa na bado wakati huo kulikuwa na kiasi cha shilingi bilioni 758 ambacho kilikuwa hakijarejeshwa, licha ya wanufaika wengi kuwa na uwezo wa kulipa. 
Wigo wa utoaji mikopo kwa wanafunzi unaweza kuongezeka endapo wanufaika waliohitimu masomo yao watarejesha mikopo hiyo kwa wakati baada ya kuanza kuingiza kipato kwa kuajiriwa au kujiajiri. Bila marejesho mazuri kutoka kwa wanufaika, waombaji wengi watakosa mikopo na mwisho watashindwa kuendelea na elimu ya juu.


Kwamba, ni muhimu kwa wanufaika wahitimu wenye kipato yaani walioajiriwa au kujiajiri wenyewe kurejesha mikopo yao kwa hiari ili kuwa na uendelevu mzuri wa utoaji mikopo kwa kuzingatia kuwa kila mwaka kuna ongezeko kubwa la waombaji wa mikopo ambao wana sifa za kukopesheka na ambao kupitia marejesho ya wanufaika pamoja na fedha zinazotolewa na serikali, Bodi ya Mikopo itaweza kuwakopesha waombaji wengi zaidi.


Waajiri wanao wajibu wa kuwasilisha taarifa za wafanyakazi wao wenye elimu ngazi ya stashahada au shahada ili Bodi ya Mikopo iweze kujiridhisha kama wafanyakazi hao ni wanufaika wa mikopo au la. Na endapo itathibitika kuwa mfanyakazi ni mnufaika wa mkopo wa elimu ya juu, mwajiri atapaswa kukata asilimia 15 ya mshahara wa mfanyakazi mnufaika wa mkopo wa elimu ya juu kila mwezi na kuwasilisha makato hayo Bodi ya Mikopo hadi pale mfanyakazi mnufaika atakapomaliza deni lake lote.


Aidha, kwa waliojiajiri wenyewe kama mamalishe, babalishe, bodaboda, mafundi wa fani mbalimbali, wakulima, wafugaji, wavuvi na wengineo, wanaweza kujisajili kwenye mfumo ili kujua deni lao na kupata Namba Maalumu ya Malipo (Control number) ambayo wataweza kulipa kiasi fulani cha fedha kulingana na kipato wanachoingiza ili mwisho wa siku waweze kumaliza deni lote na kuwawezesha wengine kupata mikopo kama walivyopata wao. Pia, kupitia kujisajili huko kwenye mfumo, wahitimu wanufaika watajua mwenendo wa taarifa za madeni yao.


Kimsingi, utaratibu wa kulipa deni si lazima mnufaika awe ni mfanyakazi wa sekta rasmi yaani aliyeajiriwa. Hapana. Hata aliyejiajiri mwenyewe au asiye katika ajira rasmi anaweza kuanza kulipa deni lake hadi akamaliza kulilipa deni lote. Cha muhimu ni mnufaika mhitimu awe na kipato, na kipato kinaweza kuwa ni kwa kuajiriwa au kujiajiri.



Ni hivi: Lipo kundi kubwa la wanafunzi wanaohitaji kukopeshwa ili kutimiza ndoto zao za kielimu, njia mojawapo ya kuwasaidia wanafunzi hawa ni wanufaika wahitimu kulipa kwa hiari mikopo yao ili nao waweze kukopesheka. Pengine mhitimu mnufaika anaweza kuwa ana kipato lakini hajaanza kurejesha mkopo wake, ni vyema kujifichua na kuanza kulipa kwa hiari. Kwa kufanya hivyo, mhitimu mnufaika atakuwa ameshiriki kutimiza ndoto za kielimu za vijana wengi wanaohitaji kuwezeshwa mkopo, na huu ndiyo uzalendo na moyo wa kupenda maendeleo.
Ni vyema kila mnufaika ajiulize kwamba kama asingepata mkopo ingekuwaje kwake kupata elimu ya juu? Hivyo aone umuhimu wa kuwa sehemu ya kuhakikisha wadogo zake pia wananufaika kupitia yeye kwa kurejesha mkopo wake.



Cha kuzingatia ni kwamba umuhimu wa wanufaika kurejesha mikopo ni mkubwa kwa maendeleo ya elimu ya juu nchini. Mbali ya Fedha zinazorejeshwa kutumika tena kutoa mikopo kwa wanafunzi wengine kama ilivyoelezwa kwa msisitizo hapo awali, kurejesha mikopo kunasaidia kudumisha uadilifu na uwazi katika mfumo wa utoaji mikopo, na kuimarisha imani ya umma katika utendaji wa HESLB. 


Kwa ujumla, kurejesha mikopo ni jukumu la kijamii linalosaidia kujenga taifa lenye elimu bora na fursa za maendeleo kwa vizazi vijavyo.

Mwandishi ni Mwalimu wa Shule ya Sekondari Funguni iliyoko wilaya ya Pangani mkoani Tanga.

Maoni: 0620 800 462.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...