Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Aliyosema Waziri wa Madini Anthony Mavunde Katika Mahojiano Maalum na Crown Media Kupitia Kipindi cha Kasri la Kikeke


 *Kuelekea Mkutano wa Kimataifa wa Uwekezaji katika Sekta ya Madini Tanzania 2024*

*Na Wizara ya Madini*

*Ukiuza Madini Nje ya Soko wewe ni mtoroshaji*

Tulikuwa na changamoto ya biashara ya Madini kabla ya mwaka 2017 ambapo ilifanyika kiholela kutokana na kukosekana kwa masoko ya madini. Hivi sasa biashara yote inafanyika sokoni, ukiuzia nje ya Soko wewe ni mtoroshaji unakiuka Sheria za nchi na kupoteza mapato ya Serikali.

*Tozo kwenye uchimbaji mdogo*

Nimefanya vikao na wadau mbalimbali kusikiliza hoja zao lengo ni kuangalia namna ya kutatua changamoto kwenye shughuli za uchimbaji mdogo wa madini na biashara ya madini. Hivi sasa kodi zote zinazolipwa Serikalini zimebaki asilimia 9.3 kutoka 38. Mrabaha ni asilimia 6, ada ya ukaguzi asilimia1, TRA asilimia 2 (withholding tax) na Service levy asilimia 0.3. Serikali imechukua hatua kubwa kusikiliza changamoto za wachimbaji wadogo, kodi inayokusanywa inasaidia kujenga nchi yetu.

*Mkakati wa Kuongeza Thamani Madini Nchini*

Kwenye hotuba yangu ya Bajeti nilieleza kuhusu mpango wa Serikali kutoendelea kutoa Leseni za uchimbaji mkubwa wa madini kama mwekezaji haleti mpango unaoridhisha wa uongezaji thamani madini. Uongezaji thamani madini unalenga kubakiza ajira nchini, ujuzi na kuongeza mapato ya nchi yetu. Suala hili kwenye Mkutano wetu wa Uwekezaji utakaofanyika tarehe 19-21 Novemba, 2024, ni jambo ambalo linakwenda kuubeba mkutano wetu.

*Tanzania kuwa Kinara wa Madini Afrika Mashariki na Kati*

Kupitia Kiwanda cha Kusafisha madini ya metali kitakachojengwa Buzwagi Kahama na Kampuni ya Tembo Nikeli kutaifanya Tanzania kuwa kinara katika uongezaji thamani madini kupitia kiwanda hicho ambacho mtaji wake ni Dola za Marekani Milioni 500. Mradi huu utakuwa ni fursa kubwa kwa Tanzania kujitangaza.

*STAMICO na Soko la Hisa*

Tumewapa leseni za utafiti Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) tunataka taarifa zao wazipeleke Toronto, London Exchange market, niliwaambia STAMICO nataka niwaone wakishindana na kampuni kubwa kama Barrick na GGML. STAMICO ni shirika lililokuwa linakwenda kufa lakini sasa hivi shirika hili linafanya vizuri sana. Shirika hili limetoka kukusanya shilingi bilioni 2 hadi bilioni 80.

*Megawati Elfu Mbili za Makaa ya Mawe*

Tuna mradi mkubwa wa kuchimba makaa ya mawe Kiwira unaofanywa na STAMICO. Tumeanza majadiliano na kampuni moja ya India yakienda vizuri kupitia mradi huo tutazalisha megawati za umeme Elfu Mbili kupitia makaa ya mawe.

*Mpango wa kuwainua wachimbaji wadogo*

Nataka nione wachimbaji wadogo wana graduate kutoka kwenye uchimbaji mdogo kwenda wa Kati. kupitia Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) tumenunua mitambo 15. tayari tumepokea mitambo Mitano (5), na imekwishaanza kazi kwa ajili ya shughuli za uchorongaji ili kuwasaidia kupata taarifa za sahihi.

*Kuwaendeleza wachimbaji wadogo*

Kupitia vituo vyetu vya mfano vya Lwamgasa Geita, Katente-Geita na Chunya, tunawaandaa wachimbaji kutumia teknolojia rahisi ili kuachana na matumizi ya zebaki. Tumefunga  mitambo ya kuchenjua dhahabu kubadili mtazamo wa matumizi ya zebaki hivi sasa wachimbaji wengi wameanza kufunga mitambo hiyo. Leo nina furaha kubwa kati ya shilingi bilioni 753 zilizokusanywa Mwaka wa Fedha 2023/24, asilimia 40 imechanganyiwa na wachimbaji wadogo.

*Mkaa wa Kupikia wa Rafiki Briquettes*

Tunatengeneza mkaa wa kupikia wa Rafiki Briquettes unaotokana na makaa ya mawe, ulianza kama majaribio na tayari hivi sasa wamefunga mashine mbili na wameanza kutafuta mawakala.

*Liganga na Mchuchuma*

Mradi huu umekuwa na historia ndefu na kilio cha watanzania wengi ni kutaka mradi huu uanze. Hivi sasa tuko kwenye hatua nzuri na tayari fidia zimekwishalipwa.

*Shilingi Bilioni 115 zimeelekezwa kwenye Utafiti wa Madini*

Katika Mwaka wa fedha 2024/25 tumepanga kununua helicopter itakayofungwa vifaa kwa ajili ya shughuli za utafiti wa madini. Utafiti ni moja ya kazi zinazotumia gharama kubwa sana, Napenda kumshukuru Mhe. Rais Samia kwa sababu kwa mwaka huu wa fedha Bajeti ya Wizara imeongezeka kufikia shilingi bilioni 231 huku shilingi bilioni 115 ni fedha za maendeleo kwa ajili ya utafiti.



Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...