Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Maambukizi ya Virusi vya Ukimwi yaendelea Kupungua Nchini


 Na. Aron Msigwa Songea, Ruvuma.

Waziri wa Afya, Mhe. Jenista Mhagama amesema kiwango cha ushamiri wa maambukizi ya Virusi vya UKIMWI nchini Tanzania kimepungua kutoka asilimia 7 mwaka 2003/2004 mpaka asilimia 4.4 mwaka 2022/23 kufuatia juhudi mbalimbali zinazofanywa na Serikali na wadau wa Sekta binafsi. 

Mhe. Mhagama ameyasema hayo leo Novemba 29,2024 mjini Songea, Ruvuma wakati akifungua kongamano la kitaifa la kisayansi na uzinduzi wa usambazaji wa ripoti ya utafiti wa viashiria na matokeo ya UKIMWI wa mwaka 2022/23 ambapo amesema kiwango cha maambukizi pia kimepungua kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto kutoka asilimia 18 za mwaka 2010 hadi asilimia 8.1 mwaka 2023 hali inayoongeza usalama wa watoto.

Leo tunazindua usambazaji wa ripoti ya matokeo ya utafiti wa viashiria vya UKIMWI mwaka 2022 - 2023 katika Kongamano lililohusisha wadau kutoka maeneo mbalimbali nchini. Takwimu hizi zitasaidia makundi mbalimbali katika kupanga mipango ya maendeleo Amesema Mhe. Mhagama.

Ameongeza kuwa ripoti ya utafiti iliyozinduliwa inaiwezesha Serikali kufahamu hali halisi ya kiwango cha maambukizi ya VVU pia kuonesha mafanikio, changamoto na mikakati inayopaswa kuchukuliwa katika mapambano dhidi ya VVU huku akiipongeza Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) na Baraza la Watu wanaoishi na VVU nchini Tanzania (NACOPHA) kwa kuweka mikakati imara , kuishauri Serikali na kuwaelimisha Watanzania kuhusu mapambano dhidi ya VVU.

Natoa wito kwa viongozi wenzangu na watu wenye uwezo wa kusambaza taarifa hizi wakiwemo wanamichezo, viongozi wa dini, wanasiasa, waandishi wa habari washiriki kikamilifu katika usambazaji wa takwimu hizi 

Amesema Serikali inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imekuwa mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI kwa kuimarisha huduma za afya nchini hali iliyochangia kwa kiasi kikubwa kupunguza maambukizi ya VVU.

 Natoa wito kwa kila Mtanzania kuwa mlinzi wa mafanikio ya mapambano hayo hapa nchini ili kuongeza ufanisi wa mapambano dhidi ya hali zote za unyanyapaa. Wizara tumetenga fedha kwa ajili ya kuanzisha kituo cha pamoja dhidi ya mapambano ya VVU, uanzishwaji wa miongozo na kusisitiza uzingatiaji wa mila na desturi nzuri za unasihi katika maeneo ya utoaji wa elimu katika maeneo mbalimbali nchini 

Katika hatua nyingine ametoa wito kwa TACAIDS , wadau wa sekta ya umma na binafsi waendelee kuwekeza katika Sekta ya afya katika uanzishaji wa viwanda vya uzalishaji bidhaa, vifaa tiba na dawa zinazohusiana na udhibiti wa UKIMWI na VVU ndani ya nchi.

Aidha, amesema Serikali inaendelea kutoa hamasa ya utoaji wa huduma za msingi kwa kuongezea nguvu zaidi katika kuyafikia makundi yaliyo katika hatari ya maambukizi ya VVU yakiwemo makundi ya vijana wenye umri wa miaka 15 hadi 24, madereva wa malori ya masafa marefu, wachimbaji wa madini migodini, wavuvi, wafanyakazi wa mashamba makubwa na kutoa wito kwa akina Baba wawe na hamasa ya kwenda kupima VVU ili kuongeza ushiriki wao katika mapambano dhidi ya VVU nchini.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Taifa ya kudhibiti Tanzania (TACAIDS) Dkt. Jerome Kamwela ameishukuru Serikali ya Mkoa wa Ruvuma kwa kukubali kuwa mwenyeji wa kongamano hilo na tukio la uzinduzi wa usambazaji wa ripoti ya utafiti wa viashiria na matokeo ya UKIMWI wa mwaka 2022/23 ambapo amesema utafiti huo ulifanyika kwa watu wenye umri wa miaka 15 na kuendelea na hufanyika kila baada ya miaka 5.

