Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Makonda, akiwasili katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC), linapofanyika Kongamano la Tano la Idhaa za Kiswahili Duniani, leo Machi 24, 2026.
Kongamano hilo limeandaliwa na Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA), likiwakutanisha wadau wa lugha ya Kiswahili kutoka ndani na nje ya nchi, na mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla.










