Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Tanzania Kuungana na Dunia Usalama wa Afya Kimataifa


📌 Dkt. Biteko Ataja Jitihada za Serikali Kuboresha Ajenda ya Mpango wa Kimataifa wa Usalama wa Afya

📌 Dkt. Biteko Afungua Kongamano la 14 la CUHAS

📌 Dkt. Biteko Aipongeza CUHAS kwa Tafiti na Mchango wake katika Sekta ya Afya

📌 Wanasayansi Kuunganisha Afya ya Binadamu, Wanyama na Mazingira kwa Matokeo Bora ya Afya


Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mwaka 2015, Tanzania iliunga mkono Ajenda ya Mpango wa Kimataifa wa Usalama wa Afya na kuharakisha utekelezaji wa Sheria za Afya za Kimataifa ili kuzuia magonjwa ya kuambukiza kusambaa kimataifa. 

Kupitia tathimini ya pamoja ya mwaka 2023 matokeo ya maendeleo ya Tanzania katika suala hilo inaonyesha hatua kubwa ambapo mwaka 2016 imedhihirika  azma imara ya Serikali katika kutekeleza Sheria za Afya za Kimataifa kwa kutumia njia moja ikikubali uunganishaji wa afya ya binadamu, wanyama, na mazingira.

Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 13, 2024 katika ufunguzi wa Kongamano la 14 la Kimataifa la Sayansi la Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Sayansi za Afya (CUHAS) lililofanyika jijini Mwanza lenye kaulimbiu “Afya Moja na Usalama wa Afya wa Kimataifa”.

Ametaja jitihada zilizofanywa na Serikali za kuhuisha miongozo na mipango kazi ili kutekeleza Ajenda ya Mpango wa Kimataifa wa Usalama wa Afya.

  “Mwongozo wa Kitaifa wa Maabara na Usalama wa Bioteknolojia, Ajenda ya Mpango ya Kazi wa Taifa  wa Usalama wa Afya, Mpango wa Mkakati wa Afya Moja (2022-2027), Mpango Mkakati wa Kitaifa wa Kudhibiti Usugu wa Vimelea vya Magonjwa dhidi ya Dawa (UVIDA 2023-2028). Pamoja na kuhamasisha ukuzaji na uendelezaji wa raslimali watu na kuchochea ushirikiano wa kisekta,” amesema Dkt. Biteko.

Ameendea kusema kuwa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kufanya jitihada za kuhakikisha Usalama wa Afya wa Kimataifa hasa kwa kutoa ufadhili wa masomo na mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu kwa lengo la kuongeza nguvu kazi kila mwaka. 

“Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mheshimiwa, Dkt. Samia Suluhu Hassan, inathamini mchango wa  Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Sayansi za Afya pamoja na Kituo cha Tiba cha Bugando kwa ushirikiano na washirika wa ndani na kimataifa kwa kuwa mabingwa katika nyanja mbalimbali za utafiti zinazohusiana na Usalama wa Afya wa Kimataifa,” ameeleza Dkt. Biteko.

Ameongeza “Pia Serikali inathamini mchango uliotolewa na Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Sayansi za Afya kuanzia mwaka 2007 hadi 2023, ambapo kimezalisha zaidi ya wataalamu wa Afya 7,000 katika fani mbalimbali za tiba, dawa, uuguzi, maabara na uchunguzi wa kiafya, na uchomaji wa mionzi ambao wamekuwa mabingwa katika Usalama wa Afya ya Kimataifa.”

Aidha, Dkt. Biteko ameipongeza CUHAS kwa kuandaa makongamano hayo ya kisayansi yanayojadili masuala ya kisera ili kutatua changamoto zilizopo katika sekta ya afya na kusema kuwa afya ya binadamu inakumbwa na matishio mengi ili kukabiliana nayo ni lazima kufanya utafiti.

“Nawapongeza kwa kuleta wataalamu kwa ajili ya kujadili masuala ya tiba, niwapongeze pia kwa ugunduzi wa aina ya kirusi kinachoitwa Bugandosis ambacho kimebadilisha mfumo wa tiba na kutoa mchango katika sekta ya afya.

Fauka ya hayo amempongeza Prof. Stephen Mshana kutoka Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Sayansi za Afya kwa kuwa mwanasayansi bora kwa mwaka 2024.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Omary Kipanga amemshukuru Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha sekta ya umma na binafsi hususan katika elimu na afya, akitolea mfano kupitia mradi wa Elimu ya Juu na Mabadiliko ya Uchumi (HEET).

Mradi ambao umesaidia elimu ya juu na kuwezesha ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi ikiwemo kutoa ufadhili wa masomo kwa wafanyakazi wa Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Sayansi za Afya.

Mhe. Kapanga ameongeza kuwa Afya Moja inasisitiza kutafuta suhulu ya pamoja ya changamoto ngumu za kiafya na kuwa Kongamano hilo linasaidia wataalamu, wanasayansi na watunga sera kujadiliana kwa pamoja Usalama wa Afya.

“Ni matumaini yangu tutanufaika kutokana na utaalamu na matokea ya tafiti zilizofanyika awali na mikakati itakayosaidia kupunguza matishio ya afya, nakishukuru Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Sayansi za Afya kwa kuandaa Kongamano hili,” amesema Mhe. Kipanga.

Naye, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Sayansi za Afya Bugando (CUHAS), Prof. Erasmus Kamugisha amesema kuwa kauli mbiu ya Kongamano hilo Afya Moja inalenga kuleta muunganiko wa binadamu, wanyama na afya ya mazingira ambayo inaathiri jamii, taifa na dunia katika kufikia matokeo bora ya afya. 

Ameongeza kuwa Kongamano hilo linalofanyika kila mwaka limehudhuriwa na takribani washiriki 500 kutoka nchi mbalimbali duniani na litakuwa na tafiti za sayansi 150 zitakazojadiliwa kwa siku mbili.

Inaelezwa kuwa tafiti mbalimbali zinazowasilishwa kupitia makongamano hayo zimeweza kushawishi kubadilishwa kwa miongozo au sera za huduma za afya nchini ikiwemo mabadiliko ya dawa. 

Aidha, kwa mwaka 2024 yamechapishwa jumla ya machapisho 271 kuhusu mada mbalimbali za tafiti.


Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...