 Tumelenga kumaliza janga la UKIMWI mwaka 2030. TACAIDS tumepanga kusambaza matokeo ya utafiti huu kwenye ngazi ya Miko ana Wilaya ili kuwezesha wadau mbalimbali kupata taarifa za utafiti huo na kuchukua hatua na kuongeza juhudi za kupambana na maambukizi mapya ya VVU pia kuweka mikakati katika maeneo ambayo bado yana changamoto.

Amesisitiza kuwa TACAIDS kwa kushirikiana na wadau wa masuala ya VVU na UKIMWI imeandaa mpango endelevu wa mwitikio wa VVU na UKIMWI unaolenga kuongeza mikakati ya uendelevu ambayo Tanzania itatekeleza mpango wa kupunguza maambukizi mapya ya VVU na vifo vinavyotokana na UKIMWI kwa asilimia 95, kupunguza unyanyapaa na ubaguzi hadi chini ya asilimia 5.

Naye Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Salum Kassim Ali Akizungumza wakati wa uzinduzi wa ripoti hiyo ameeleza kuwa matumizi ya takwimu rasmi ni muhimu katika kuchochea maendeleo nchini, kuongeza uwajibikaji, kuleta mabadiliko na matokeo chanya yaliyokusudiwa katika mipango yote ya maendeleo.

Amesema takwimu rasmi zinazotokana na utafiti wa viashiria na matokeo ya UKIMWI za mwaka 2022 -2023 zitaiwezesha Tanzania kujipima na kutathmini ufanisi wa mbinu za kukabiliana na maambukizi mapya ya VVU akisisitza kuwa takwimu zilizokusanywa zimezingatia vigezo vyote na zitasaidia kupanga mipango ya ndani na kutumiwa na wadau mbalimbali wa ndani na nje ya Tanzania.

 Nawaomba watumiaji wa takwimu hizi wasipotoshe, wazitumie kwa usahihi na sio kwa lengo la kupotosha au kujipatia umaarufu kwa kuwa yanalindwa na Sheria amesema Salum Kassim Ali.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Programu, CDC Dkt. George Mgomella Akizungumza kwa niaba Balozi wa Marekani nchini Tanzania ameeleza kuwa Tanzania imeendela kupata mafanikio katika mapambano dhidi ya VVU kupitia programu mbalimbali ambazo zimesaidia kwa kiwango kikubwa kupunguza madhara kwa watu wanaoishi na VVU na maambukizi mapya ya VVU.

Amesema matokeo ya utafiti wa viashiria vya UKIMWI kwa mwaka 2022 - 2023 yanaonesha kuwa utoaji wa huduma kwa wanaoishi na VVU na uzuiaji wa maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto wakati wa kujifungua umeimarika nchini Tanzania.

Utafiti huu unatupa kazi ya kuongeza nguvu zaidi katika eneo la kukabiliana na maambukizi mapya husani kwa kundi la vijana kuanzia Miaka 15 amabao wanaonekana kuchangia maambukizi mapya. Serikali ya Tanzania imejitahidi kuimarisha huduma za afya, kushirikiana na wadau mbalimbali kuboresha huduma Kinga na matibabu kwa wananchi  

 Akizungumza kwa niaba ya Baraza la Watu Wanaoishi na VVU Tanzania (NACOPHA), Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza hilo, Deogratius Rutata ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais Samia kwa kuendelea kuijali jamii ya watu wanaoishi na VVU Tanzania kwa kuipatia dawa za kufubaza VVU 

Tunaishukuru Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kuendelea kuimarisha utoaji wa taarifa zikiwemo takwimu za kuhusu maambukizi ya VVU na UKIMWI hapa nchini kwa mwaka 2022-2023 .Hatua hii inatuongezea jukumu la kuongeza mapambano zaidi ya kufikia maambukizi sifuri ifikapo 2030.

NACOPHA tutaendelea kushirikiana na Serikali na wadau wengine wa Afua za UKIMWI kuunga mkono mapambano dhidi ya maambukizi VVU kwa kuwa tunalo jukumu muhimu la kuisaidia Serikali na jamii nzima kupata matokeo chanya.




Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...