Kwa Mujibu Taarifa iliyotolewa na CAF, Miongoni mwa sababu zilizochangia kusogezwa mbele kwa Michuano ya CHAN ni pamoja na kutokamilika kwa miundombinu ya kusakatia Kabumbu ikiwemo Viwanja pamoja na hoteli katika Mataifa ya Kenya,Uganda na Tanzania kulikotarajiwa kufanyika Michuano hiyo.
Kusogezwa mbele kwa Michuano ya CHAN hadi mwezi August kunalenga kuyapata fursa Mataifa hayo kukamilisha maandalizi yanayohitajika ili kuwezesha Michuano kufanyika kwa ufanisi.
Hata hivyo CAF imesema Droo kwa ajili ya kupanga Makundi ya CHAN itafanyika Januari 15 Mwaka huu Jijini Nairobi Nchini Kenya kama ilivyokuwa imepangwa