Watumishi wa umma nchini Uganda wanaoendesha biashara za kibinafsi ndani ya sekta zao za kitaaluma sasa wanakabiliwa na matarajio ya athari mbaya, huku serikali ikijiandaa kubana kuanzia Julai 1, 2025.
Hatua hiyo ambayo imekuwa mjadala kwa miaka mingi, inalenga kutekeleza uzingatiaji wa kanuni za utumishi wa umma huku serikali ikilenga zaidi sekta za afya na elimu kwa kuanzia.
Mara nyingi mijadala juu ya suala hilo imekuwa ikijitokeza, huku walimu wengi walio katika utumishi wa umma wakituhumiwa kutumia muda wao mwingi katika shule binafsi huku madaktari wakitajwa kujihusisha na wizi wa vifaa tiba vya kliniki zao, rufaa zinazotia shaka na utoro kazini.
Maafisa kadhaa wa umma katika sekta ya afya wanamiliki hospitali, zahanati, maduka ya dawa na pia wanajishughulisha na ajira za kudumu huko nje.
Ni zaidi ya hivyo katika sekta ya elimu ambapo walimu katika shule za umma wamekuwa wakifundisha kwenye shule za kibinafsi huku maafisa kadhaa akiwemo waziri wakiendesha shule zao wenyewe na kusababisha migongano ya kimaslahi.
Dennis Mugimba, msemaji wa Wizara ya Elimu na Michezo, amethibitisha kwamba marufuku hiyo si sera mpya bali kwa sasa inatekelezwa vikali.
"Ukizungumzia kanuni za kudumu za utumishi wa umma, huruhusiwi kushika kazi mbili. Huwezi kuwa sehemu mbili kwa wakati mmoja. Huwezi kuajiriwa na serikali na sekta binafsi kwa wakati mmoja," Mugimba alieleza.
Wakati sera hiyo inaakisi mbinu inayotumika katika nchi jirani ya Rwanda, ambapo watumishi wa umma, wakiwemo madaktari, wamepigwa marufuku kujihusisha na kazi za kibinafsi, hali ya Uganda ni tofauti.
Nchini Rwanda, watumishi wa umma wanalipwa fidia ya mishahara ya juu na mazingira bora ya kazi, ambapo nchini Uganda, wafanyakazi wengi wa serikali katika sekta ya afya na elimu hutegemea mapato kutoka kwa kliniki za kibinafsi ili kuongeza mishahara yao ambayo mara nyingi haitoshi.
Hii imesababisha wasiwasi kwamba kutekeleza marufuku hiyo kunaweza kuzidisha uhaba mkubwa wa wafanyakazi katika mfumo wa huduma ya afya ya umma nchini Uganda.
