Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Waziri Mkuu aonesha vitendo katika kudhibiti matumizi ya kuni

*Azuru Makutupora JKT, Msalato Sekondari na Gereza la Isanga

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa leo (Alhamisi, Novemba 7, 2024) amefanya ziara jijini Dodoma ili kukagua utekelezaji wa Mkakati wa Kitaifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwenye taasisi zenye watu zaidi ya 100.

Waziri Mkuu ametembelea kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa ya Makutupora (834 KJ), shule ya Sekondari Msalato na Gereza la Isanga ili kuona utekelezaji wa maelekezo ya Serikali kuwa taasisi zote za Serikali na binafsi zinazotumia nishati ya kuni kuandaa chakula cha watu zaidi ya 100 kwa siku zisitishe matumizi ya kuni na mkaa kuwekeza katika matumizi ya nishati safi ya kupikia ifikapo Desemba 31, 2024. 


Akizungumza na viongozi wa mkoa wa Dodoma na wa taasisi zote tatu kwa nyakati tofauti, Waziri Mkuu aliwaeleza viongozi hao kwamba Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alishatoa maelekezo na yeye anapita kuangalia kama wamebadilisha mifumo inayotumika kwenye taasisi hizo.

“Nishati safi ya kupikia ni ubunifu wa Rais wetu ambaye amebobea katika masuala ya utunzaji mazingira, Rais wetu ametajwa kuwa ni kinara wa kampeni ya nishati safi barani Afrika. Tusije kushangaa akiwa kinara wa kampeni hii duniani, kwani ameshaenda Italia na Ufaransa kutoa mihadhara kuhusu nishati safi,” amesema.

“Kwa vile Afrika na dunia inamtambua, Watanzania tusibaki nyuma, na ndiyo maana tuliunda Kamati ya Kitaifa yenye wajumbe kutoka Tanzania Bara na Zanzibar. Wakati kampeni hii inaendelea, tumetoa fursa kwa wajasiriamali kuanza biashara ya kuuza mitungi ya gesi, mkaa mbadala na KUNIPOA kama njia ya kuwatoa wananchi wetu kwenye nishati chafu ambayo ni kuni za kawaida na mkaa wa miti.” 

Amesema majeshi, polisi, vyuo vya elimu ya kati na ya juu, vyuo vya wizara mbalimbali kama elimu, afya na kilimo ni baadhi ya maeneo ambayo yanapaswa kubadilisha mifumo yao ya kupikia kwani yana idadi kubwa ya watumiaji vya vyakula. 

Alitumia fursa hiyo kuwaagiza Wakuu wa Mikoa na Wilaya kote nchini, wafanye ukaguzi kwenye taasisi zote hizo na wahamasishe wajasiriamali wanaopika chakula cha watu wengi kama vile kwenye harusi ili nao waweze kubadilisha mifumo yao ya kupikia. “Kupitia Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya wa Dodoma, ninawaagiza Wakuu wa Mikoa na Wilaya kote nchini nendeni mkakague watu hao ili wabadilishe teknolojia zao, ziendane na matumizi ya nishati safi ya kupikia.”

Amesema ifikapo Desemba, mwaka huu wakuu hao watatakiwa watoe taarifa ya utekelezaji ikionesha ni taasisi ngapi tayari zimetekeleza agizo hilo. “Tunataka ifikapo Desemba, tujue taasisi ngapi tayari zimekamilisha, ngapi bado na mpango kazi ukoje wa taasisi hizo. Tunataka ifikapo mwaka 2033, tuwe na asilimia 80 ya Watanzania wanaotumia nishati safi ya kupikia.”

Mapema, akielezea utekelezaji wa programu hiyo kwenye makambi, Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa, Meja Jenerali Rajabu Mabele alimweleza Waziri Mkuu kwamba wameanza kutumia mfumo wa nishati safi kwenye vikosi vyote 26 vya JKT.

Alisema JKT kwa kushirikiana na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wanatekeleza mradi utakaowapatia majiko banifu na sufuria zake 291 kwa vikosi vyote, majiko ya gesi na sufuria zake 180, mitambo ya biogas tisa na majiko yake, mashine za kutengeneza mkaa mbadala 60 ambapo mafunzo kwa vijana kuhusu mitambo hii yataendeshwa na REA.

“Mradi wote utagharimu shilingi bilioni 5.7 ambapo REA watatoa shilingi bilioni 4.34 (asilimia 76) na JKT itachangia sh. bilioni 1.38 sawa na asilimia 24.”

Naye, Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Msalato, Mwl. Mwasiti Msokola alisema shule hiyo inatumia mkaa mbadala unaoitwa KUNIPOA ambao unatengezwa kwa kutumia maganda ya miwa, miti na pumba za mazao.

Alisema zamani walikuwa wakitumia sh. milioni 4.5 kila mwezi ili kununua kuni za kawaida, lakini kwa sasa wanaokoa sh. milioni 1.3 kwa kutumia KUNIPOA.

Kwa upande wake, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Jeremiah Katungu alisema Jeshi hilo kwa kushirikiana na REA linatekeleza programu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia magerezani ambayo inahusisha vituo 211 ambapo kati ya hivyo magereza ni 129, ofisi 26 za Magereza za Mikoa na Vyuo vya Magereza vinne.

Alitaja vituo vingine kuwa ni Makao Makuu, Bohari Kuu, Hospitali kuu ya Jeshi, Karakana, Shule ya Sekondari Bwawani, Kikosi Maalum na Kambi za Magereza 47. 

Alisema programu hiyo pia inahusisha utekelezaji wa miradi kadhaa ikiwemo ujenzi wa mitambo 126 ya Biogesi, usimikaji wa mifumo 64 ya gesi ya LPG, ununuzi wa tani 865 za Mkaa Mbadala wa Rafiki; ununuzi wa mashine 61 za kutengeneza Mkaa Mbadala unaotokana na Mabaki ya Mazao na kuimarisha matumizi ya gesi asilia katika magereza ya Lilungu (Mtwara), Keko na Ukonga Complex (Dar es Salaam).








Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...