Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Fahamu Taratibu za Kupata Mikopo wa Kununua Vifaa Vya Solar Kwa Ajili ya Miradi yako Toka NMB Bank Tawi la Musoma



Na Emmanuel Chibasa-Musoma

Changamoto ya ukosefu wa fedha kwa wakulima wadogo katika wilaya ya Musoma Mkoani Mara, inatajwa kuwa sababu kubwa inayoplelekea kushindwa kumudu gharama ya kununua vifaa vya nishati ya umeme jua, kwa ajili ya shughuli za kilimo cha umwagiliaji na kusababisha chakula kinachozalishwa  kupotea baada ya mavuno kutokana na uhaba wa uhifadhi baridi na miundombinu duni ya usafirishaji, pamoja na ongezeko la joto linalochochewa na mabadiliko ya hali ya hewa.

Pia kukosekana Miradi inayotekelezwa na Kampuni za nishati ya jua katika wilaya ya Musoma kunachangia wakulima wadogo kuendelea kupoteza mazao ya Kilimo na Uvuvi baada ya mavuno kutoka na kukosa miradi inayoweza kuwasaidia  teknolojia  na vyumba vya uhifadhi wa baridi vinavyoendeshwa kwa nishati ya jua bila kuhitaji kuunganishwa kwenye gridi ya taifa, ili kulinda chakula baada ya mavuno hali inayochangia kuathiri mapato ya wakulima pamoja na uhaba wa chakula.

Inaelezwa kuwa, endapo  pampu zinazotumia nishati ya umeme jua zingekua zinapatikana kwa gharama nafuu kwa wakulima wadogo katika bara la Africa,  basi wakulima milioni 7 wangeweza kuongeza wingi wa mavuno angalau  kwa 30% na kusaidia kupunguza matumizi  ya pampu za maji Zinazotumia mafuta ya dizeli na kuepuka tani milioni 197 za uzalishaji wa CO2, na hii ni sawa na kuondoa magari ya petroli zaidi ya milioni 46 barabarani kwa mwaka mmoja, ambapo pia wakulima wangeweza kuokoa Dola za Marekani bilioni 50 kwenye gharama za mafuta.

Taasisi za kifedha ikiwa ni pamoja na benki za ndani zinatajwa kusaidia kutatua changamoto hizo kwa wakulima wadogo kwa kutoa mikopo kwa watumiaji wa mwisho wa teknolojia za vifaa vya nishati ya umeme jua, Lakini upatikanaji wa fedha  kwa wakulima wadogo, bado ni changamoto licha ya uwepo wa uhitaji mkubwa toka kwa wakulima hao ili kuweza kulima kilimo cha tija.

WAKULIMA WANAVYOSEMA KUHUSU UPATIKANAJI WA MIKOPO

Deus Gondela mkulima mkazi wa Musoma Vijijini anasema kwa wakulima wadogo kupata fedha benki ni changamoto licha ya kuwa na dhamana ya mashamba wanayotumia kulima mazao ya chakula na biashara, lakini bado taasisi za benki haziwaamini huku taasisi nyingine za fedha wanapoweza kupata mikopo zikiwa na riba kubwa.

“ Sisi wakulima wadogo bado hawatuamini huko kwenye mabenki, niliwahi kwenda benki kuomba mkopo kwa ajili ya kulendeleza kilimo changu lakini alikuja mfanyakazi kutembelea eneo langu na kunihoji maswali na mwisho aliniambia ni vigumu kupata mkopo kwa sababu sikua na vielelezo vinavyoonesha mwenendo wa kilimo change katika kuingiza kipato” Amesema Deus

Joseph Okaka mkulima mkazi wa kijiji cha Bugwema Musoma Vijijini anasema licha ya serikali kuhamasisha wakulima wajiunge katika vikundi, ili waweze kupata mikopo katika taasisi za fedha kwa ajili ya kusaidia kuendesha shughuli zao za kilimo, lakini changamoto inayojitokeza ni baadhi ya wanakikundi kutokua waaminifu katika kurejesha fedha za mikopo hali inayopelekea benki kushindwa kuendelea kuwapa mikopo.


“Mimi binafsi naona kukosekana kwa uaminifu kati yetu ndio sababu tunakosa fursa za mikopo, mfano hapa kijijini sisi kama wakulima wa kilimo cha umwagiliaji hatuna kikundi na kila mtu analima kwa uwezo wake na anajua mwenyewe jinsi ya kujitafutia fedha kutokana na kukosekana kwa uaminifu kati yetu lakini pia hizo benki nazo haziji kututembelea ili ziweze kutusaidia hata kwa mkulima mmoja mmoja” Amesema Okaka.

Naye Loyce Joshua mkulima wa shamba la mboga mboga katika kijiji cha Bugwema anasema kutokana na kukosa mafaniko katika kilimo cha umwagiliaji kwa kutumia pampu za mafuta kunamfanya ashindwe kukopa fedha kwenye taasisi za fedha kutokana na kutojua namna nzuri ya kurejesha fedha hizo huku Penina Marcus akieleza uhitaji wa mafunzo ya maswala ya fedha na uwezeshwaji wa fedha zisizo na riba ili kwanza waweze kukua na kuimaisha uchumi katika shughuli zao za kilimo cha umwagiliaji.


