Wananchi wa kijiji cha Magubike wilayani Kilosa Mkoani Morogoro wamefunga barabara kuu ya Dodoma-Morogoro kwa zaidi ya saa Saba baada ya mtoto Nuru anayesoma elimu ya awali kugongwa na gari inayodaiwa kuwa ya serikali.
Kufungwa kwa barabara hiyo kuu ya Morogoro -Dodoma kumesabisha msururi mkubwa wa magari yakiwemo mabasi ya abiria
Uamuzi wa kufunga barabara hiyo umechukuliwa na wananchi ili kushinikiza serikali kuweka matuta kwenye eneo hilo ili kupunguza ajali zinazotokea Mara kwa Mara na kukatisha uhai wa baadhi ya watu na kujeruhi wengine.
Akiwa katika eneo hilo,Dkt.Jafo alilazimika kuzungumza kwa njia ya siku na Waziri wa ujenzi Innocent Bashungwa ambaye ameahidi wakala wa barabara nchini(Tanroads) katika kwenye eneo hilo na kuweka matuta.
Akizungumza na wananchi hao,Jafo amewaomba kuwa na subra jambo hilo ameliona na amewasiliana na waziri Bashungwa na hatua za haraka zitachukuliwa kama wananchi wanavyotaka