Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Uongozi wa Shule za Kaizerege Wamshukuru Rais Samia


Na Angela Sebastian; Bukoba 

UONGOZI wa shule za Kaizirege na Kemebos zilizopo Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera wamemshukuru Dk.Samia Suluhu Hassan kwa nia yake ya kugharamia masomo ya elimu ya juu ndani na nje ya nchi, wanafunzi wanne wa shule hiyo waliohitimu kidato cha sita mwaka huu kati ya 50 wa mchepue wa Sayansi nchi nzima.

Wanafunzi hao waliopata matoke ya daraja la kwanza la alama tatu katika mchepuo wa Sayansi ni Anitha  Kulwa aliyekuwa akisoma PCM,Bright Yohana PCB pia Christopher Wambura na Cleophas Wambura ambao ni watoto mapacha waliosoma PCB.

Wakato huohuo uongozi wa shule hiyo umetoa tuzo yenye thamani ya shilingi milioni 20 kwa wanafunzi hao kama motisha na pongezi kwa matokeo hayo.

Mkurugenzi wa shule za Kaizirege na Kemebos Eusto Ntagalinda akikabidhi tuzo hizo jana shuleni hapo Minispaa ya Bukoba ambapo alimshukuru Dk.Samia kwa kutoa ufadhili huo wa masomo kwa vijana hao wanne ambao walikuwa wakisoma mchepuo wa Sayansi hari itakayosababisha wengine kuiga mfano huo wa kufanya bidii katika msomo na kupata matokeo mazuri.

Akikabidhi tuzo hizo Ntagalinda amesema alianzisha tuzo hiyo kwa ajili ya wanafunzi wanaofanya vizuri katika matoke ya kidato cha sita na kuingia 10 bora kwa lengo la kuweka hamasa kwa wanafunzi wote ili waweze kusoma kwa bidii, kupata matokeo mazuri na ya heshima. 

"Kwanini ninaamua kutoa zawadi kwa wanafunzi wanaofanya vizuri siyo kwamba nina fedha nyingi bali ni kuhamasisha wanafunzi wote wanaosoma hapa kusoma kwa bidii,yawezakana hii tuzo ndiyo iliyowaongezea nguvu ya kusoma na kupata matokeo mazuri ambayo yametuheshimisha sisi,wao na Taifa letu"ameeleza Ntagalinda. 

Amesema watoto hao wameishavuna mengi wameua ndege wengi kwa jiwe moja ambapo ufaulu wao wa juu umewapatia zawadi ya kila mmoja kupata shl mil tano pia kutokana na taarifa nilizopata kutoka kwa mkuu wa shule kuwa wanafunzi hao wamepata ufadhili na si mkopo bali watasomeshwa na Serikali bure elimu yao ya juu.

Amesema kuwa mtoto anapofauru masomo yake vizuri ni furaha na fahari kwa wazazi,jamaa na ndugu hivyo ata hawa wameishapata zawadi nyingi tangu matokeo yalipotangazwa ikiwemo kwenda kusoma bure na kupitia kujituma kwao wataweza kupata nafasi nzuri za kazi Serikali pindi watakapo maliza masomo ya elimu ya juu. 

Aidha amewashauri wanafunzi walioko katika madarasa ya mitihani kujituma na kusoma kwa bidii,kutumia muda mwingi kwenye masomo kwasababu wamekwenda shuleni kusoma na si vinginevyo,kwani wanatofautiana kiuwezo wa darasani kwani binadamu hawalingani hivyo linalowezeka kwa wakati huo lisingoje kesho watumie muda wao vizuri kusoma.

"Wanafunzi waliobaki jiepushe na makundi yasiyofaa na jiwekeeni malengo ya kufanya vizuri katika masomo yenu na kupata matokeo mazuri maana mimi mkurugenzi wenu nipo tayali kuendelea kutoa zawadi kwa kila atakayekudhi vigezo na sitajali idadi ya wanafunzi hivyo nipimeni kwa kufauru ndipo mtanifahamu kuwa naguswa na matokeo mazuri "ameeleza mkurugenzi. 

Kwa upande wa mkuu wa shule hizo mwalimu Kishe Ilamulira ameeleza kuwa wanafunzi hao watagharamiwa masomo yao ya vyuo vikuu na Rais Dk. SamiaSuluhu Hassan,ambapo Anitha atakwenda kusoma nje ya nchi kwani amekuwa mwanafunzi wa tatu kitaifa kati ya wanafunzi 50 wa mchepuo wa Sayansi wenye hesabu ndani yake huku Bright,Christopher na Cleophas watasoma vyuo vikuu vya ndani ya nchi.

Amesema tuzo hizo zinaongeza molali kwa wanafunzi wa kidato cha tano na sita ili kuweza kufanya vizuri katika mitihani yao ya Taifa.

Kwa upande wa wanafunzi hao wamesema siri ya mafanikio yao katika kupata ushindi  shuleni  hapo ni kuomba Mungu, kujiwekea malengo,kusoma kwa bidii,kujiamini,ushirikiano, kujikubali na kujifunza vitu vipya na kuheshimu kila mmoja kwa nafasi yake na kijituma.

Anitha Kulwa ni mmoja wa wanafunzi hao amesema shule yao inatayalisha wanafunzi kwa kutoa elimu bora,kuwajengea vipaji na kujiamini ambapo mambo hayo huwasaidia katika kutujengea uwezo wa kujiamini popote wanapokwenda,kuendelea kuwa vinara katika mitihani yao na kujijengea heshima ya pekee wao na Taifa kwa ujumla.

Bright,Christopher na Cleophas wamemshukuru Rais Dk Samia kwa kuanzisha utaratibu wa kuwafadhili watoto wanaofanya vizuri katika mitihani yao kwamba imekuwa kichocheo cha wanafunzi kujituma na kusoma kwa bidii ili waweze kupata nafasi hiyo.

Nao wazazi wa wanafunzi hao wameishukuru Serikali na Uongozi wa shule za Kaizirege na Kemebos kwa tuzo hizo na ufadhili wa masomo kwa watoto wao huku wakiwashauri wanafunzi wengine kusoma kwa malengo ili kufikia malengo yao ya kupata matokeo mazuri. 

Juliana Maguzu ni mama mzazi wa Anitha amewashauri wanafunzi hao kutobweteka huko waendako kwasababu bado wanayo kazi kubwa mbele yao hapa wamejenga msingi bado kukamilisha nyumba pia akawataka waliobaki hasa madarasa ya mitihani kutambua kuwa bila elimu maisha hayaendi,hivyo wasome kwa bidii.







Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...