Mbunge Wanu Ameir Afungua Mafunzo Kuwajengea Uwezo Viongozi Uwt

GEORGE MARATO TV
0


Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kusingi Unguja, Mhe. Wanu Hafidh Ameir amefungua mafunzo elekezi kwa viongozi na watendaji wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kuanzia ngazi ya Matawi, Wadi, Jimbo na Wilaya yaliyofanyika kwenye ukumbi wa TASAF, Zanzibar

Wanu amefungua mafunzo hayo tarehe 20 Aprili, 2025 yenye lengo la kuwajengea uwezo viongozi na watendaji wa UWT hasa kutokana na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinapoelekea kushiriki uchaguzi mkuu wa kuchagua Rais, Wabunge, Wawakilishi na Madiwani nchi nzima ifikapo mwezi Oktoba, 2025.

Akizungumza katika mafunzo hayo, Mhe. Wanu Ameir amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwawezesha viongozi hao wa UWT ngazi zote kukumbuka wajibu wao hasa CCM inapokuwa kwenye uchaguzi na kupanga mipango ya ushindi

Mhe. Wanu Ameir amewasisitiza wanawake kuwa wasisite kujitokeza kuchukua fomu na kugombea nafasi za uongozi wa dola nchini kwani Wanawake wanaweza lakini ni lazima kwanza wathubutu kwa kuonesha nia ya kuwatumikia wananchi

Mwisho, Mhe. Wanu Ameir amewapongeza viongozi na watendaji wote wa UWT kwa kujitokeza kwa wingi kushiriki mafunzo hayo kwani hii imeonyesha wazi kuwa UWT wako tayari kujifunza ili kuongeza ufanisi katika majukumu yao.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top