Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Rc Mtambi Aagiza Kusitishwa Uchaguzi wa Viongozi wa Mgodi wa Irasanilo

 


Na Ghati Msamba- Mara 

Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kanali Evans Mtambi, amemuagiza Afisa Madini wa Mkoa huo, Amin Msuya, kusitisha uchaguzi wa viongozi wa mgodi wa Irasanilo, uliopo Buhemba, Wilaya ya Butiama, na kupitia upya kanuni na katiba ya Kikundi cha Wachimbaji Wadogo wa mgodi huo ndani ya siku 21.

Ameyasema hayo kwenye kikao cha Wachimbaji Wadogo  na viongozi wao kilichofanyika katika ukumbi wa uwekezaji wa mkoa huo.

Lengo la kikao hicho ni kutatua changamoto za migogoro iliyopo baina ya wachimbaji wadogo na viongozi ili kila mmoja wao apate misingi stahiki ya kiutawala.

Amewataka pia wachimbaji kuachana na tabia za kujiwekea makundi ambayo hayatawasaidia lolote na badala yake wabadilike na waungane kwa pamoja ili waweze kujikuzia uchumi na kuendelea kusimamia shughuli za mgodi, ili viongozi waliokuwepo wapishe uchunguzi.

"Nimefuatilia hiki Kikundi kingetulia mngekuwa mbali, na mngekuwa mmeishaanzisha mradi wa ujenzi wa hoteli kubwa ambayo ingeweza kuwa chanzo cha kuwakuzia uchumi," Amesema Mtambi.

Aidha, mnamo Januari 15, 2024, Mkuu wa Wilaya ya Butiama, Moses Kaegele, alifanya kikao kilichowakutanisha pamoja Afisa Madini mkazi wa Mkoa wa Mara, viongozi wa mpito, na wawakilishi wa wanachama.

Katika kikao hicho, ilielekezwa kuwa viongozi wa muda wahudumu kwa siku 30 kuanzia tarehe ya kikao. Afisa Madini alielekezwa kubainisha majukumu yanayoweza/yasiyoweza kufanywa katika kipindi hicho cha uongozi wa muda.

Majukumu hayo ni kusimamia katiba ya kikundi, kusimamia na kuhakikisha shughuli za mgodi zinaendelea, kusimamia na kuhakikisha mapato ya kikundi na serikali yanakusanywa kwa mujibu wa taratibu zilizopo, kuwasilisha kikundi kwenye shughuli za nje ya kikundi, na kusimamia kulinda mali za kikundi.

Pia, viongozi wa mpito hawakutakiwa kusaini mikataba ya aina yoyote, kutokuajiri au kufukuza waajiriwa wa mgodi kwa kipindi hicho, kutoitisha uchaguzi wa aina yoyote ile, kutovunja au kutengua wajumbe wa kamati tendaji na kamati ya uongozi, na kutekeleza majukumu mengine ambayo hayataathiri taswira na ufanisi wa mgodi kwa ujumla.

Mkuu wa Mkoa amesema kuwa baada ya kusikiliza kero za wachimbaji, amebaini kuwa tatizo la Katiba na uongozi linahitaji hatua za haraka.

"Naagiza kamati yangu ya mgogoro, wanasheria, Afisa Ushirika, Afisa Maendeleo, na Mkuu wa Wilaya ya Butiama, kaeni na wachimbaji, mtakalia hapa Musoma au Butiama, kabla ya Ijumaa mkiangalia kama mtakuwa mmepitia Katiba hiyo na kutoa mapendekezo. Wiki ijayo, mnipatie rasimu hiyo ili niipitie," alisema Mkuu Mtambi.

Afisa Madini wa Mkoa wa Mara amesema kuwa ofisi ya madini ipo tayari kushirikiana na wachimbaji ili kuhakikisha mgodi unaendelea kufanya kazi vizuri na kuwa chanzo cha ajira stahiki.

Afisa Madini amesema walizuiwa baadhi ya majukumu kwa sababu viongozi wa mpito ni wa muda wa mwezi mmoja. Hata hivyo, Mwenyekiti na Katibu wa kikundi wanaendelea na majukumu yao kama viongozi wa muda.

Katibu wa muda wa Kikundi cha Irasanilo, Malima Bunyoga, amesema anatamani uchaguzi ufanyike kwa sababu hata yeye amepewa mipaka ya kazi, jambo ambalo limesababisha ashindwe kuwajibika ipasavyo. Alitoa malalamiko kuhusu Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kutoza gharama za matumizi ya umeme kwa makadirio badala ya malipo kupitia mfumo wa Luku.

"Umeme tunaolipa kwa TANESCO ni kwa makadirio, hatulipi kwa mfumo wa Luku. Kwa kipindi nilichokaa kwenye ukatibu, tangu Januari hadi Oktoba, tumelipa TANESCO zaidi ya Tsh. Milioni 182," amesema Malima.

"Malipo ya bili ya umeme mwaka 2024: Januari, Tsh. 5,484,558; Februari, Tsh. 7,480,932; Machi, Tsh. 19,424,512; Aprili, Tsh. 21,491,753; Mei, Tsh. 21,191,930; Juni, Tsh. 24,302,143; Julai, Tsh. 19,537,318; Agosti, Tsh. 18,674,079; Septemba, Tsh. 16,392,015; Oktoba, Tsh. 14,267,934; na Novemba, Tsh. 14,581,981, jumla ya fedha zote ni Tsh. 182,829,154," amesema Malima.

Ameongeza: "Mimi nimefungwa na majukumu, sihusiki tena kufanya kazi kwasababu mimi ni wa muda. Mgodi sio kwamba hautoi hela, unatoa hela lakini cha ajabu, mgodi hauna hela. Wakati tunaanzisha mgodi, watu tuliuza kuku."

"Uchaguzi unachelewesha mambo, uchunguzi unafanyika kwa gharama kubwa. Walitaka Tsh. Milioni 15 kwa uchunguzi wa awamu ya pili, tukavutana na tukataka watufanyie kwa Tsh. Milioni 4, lakini wilaya ililazimisha zikafika Tsh. Milioni 9. Viongozi wa wilaya wanaomba hela," amesema Malima.

"Wanafagilia wale wapigaji akikupa elfu 20,000 unasema fulani mzuri, huu mgodi ni wa kindugundugu. Halmashauri inatuumiza inatoza ushuru Tsh. 1,000 kwa kila kiroba chenye mawe yanayodhaniwa kuwa na dhahabu. Hiyo pesa ni kubwa sana na haitoi risiti ya mapato. Halmashauri haituletei faida itokanayo na makusanyo," amesema Malima.

Hata hivyo, ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama inalaumiwa kwa kuchelewa kumaliza ukaguzi wa viongozi wa Irasanilo waliotuhumiwa kwa ufujaji wa fedha za kikundi. Hadi sasa, ni miezi kumi, ofisi hiyo haijatoa ripoti ya uchunguzi wala kuwawajibisha waliobainika kuwa na makosa.

Kuchelewa kwa ripoti hiyo kumefanya viongozi wa muda kuendelea kushika nafasi hizo, jambo ambalo limekisorotesha kikundi, kwani viongozi wa mpito, akiwemo Mwenyekiti na Katibu, wamepewa mipaka ya majukumu, jambo ambalo linarudisha nyuma ufanisi wa kazi.


Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...