Hakuna Taifa Endelevu Bila Usimamizi wa Haki - Rais Samia

GEORGE MARATO TV
0


Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan amesema hakuna Taifa  lenye maendeleo  endelevu na ustawi   wa  watuwake bila usimamizi mzuri wa haki

Dkt. Samia ameeleza hayo leo januari 13, 2026 wakati akifungua mkutano mkuu wa mwaka wa chama cha mahakama na majaji Tanzania (TMJA) uliofanyika viwanja vya makao makuu mahakama mkoani Dodoma




Uwepo wa mahakama huru yenye uwezo na uadilifu ni nguzo muhimu  ya utawala  bora na msingi wa upatikanaji wa haki

Serikali itaendelea kuulinda na kuuheshimu uhuru wa mahakama bila kujali itikadi. 

Ametoa rai kwa majaji na mahakama  kuwa uhuru huu hamna budi kwenda sambamba na uwajibikaji, uadilifu, nidhamu na utii wa sheria na uzalendo kwa Taifa letu. 



Aidha amesema Watanzania wanamatumaini makubwa sana na wangependa kuona mahakama inagosimamia haki kwa uwazi na kwa kuzingatia misingi ya kikatiba sheria na utu. 

Kwa Upande wake Jaji mkuu wa Tanzania Ndg.George Masaju ameiomba  serikali  kuiongezea mahakama bajeti ili iweze kufanya maboresho ya kiutendaji katika mahakama zake 

Na Rais wa chama cha mahakimu na majaji amesema katika mkutano huo wa 41  ume hudhuriwa na wanachama 1200  kati ya 1700







Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top