UPATIKANAJI WA MIKOPO BENKI

Hali ya Upatikanaji wa mikopo Kwa wakulima wadogo  katika benki hapa nchini inaelezwa kuwa bado ni changamoto kutokana na masharti yanayowekwa na Benki.

Wakulima wadogo nao bado wanahitaji kubwa la fedha  kwa ajili Kusaidia kuendeleza shughuli zao za kilimo Ikiwa ni pamoja na kumudu gharama ya kununua vifaa vya nishati ya umeme jua lakini wanashindwa, hali inayopelekea wakulima wengi kushindwa kutumia teknolojia hiyo sababu  gharama nyingi ziko kwa watumiaji wa mwisho kama wauzaji wa vifaa na wakulima wadogo.

Sopeter Justin ni meneja wa NMB Bank tawi la Musoma, anasema katika benki hiyo wanatoa mikopo kwa wakulima na kuna mtaalam ambaye anahusika kushughulikia maswala ya wakulima.

Anasema changamoto kubwa kwa wakulima wadogo kushindwa kupata mikopo benki ni kutokana na wakulima wadogo kutokua na utaratibu wa kuweka kumbukumbu ya jinsi ya wanavyoendesha shughuli zao za kilimo pamoja na kutokua na utaratibu wa kutunza fedha zao benki pindi wanapovuna na kuuza mazao yao.

Ameongeza kuwa kutokana na wakulima kutokua na akaunti benki inawapa wakati mgumu kutambua kiasi cha Fedha anachopata Katika shughuli zake za kilimo  ili aweze kukadiriwa kiasi kinachaweza kukopeshwa na kumsaidia kuendesha shughuli zake lakini pia kurejesha fedha za mkopo bila Changamoto yeyote.

“ Sisi kama benki ya NMB tuko tayari kumkopesha mkulima au mtu yeyote anaehitaji kuwekeza kwenye nishati ya umeme jua katika miradi ya kilimo, uvuvi na hata uzalishaji mwingine lakini unakuta mkulima anakuja kufuata huduma ya mkopo anahitaji mfano kukopa milioni tano, unaenda kumtembelea kweli unakuta ana shamba lakini ukimuliza akuoneshe rekodi jinsi anavyouza mazao yake unakuta hana, ukimwambia tunahitaji tuone rekodi za fedha katika akaunti yako unakuta pia hana.

Mkulima huyu anakwambia we nipe tu mkopo ntaweza kurudisha fedha, Hii ndio changamoto kubwa kwa wakulima wadogo katika kupata mikopo benki." Amesema Sospeter

Nawaomba wakulima katika mkoa wa Mara wanaohitaji kuwekeza kwenye miradi ya nishati ya umeme jua waje tuwahudumie fedha zipo, Wakulima wadogo nawaomba waanze kujenga utaratibu wa kuweka rekodi ya shughuli zao za kilimo katika maandishi lakini pia wafungue akaunti  ambazo watakua wanatumia kuweka na  kutoa fedha pindi wanapouza mazao yao ili kutuweza kufahamu mzunguko wa fedha zake utakaotuwezesha kufahamu kiasi cha fedha anacho stahili kukopa” Amesema Sospeter


USHAURI WA WADAU KWA BENKI KUHUSU MIKOPO

Majura Maingu ni Meneja wa shirika la Victoria Fishing and Farming Organization(VIFAFIO) lenye makao yake makuu katika halimashauri ya manispaa ya Musoma, anasema benki nyingi hapa nchini zimekua zikiogopa kuwakopesha wakulima kutokana na kutokua na uhakakika wa kurejesha fedha zao, kutokana na changamoto mbalimbali zinazokuwa zinawakabili wakulima ikiwa ni pamoja na mabadiriko ya hali ya hewa inayopelekea mkulima kutokua na uhakika wa kupata mavuno.

Pia anasema wakulima wengi katika maeneo ya vijijini wanaendesha shughuli za kilimo katika mashamba ya familia na moja ya hitaji kuu la benki katika kupata mkopo ni lazima uwe na dhamana. Hali hii inapelekea kushindwa kutimiza masharti ya benki huku changamoto nyingine akisema ni taasisi za benki kutoruhusu pia mifugo kutumika kama dhamana.

“ Ushauri wangu kwa Benki mbali  na kuangalia dhamana ya eneo la mkulima wangeweka pia utaratibu wa wakulima wenye katika vikundi kuwadhini wenzao ili kusaidia kurahisisha upatikanaji wa mikopo kwa urahisi ili kurahisisha kuwafikia wakulima wengi zaidi na ambao pia wantumia mashamba ya familia na wanashindwa kuweka dhamana ya mashamba.” Amesema Majura

Ukuaji wa matumizi ya teknolojia ya nishati ya jua yataongezeka kwa kasi endapo wakulima na watumiaji wa nishati ya umeme jua watapata vifaa kwa ghrama nafuu hasa katika maeneo ya vijijini na ukuaji wake unategemea watumiaji wa mwisho kumudu teknolojia hii ambao wengi wao kwa sasa. Hawawezi hali inayopelekea asilimia 90% ya wakulima Kusini mwa Jangwa la Sahara ambao wangeweza kufaidika na pampu za maji  zinazotumia nishati ya za jua hawawezi kumudu kutokana na gharama za juu za awali au ukosefu wa mikopo.



Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...